Mapato Simba na Yanga kuna kila dalili ya Ufisadi

Songambele

JF-Expert Member
Nov 20, 2007
4,695
2,553
TFF wametoa taarifa ya mapato yaliyopatikana katika mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga kuwa ni TZS 239 millioni na jumla ya watu 52,890walishuhudia mpambano huo wa kukata na shoka. Idadi hii wa watazamaji halingani kabisa na taarifa zote zilizotolewa kuhusiana idadi ya watazamaji.

Lakini ni kwa mara ya kwanza uwanja ulijaa kuliko katika mechi zilizotanguliwa na imani ya watu ni kuona na mapato pia yanavunja rekodi mapaka VIP watu walisimama. Uuzwaji wenyewe wa Tiketi ulikuwa na utata mie nilipata tiketi ya Taifa stars na Cameroun. Vyovyote vile watu wamepiga hela hapa na hesabu ya TFF sio sahihi kwa justification yoyote ile. Sababu ya kusema waliingia watu wengi zaidi kwa TZS 3,000 basi kuna watu zaidi ya 70,000 waliingia uwanjani kwa hiyo kuna idadi ya watu kama 18,000 hawako katika vitabu vya TFF na si chini ya TZS 54,000 hazipo kabisa katika mahesabu.

Kuna haja ya kuchunguza TFF na kujiridhisha kama hakuna ufisadi manake kuna kila dalili kama TFF pia ni chaka la mafisadi. watu wanatengeneza mazingira tata ya tiketi na wanacapitalize. Kwa kuwa hakuna jiwe litakalo achwa bila kugeuzwa basi iwe zamu ya TFF sasa.
 
TFF wametoa taarifa ya mapato yaliyopatikana katika mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga kuwa ni TZS 239 millioni na jumla ya watu 52,890walishuhudia mpambano huo wa kukata na shoka. Idadi hii wa watazamaji halingani kabisa na taarifa zote zilizotolewa kuhusiana idadi ya watazamaji.

Lakini ni kwa mara ya kwanza uwanja ulijaa kuliko katika mechi zilizotanguliwa na imani ya watu ni kuona na mapato pia yanavunja rekodi mapaka VIP watu walisimama. Uuzwaji wenyewe wa Tiketi ulikuwa na utata mie nilipata tiketi ya Taifa stars na Cameroun. Vyovyote vile watu wamepiga hela hapa na hesabu ya TFF sio sahihi kwa justification yoyote ile. Sababu ya kusema waliingia watu wengi zaidi kwa TZS 3,000 basi kuna watu zaidi ya 70,000 waliingia uwanjani kwa hiyo kuna idadi ya watu kama 18,000 hawako katika vitabu vya TFF na si chini ya TZS 54,000 hazipo kabisa katika mahesabu.

Kuna haja ya kuchunguza TFF na kujiridhisha kama hakuna ufisadi manake kuna kila dalili kama TFF pia ni chaka la mafisadi. watu wanatengeneza mazingira tata ya tiketi na wanacapitalize. Kwa kuwa hakuna jiwe litakalo achwa bila kugeuzwa basi iwe zamu ya TFF sasa.

Heshima mbele mkuu Songambele,Hakuna sehemu imejaa Mafisadi kama TFF,pale kuna watu lengo lao ni kuchuma pesa tu na si kuendeleza soka..we fikiria Uwanja ulijaa kiasi kwamba watu wengi tu walikosa nafasi za kukaa(viti),hii haikai akilini hata kidogo,fikiria uwanja una uwezo wa kubeba watu 57,000 wakiwa wamekaa vitini,lakini leo twaambiwa kwamba watu walioingia ni 52,890,sasa inakaaje hii ilhali uwanja ulijaa mpaka watu wengine wakakosa viti,huu ni wizi wa mchana kweupee..Halafu inakuwaje fedha iliyopatikana ni Tshs.million 239 lakini kila timu imepewa Tshs.million 41..Huu si unyonyaji jamani..aaaargh inakera kwa kweli
 
TFF walipata mwanya kuiba pale walipo badilisha ticket zile zenye mihuli ya kiislam.
Wajaleta ticket zingine weeeeeeee hazina hesabu hapo wamekula pasu pasu na watu walivyo jaa vile mpaka sehemu za ngazi watu walikaa wengine walisimama leo eti watu wameingia elfu 52 haiwezekani...
 
Huu jamani ni wizi wa mchana kweupeeee. Hivi huo uwanja bado haujabinafsishwa kwa mbia kuusimamia?? Hatukuwa nao mapato yalikuwa duni na walikwapua bado kupitia njia za makomandooo na wengineo. Leo tuna uwanja wa kisasa ambao ndani ya miaka 2 ukisimamiwa vema tunaondokana na ukwasi katika kuendeleza soka letu nchini.
Tff ni sehemu ya watanzania wengi wababaishajii. Jamani tuna matatizo ya ubabaishaji hatupendi tuu kulijadili kwa mapana. Hatuna rekodi bora ya kuongoza na kusimamia mali zetu kwa uendelevuuuu. Mashirika yote ya umma tuliua ila bado twaleta unafiki yakibinafsishwa.... Beer za kupanga foleni na majina hapo nyuma leo ni historia hakuna sehemu yeyote ya tanzania kuanzia ngazi ya kata haina store ya beer na zipo walau 4products.....

