g.n.n
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 407
- 49
Dah bonge la stori mzazi.
Nakumbuka nilipokuwa primary school tena darasa la pili tulikuwa na kale ka tabia ka kiume ka sijui ni kupenda au what ist called but ni kwamba unaweza kuwa una "wachumba" kumi ambao ni wewe peke yako unawaita wachumba maana hata wao wenyewe hawajui wala marafiki zako pia hawajui.
Sasa nilipata binti wa kwanza ambaye aliniita mpenzi nikiwa darasa la sita, stori yenyewe ilikuwa hivi
Kuna kibinti kilihamia shuleni kwetu na darasani kwetu kutoka shule ya jirani, kilikuwa kirembo kiasi chake na nakumbuka niliwahi kukifanyia kituko kikanipeleka kwa mwalimu nikapewa kichapo so nikakichukia fulani hivi. Sasa tulipoingia darasa la sita kikawa kimepata komunio ya kwanza kwenye mwezi wa sita hivi (rc watakuwa wanaijua hii) sasa kawaida huwa wanajipamba sana watoto wa enzi hizo so nakumbuka mama alialikwa kwenye sherehe ya hicho kitoto maana tulikuwa tunakaa jirani (mtaa wa chini na juu) so tukaenda, siku hiyo kile kitoto kikawa karibu sana na mimi tena kikanihonga na keki na kwenye dance kikaja kunifuata.
Sasa kesho yake tukaendelea na shule na nakumbuka tulikuwa tumemaliza mitihani so tukawa na wiki mbili za kucheza sana na kuzagaa nje (wale waliosoma zamani wataikumbuka hii) so kikaja kina rasta zake na ukweli kilikuwa kinaonekana bomba ile mbaya. Mh kwenye boys group ukawa mjadala na ghafla boys wote wakaanza kusema hiki kitoto kizuri na kila mmoja akajiapiza kumpata, i was one of them ila tukakubaliana kuwa atakayempata awaambie wenzake ili wasitishe mawindo.
To make the story short baadae nikajikuta nimebahatika ingawa sikumbuki ku muapproach, dah nakumbuka the whole school knew na tena na ile kura ya nani anatoka na nani ilipopigwa nilikuwa naongoza ingawa sikupewa adhabu maana mwalimu aliyeiitisha nilikuwa nafanya vizuri sana somo lake so tukawa washkaji sana tu so nikapona hilo soo na nafikiri nikawaponyesha na wenzangu wengine.
Mtindo wa mawasiliano ulikuwa simu za mezani, barua kwenye jalada la daftari na baadae washkaji zangu wakanitenga kwasababu walikuwa wanajua mwisho wa siku nitabaki na hako ka binti na washkaji zake wakamtenga so thats how my primary school love was. Ohhhh it ended kwenye kuitana mpenzi tu and nothing else............ na kupeana kadi zilizofutwa majina na kuandikwa la kwangu.
How was your primary school love?