Mapadre kuoa sio dawa ya matatizo - Pengo

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,809
Mapadre kuoa sio dawa ya matatizo - Pengo

Ahoji: Mbona wanandoa wenye watoto, wataalamu wanabaka na kunajisi?
Ataka wasigeuze sakramenti kuwa mali yao

Na Joseph Sabinus 2002

ASKOFU Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amesema licha ya mapadre kuonesha mfano bora wa kuithamini Sakramenti ya Upatanisho, hoja za baadhi ya watu kuwataka waoe ili kuepuka zinaa hazina msingi kwani watu wengine wameoa lakini wanabaka, kunajisi na kulawiti.

Akizungumza wakati wa Ibada ya Alhamisi Kuu, iliyokuwa Sikuku ya Makasisi duniani, Kardinali Pengo alisema makasisi hawana budi kuithamini Sakramenti ya Upatanisho ili waamini waige mfano wao badala ya ilivyo sasa ambapo makasisi wengine hudiriki hata kuwakaripia waamini na wengine kutoa kazi hiyo kwa kulipua.

Katika Ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, Dar es Salaam, ambapo mapadre walirudia ahadi zao za Upadre, Kardinali Pengo aliadhimisha misa ya kubariki mafuta ya wagonjwa, Krisima Takatifu na mafuta ya wakatekumeni.

Alisema baadhi ya makasisi katika Kanisa wamekuwa wakifanya makosa kuipuuzia Sakramenti ya Upatanisho na kwamba hali hiyo imekuwa kikwazo kwa waamini wengine.

Alisisitiza ukweli kuwa, katika Sakramenti ya Ekaristi, Kristo yupo kabisa kabisa kati ya wanadamu na anafika kila mahali kwa kuazima uso na sauti ya kila kuhani na hivyo, makasisi watoe nafasi kwa Kristo kufufuka na kufika kila mahali walipo.

"Ni kweli kabisa Ekaristi humuunganisha Mungu na mwanadamu. Hivyo, haiwezi kumuacha mwanadamu na dhambi kwani dhambi haikai pamoja na Mungu," alisema.

Akaongeza, "Lakini huwezi kupokea Ekaristi bila kuwa tayari. Hivyo, umuhimu wa Sakramenti ya Upatanisho unapuuzwa kwa uzembe na ukali wa kusulubu...ingawaje inapendwa hata na vijana".
Aidha, Kardinali Pengo alisema, "Makosa ambayo tumekuwa tukiyafanya makasisi, ni kwamba baadhi yetu tumekuwa wa kwanza kuipuuuza Sakramenti ya Upatanisho na sasa waamini wameona ikiwa hao wenyewe waliopewa jukumu hilo na Mungu wameipuuza sisi tufanye nini," alisema.

Alihimiza wito wa Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili kwa makasisi kuwa makasisi hawana budi kujenga na kuonesha mfano bora kwa wao wenyewe kuithamini Sakramenti hiyo.
Alisema, "Ni makosa kama mtu atakuja anasema padre nahitaji Sakramenti ya Upatanisho, ukapuuza na kuona kuwa eti labda kuna jambo lingine la muhimu zaidi. Makasisi, sisi wenyewe tuanze kwa kuiandaa Sakaramenti hii kwa moyo wa furaha."

Akisisitiza katika kipengele cha kuipuuza Sakaramenti hiyo, Kardinali Pengo alisema baadhi ya makasisi wamekuwa hawazingatii hali aliyo nayo muumini wakati akiomba Upatanisho.
Alisema, kosa wanalolifanya baadhi ya makasisi ni kuwa wakali kiasi cha kuwafanya waamini waione Sakaramenti ya Upatanisho kama sehemu ya kuongezea mateso, uchungu na kupata hukumu.
"Usimsulibishe muumini mpaka akaona kama Sakramenti ya Upatanisho ni hivi, heri niende hivyo hivyo kwa Mungu na dhambi zangu atanisamehe mwenyewe kwa ukarimu wake," alisema.
Alisema kosa lingine wanalolifanya makasisi hao, ni kutoa maondoleo bila kuridhika vya kutosha kuwa muumini yuko katika hali ya toba ya kweli.

"Wengine wanafanya juu juu tu wakisema eti Mungu mwenyewe anajua. Wanasema umeondolewa dhambi bila kutafakari kama kweli huyu amejiweka tayari," alisema.

