Mapenzi, yapo kweli?

TANMO

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
11,463
11,166
Wanajamii kwa mtazamo wangu nimeona kuwa mapenzi kwa sasa yanachanganya sana kiasi kwamba mtu ukifikiria sana unaweza kuibuka na uamuzi kuwa ni bora usijiingize kabisa kwenye huo ulimwengu wa kimapenzi. Utamkuta mwanadada ana mtu ambaye anampenda sana (siku hizi inasemwa anam-feel) huyo ndiye anakuwa dream husband wake wakati huo huo pembeni kuna kibosile anayemtatulia matatizo yake ya kiuchumi, pembeni tena kuna mwingine ambaye anamfikisha vyema kwenye tendo (kwa mujibu wao) wengine wanadiriki humu jamvini kusema kuwa wanapenda kujiexpress lakini si na waume zao (wapo wanaosaidia) n.k n.k n.k……

Tukija kwa upande wa wanaume, utakuta kuna mwanadada ambaye anakuwa anam-feel kiasi cha kumchukulia kama wife wake (kama hawajaoana). Wakati huo huo kuna mwingine kwa ajili ya kumpatia huduma ya mtandao (Wasiliana na Chrispin au Fidel kama hujui hii ni nini) wakati huo huo naye anataka aukemee uzee (kwa mujibu wa Annina), miongoni mwa tetezi wanazotumia mabinti wanaoamua kujiingiza kwenye usagaji ni pamoja na wanaume kutokujali hisia zao, kutokuwa waaminifu, kutowaridhisha vyema kwenye tendo (kwa mujibu wa maelezo niliyopata kwa baadhi yao) n.k n.k n.k…..

Kwa hali hii, wanajamii wenzangu, tunaelekea wapi hasa? Na ni upi mtazamo wako kama mwanajamii mwenzangu, nini hasa kifanyike ili kunusuru kizazi kijacho?
Jiulize...............................................
 
kweli ndugu hyo ishu imekua very serious, cha ajabu ni kwamba inachukuliwa kama kitu cha kawaida kabisa! Huku ni kujidhalilisha ndugu zangu, na ni mwanzo wa kueneza magonjwa hatari kama ukimwi..kwa mtazamo wangu naona hapa hakuna mapenzi bali ni tamaa tu! mapenzi na ngono ni vitu viwili tofauti kabisa..Tunahitaji kubadilika na kujiheshimu, pia kuwaheshimu wapendwa wetu kwa kuwa waaminifu na kuji commit kiukweli!!

amani kwenu.
 
Wanajamii kwa mtazamo wangu nimeona kuwa mapenzi kwa sasa yanachanganya sana kiasi kwamba mtu ukifikiria sana unaweza kuibuka na uamuzi kuwa ni bora usijiingize kabisa kwenye huo ulimwengu wa kimapenzi. Utamkuta mwanadada ana mtu ambaye anampenda sana (siku hizi inasemwa anam-feel) huyo ndiye anakuwa dream husband wake wakati huo huo pembeni kuna kibosile anayemtatulia matatizo yake ya kiuchumi, pembeni tena kuna mwingine ambaye anamfikisha vyema kwenye tendo (kwa mujibu wao) wengine wanadiriki humu jamvini kusema kuwa wanapenda kujiexpress lakini si na waume zao (wapo wanaosaidia) n.k n.k n.k……

Tukija kwa upande wa wanaume, utakuta kuna mwanadada ambaye anakuwa anam-feel kiasi cha kumchukulia kama wife wake (kama hawajaoana). Wakati huo huo kuna mwingine kwa ajili ya kumpatia huduma ya mtandao (Wasiliana na Chrispin au Fidel kama hujui hii ni nini) wakati huo huo naye anataka aukemee uzee (kwa mujibu wa Annina), miongoni mwa tetezi wanazotumia mabinti wanaoamua kujiingiza kwenye usagaji ni pamoja na wanaume kutokujali hisia zao, kutokuwa waaminifu, kutowaridhisha vyema kwenye tendo (kwa mujibu wa maelezo niliyopata kwa baadhi yao) n.k n.k n.k…..

Kwa hali hii, wanajamii wenzangu, tunaelekea wapi hasa? Na ni upi mtazamo wako kama mwanajamii mwenzangu, nini hasa kifanyike ili kunusuru kizazi kijacho?
Jiulize...............................................

Wapo wanaume na wanawake ambao wana ''full package'' ya hizo sababu zinazopelekea watu kuna mpenzi zaidi ya mmoja! Ukimpata huyo mambo tamabarare. Lakini haina maana kwamba usimpopata huyo basi uendekeze vijisababu visivyokuwa na msingi ili ku-justify cheating!
 
seriously, kama unaelewa thamani ya utu wako huwezi fanya huu upumbavu!!
 
mapenzi yapo bwana mkubwa!
unayoyajadili ni ''human weaknesses''
 
jamani tusidanganyane hizi ni siku za mwisho watuwataka tamaa za kila aina wabinafsi wenyekupenda kupenda pesa na mengine mengi ila ktk hayo yote wapo wenye mapenzi ya kweli na ya dhati kabisa na zaidi wenye hofu ya mungu
 
mapenzi yapo bwana mkubwa!
unayoyajadili ni ''human weaknesses''


ni kweli nakubaliana na wewe kuwa mapenzi ya kweli yapo tena wakinadada ndo wanaoweza kuonesha mapenzi ya kweli.
sisi wanaume mara nyingi huwa tunaonesha mapenzi ya kutamani, wanume tunapenda kutokea mdomoni lakini wanawake wanapenda kutokea moyoni.
REMEMBER: When a Woman is walking, She always walk to Communicate...!!!

But when a Man is walking He walks juSt to COVER a Distance...!!!
 
ni kweli nakubaliana na wewe kuwa mapenzi ya kweli yapo tena wakinadada ndo wanaoweza kuonesha mapenzi ya kweli.
sisi wanaume mara nyingi huwa tunaonesha mapenzi ya kutamani, wanume tunapenda kutokea mdomoni lakini wanawake wanapenda kutokea moyoni.
remember: when a woman is walking, she always walk to communicate...!!!

but when a man is walking he walks just to cover a distance...!!!

....mmh!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom