Yupo kibinti kimenipitisha njia moja mara tatu.Kinakwenda Tandika huko na kimepeleka nguo zangu kwa mganga yaani sina hamu.Hivi visister doo mmmmmmmhhhhh hata kuviona sitamani
Mkuu Laigwanan,tatizo jingine la kinamama ni makundi,anatokea mmoja anawambia wenzie 'si mnaona siku hizi baba bishanga hakai tena bar nimemzibiti' , 'kivipi' anaulizwa ,' ah yuko babu mbagala charambe,hatari huyo' baada ya hapo haooooo kwa babu mbagala,na hela yote ya mboga inaishia huko.Kumbe masikini Bishanga kajichokea na mipombe ya kila siku au kipato kimepungua au kisukari kimeanza.
Ndio mkome na kutulia kwa wake zenu ebo!
Niliwahi kusikia siku za nyuma Clouds FM, njia panda... small house moja alimwekea mume wa mtu nyama ya ng'ombe kunako ikulu (kwenye nyeti) kwa siku 7, Ile nyama akachomewa, akapewa. Baada ya siku kadhaa, yule bwana akahamia kwa small house na hata kazini akawa haendi, na mwisho wake akawa kama zuzu, na kazi akafukuzwa,
Mmm! Mungu atustiri na watoto wetu wakiume,mambo kama haya sijui limbwata sijui nini yote yanatokea na yule mwanamke asie jiamini kwa mumewe au mpenzi wake,kama unajituma kisawasawa na mbunifu mzuri wa mambo,kauli nzuri mkarimu kwa umpendae kwengine akafate nini?
Lakini mume akiwa nyumbani unamuliza leo hutoki manake bwana ww kwa mwendo kama tyre gari! au mume yuko nyumbani ww unatoka unakwenda kwa shoga kuongea kuhusu kikao cha harusi,au uko nyumbani ww uko busy na cm sms kwakwenda mbele,mwenzio akimpata anampa Raha ndio unakumbuka shuka kushakucha matokeo yake unaishia kwa babu,babu anakupa dawa anakwambia hii dawa lazima nianze kuiweka hapa kwenye uume wangu niweke huko halafu na wewe ukampe mumeo,yote hayo kwa ujinga wako2.
kabisa nakubaliana na wewe cantalisia watalishwa mpaka nyama za pakaHakuna dawa ya mapenzi duniani jamani, wamama/mabint wanjanja na wanaojua kutumia usanii wa mapenzi cku zote waume/wapenzi wao hawanaga ujanja kbs,kazi yao ni kumsikiliza yf/gf anasemaje na kutekeleza wala hawakumbuki cha hawara wala kimada,polen wenye mahawara mtalishwa mpaka mavi kwa stail hiyo!
Bishanga haya mambo yapo sana na kwenye jamii zetu hizi kudanganyana kwingi sana na wanaamini sana haya mambo ambayo kwa hakika hayasaidii. Na hao waganga ni wadanganyifu sana hawana lolote na hata madawa wanayotoa mengine ni ya uwongo ni miti na maganba tuu wametoa kwenye mti wanakupa kama dawa