Aidha, Kardinali Pengo aliikemea tabia ya baadhi ya makasisi kujiona kama wanaostahili kutwaa mamlaka ya Mungu.
"...Wengine wanafanya kosa la kujifanya kwamba wewe ndiye unayeondoa dhambi kwa nguvu na tamko lako; sivyo. Wewe unamwakilisha Kristo aliye katika mazingira yako," alisema.
Alisema ni wajibu wa makasisi kuwatambua vema waamini wao ili kuwahudumia kulingana na mahitaji ya kila mmoja
"Wengine wanajificha, wengine wanakuja ili kupata nafasi za kueleza shida zao pia, wengine wanakuja kwa nia njema lakini hawajui waseme au wafanye nini. Hali hizo zisitufanye tuone kama ni udhia... lazima tuwe tayari kuwahudumia wote.

Alisema makasisi hawapaswi kuigeuza na kuiona Sakramenti ya Upatanisho kama mali yao binafsi, bali wazingatie kuwa ni mali ya Mungu.

"Tusigeuze Sakramenti hii kuwa yetu, kuwa mahali popote naweza kusema umeondolewa dhambi... Kila mtu ahudumiwe pamoja na mapungufu yake.

Alitaka kila mmoja wa makasisi atambue na kukubali kuwa anafanya kazi kwa nguvu za Mungu.

"Asiwepo anayesema kuwa mimi nisipotamka kwamba umeondolewa dhambi, dhambi zako hazitaondolewa; kama kwamba wewe ni Mungu.
Aidha, katika ibada hiyo iliyohudhuriwa pia na Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Method Kilaini, Kardinali Pengo alisema, makasisi watambue kuwa wanaangaliwa na jamii ya kitaifa na kimataifa hivyo, ni wajibu wao kudumu katika uadilifu na kuepuka vitendo vyote vinavyoweza kushusha heshima ya Kanisa.

"Baadhi yetu mapadre duniani tumefanya vitu ambavyo ni ishara ya dhambi katika ngazi ya juu kabisa. Wengine wamekwisha shitakiwa kwa kubaka, kufanya mapenzi ya ajabu na wavulana hadi kufikia watu kusema ni heri Kanisa liruhusu makasisi wake kuoa," alisema.
Alisema kuwarushu mapadre kuoa sio suluhisho la vitendo hivyo viovu kwa kuwa hata wanataaluma mbalimbali wamekuwa wakisikika kwa kiwango kikubwa kushiriki kwao katika vitendo hivyo licha ya kuwa ni watu wenye wake zao.

Kardinali alitoa mfano wa baadhi ya watu ambao licha ya kuwa na wake zao nyumbani, lakini unashangaa anambaka au kufanya vitu vya ajabu na mtoto wake wa kuzaa" alisema
 
1. Sasa dawa ya kuzini na kubaka kwa Mapadre kama yule Kimaro aliyemfanya vibaya mtoto mdogo wa kiume pale UD ni nini?

2. Kanisa Katoliki kwa vitendo hivi limetupa aibu kubwa watu wote duniani- hata kuwakwaza watu wasio Wakristo kuogopa kuamini Ukristo.

3. Kwa hiyo Pengo anawatetea Mapadre wanoharibu ndoa za watu na kubaka vijana wadogo wakiume? Aibu kweli!
 
Nadhani itasaidia na itapunguza huko kuzidiwa kwao, ambako mara nyingi kunasababisha waanze kufanya hivyo vitendo vibaya.
 
Kumbukeni wale wakuu wa kkkt walipofanya mkutano wa kuruhusu ushoga! Pengine ndiyo dawa.!!!!!!!!!!!!!!
 
Ofcourse Biblia yenyenyewe imesema ni heri kuoa kuliko kuwaka tamaa!!

Hii sakramenti ya ukatoliki ya mapadre kutooa ni unafiki mkubwa! kwani kuoa wanaoa kila siku sema hawaweki hadharani! Yaani hao wanao kutilizwa kama kina Kimaro ni bahati mbaya tu, ila 90 % wako bize sana tu! Na ndo maana hawajamtupa wala kumlaani mwenzao kwani wanajua ni bahati mbaya tu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom