nanchi
Member
- Jan 29, 2012
- 66
- 7
Inanisumbua kichwa wadau ;ni kipindi cha zaidi ya miezi tisa nimefahamiana na dada mmoja. Tulikutana arusha nilikenda kumtembelea mama yangu mdogo maeneo ya njiro karibu na chuo.kilicho pelekea kumfaham ni ufamilfrnd walionao ndugu zangu nafamilia yao.naweza kumuita dada kwani ananizid zaid ya miaka 3.wakat wa mazungumzo tulijikuta tunaisha dar tena mtaa mmoja.mara kwa mara akawa ananiambia tupange safari moja wakati wa kurud dar.nikamwambia sawa itakua hivyo.tukapanga kuondoka siku ya juma pili,akasisitiza nisiende kukata tiket bila yeye nikamwambia sawa.ilipofika ijumaa siku mbili kabla ya safari nilimtaka tukakate tiket akanijibu kwenye simu ukifika getini nijulishe, ok kidume nikajiandaa nikajivuta getini kwani ni jirani tu.mwanaume nikaenda hewani nikajibiwa nisubiri.akatoka dada anantandio na ndala mikono nyuma nikajiuliza tunaendaje town kwa dizain hii kimoyomoyo,nashangaa kukabidhiwa bahasha kuchek ndani tiket ya dar xpress nikashukuru na kuondoka kwni nilikua namuogopa bado.jumapili asubuh alinipitia na tax safar ikaanza kwenda stand. Tulipanda bus na kuanza safar kwenda dar.tulipokua njiani kila mmoja alikua muoga kuanzisha story.tulifika mombo tukala tukarud kwenye bus kuendelea na safari.tulifika dar saa kumi na moja tukachukua bajaj kama kawaida ya wana daslam. Tuliondoka had kwangu ninapoishi akapajua then akanielekeza anapo patikana kikaz akaondoka.wkend ilipofika nilienda kumtembelea offn kwake tukastory sana ila alikua akionyesha heshima flani kidume nikatulia tu!ilipofika saa kumi na mbili nikaondoka kwenda hm.kuanzia hapo mara nyingi akawa anapenda kukaa namm,kwa sababu ya shuguli zangu ikawa inashindikana.mara nyingi asubuh ananitumia credit na salamu za mara kwa mara haziishi.imefika sasa mara nying wk end tunatoka pamoja kwenda club na sehem nyingi za starehe na garamanizake. imefikia kumjua demu wangu na kumtaka asiwe na wasiwasi nae juu yangu.na kweli dem wangu hana shida nae kabisa.imefika sasa ananinunulia nguo tena za bei Kali na amekua akiniambia(nakupenda sana kaka yangu)tumekua tukiitana kaka na dada siku zote.isitoshe anajamaa yake huko mwanza na huyo bwana ana mke.tena jamaa yake ananifaham na hana wivu na mm.nimekua naenda hm kwake na anaishi peke yake kama mm,hivyo tumekua tukikaa pamoja nyakati za jioni kama dem wangu yupo chuo.tumekua tukistory kwake had saa sita za usiku.na kuniambia vile anavyo kerwa na kukaa peke yake. Mara nyingi tumekua tukizungumzia mapenz yake na kunitaka kumpa undani wa mapenz yetu yalivyo na tulivyo anza.jumapil ya wk iliyo isha ametoka kuoga na kubadilishia nguo mbele yangu na kuniambia usiogope ni kawaida,dah nilienda mjengo mbaya kwani dada mwenyeme kajaliwa mashalah na mwenyez mungu usiguse.Kwa maana hii nini maana yake? Nisaisieni mawazo mandugu.