Huo uwanja naupa miaka 4 ya mwanzo kama hatua za makusudi kuusimamia hazichukuliwi tutaona utakavyokuwa na hali mbovuuuuuuuuuuuu....
Tuliahidiwa kupata uwanja na tumepata jambo la nadra sana mwanasiasa wa kitanzania kuahidi na kutekeleza leo hii tunautumia kama sehemu ya wachache kujineemesha...
Haingiii akilini kuuza tiketi za nyuma mechi za wakati huuu... Eti tuliprint nyingi...mfumo wa ligi ya vodacom hakuna kipengele cha tiketiiii......??? (tff hao longo longo zao)

tff sio lolote ni kijiwe cha wasanii na kwa walioko sasa na jamii inayowazunguka hawatafanya wanayotakiwa kwa stahili.
 
simple mathematics:
siti 39,000 kwa shlingi 3000 = 117,000,000/=
na wanasema waliingia watu 52,890 - 39,000 = 13,890 * 10,000 = 138,900,000 + 117,000,000 = 255,900,000/=
haya ni kwa makadirio ya chini sana bila kuzingatia viingio vingine vya juu. hapa maheszabu yanaonyesha kwa watu wa viingilio vya 3000 na 10,000 tu lakini tayari mahesabu yanazidi hayo ya TFF.
kuna harufu ya uchafu hapa!!!
 
na wale makomandoo wa kwenye mageti huwa wanaingiza watu hovyo hovyo bila ticket na hawaelekezi wapi kwa kupata ticket. ukiwa na elf 1 au mbili ukiwapa wanakupeleka mpaka kwenye siti. I saw it live!!!!!!!!!!!!! kuna uchafu sana pale na watu wanapata pesa nyingi bila kuzifanyia kazi.
TFF kwanini mna mlolongo mrefu sana wa watu mnaowaingiza bure??????? why ?????? na mnalalamika sana kuwa hamna hela?????? mmeambiwa na Rais mjiandae kuajiri kocha wenyewe mtaweza ilhali mnachezea opportunities????????
hayo mapato mnayotangaza mnadanganya umma. hamuwezi kuungwa mkono kabisa
 
na wale makomandoo wa kwenye mageti huwa wanaingiza watu hovyo hovyo bila ticket na hawaelekezi wapi kwa kupata ticket. ukiwa na elf 1 au mbili ukiwapa wanakupeleka mpaka kwenye siti. I saw it live!!!!!!!!!!!!! kuna uchafu sana pale na watu wanapata pesa nyingi bila kuzifanyia kazi.
TFF kwanini mna mlolongo mrefu sana wa watu mnaowaingiza bure??????? why ?????? na mnalalamika sana kuwa hamna hela?????? mmeambiwa na Rais mjiandae kuajiri kocha wenyewe mtaweza ilhali mnachezea opportunities????????
hayo mapato mnayotangaza mnadanganya umma. hamuwezi kuungwa mkono kabisa

PCB kama bado ipo functional wangeanzia na hawa TFF, maana sehemu zingine wameshindwa

Ushi wa Rombo
 
Mimi nafikiri mfumo mzima wa ligi ya Tanzania inabidi ubadilike kutoka mfumo huu tulionao wa ridhaa na kwenda mfumo wa kibiashara. Tukifanya hivyo TFF na wadau wengine wa michezo ya miguu wataachana na dhana ya kuzitegemea Yanga na Simba. Mbona Afrika ya Kusini wana klabu mbili kubwa Orlando Pirates na Kaizer Chiefs lakini bado shirikisho lao la michezo linajiendesha bila kuzitegmea klabu hizo. Migogoro katika michezo huwa haiishi lakini tunaweza tukaamua sasa tubadili huu mfumo. Ndio maana Yanga waligoma kuingiza timu kwenye michuano ya Castle sababu kubwa ni hiyo wanajiona kuwa wako wao bila wao na Simba TFF haiwezi kupata kipato ni dhana mbaya sana.
 
Tatizo hata klabu zenyewe viongozi hamna kitu kichwani. mechi yenu inaingiza shilingi milioni 255 kwa dakika tisini tu halafu nyie mlioziingiza mnachopata hakifiki hata nusu yake na mnakubali!!! Ni kwa ujinga kama huu ndio maana klabu best za ulaya ziliamua kujipanga upya na kuwatia jambajamba UEFA hadi wakawaanzishia ligi yenye mapato ya Champions League. Nadhani hata Uingereza walifanya hivyo hivyo. MImi nilidhani kabla hakujakatwa chochote timu zilizocheza zilipaswa kupewa nusu ya hela zote, kwa maana ya Milioni 125 na kwa maana hiyo kila timu kuondoka na angalau Milioni 60 na ushee kibindonindio makato yaanze! hebu fikiria, tiketi za mchezo zimegharibu shs milioni 12,376,260/= halafu gharama za maandalizi ya mechi shilingi milioni 43,358,948/=!!!masikini wachezaji wa Tanzania!
 
Back
Top Bottom