Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Maonyesho ya Maiti Zikijamiiana Nchini Ujerumani
Unaweza kuamini kuwa hili si sanamu ni maiti ya mtu aliyejitolea mwili wake kwa bwana Hagens, Picha zaidi nenda kwenye Photo GalleryThursday, September 17, 2009 8:03 AM
Mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu (Anatomy) wa nchini Ujerumani amezua mjadala mrefu kutokana na maonyesho yake ya maiti za binadamu zikiwa katika staili mbali mbali za kujamiiana. Gunther von Hagens mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu na wanyama (Anatomy) amezua mjadala mrefu nchini humo kutokana na maonyesho yake aliyoyaandaa ya maiti za binadamu zikiwa katika mikao mbali mbali ya staili za ngono.
Hagens anatumia njia aliyoigundua mwenyewe inayojulikana kitaalamu kama "plastination" ambapo maiti hutolewa ngozi yote na kisha majimaji yote kwenye maiti kukaushwa.
Hagens hutumia plastiki zilizotengenezwa kwa madini ya silicon kuziweka maiti hizo katika maumbile mbali mbali kuonyesha maisha ya kila siku ya mwanadamu.
Hagens na mkewe Angelina Whalley wameishafanya maonyesho kama hayo katika sehemu mbali mbali duniani na inakadiriwa watu milioni 27 toka sehemu mbali mbali duniani wameishahudhuria maonyesho yake.
Lakini katika maonyesho yake mapya yanayofunguliwa hivi karibuni Hagens ameamua kuziweka maiti zionekane kama zinajamiiana na kuzua mjadala mkali nchini Ujerumani.
Baadhi ya wanasiasa nchini Ujerumani wamesema kuwa maonyesho hayo hayaonyeshi heshima kwa maiti na wamesema hayakubaliki katika jamii.
Hagens alisema kuwa maiti anazozitumia kwenye kazi zake ni za watu waliojitolea miili yao kwake kabla hajafariki. Hagens aliongeza zaidi kuwa yeye mwenyewe ameishajitolea maiti yake itumike namna hiyo akishafariki.
Hata hivyo baada ya jumba lenye ukumbi ambao angefanya maonyesho yake hayo kukataa maiti zinazoonekana kama zinajamiiana, Hagens alisema kuwa atapeleka maiti zake zingine katika maonyesho hayo zikiwa katika hali tofauti kwa mfano kuna maiti zinazoonekana kama vile zinacheza drafti, soka na mpira wa kikapu. GONGA HAPA KWA PICHA ZA MAITI HIZO
www.nifahamishe.com
Unaweza kuamini kuwa hili si sanamu ni maiti ya mtu aliyejitolea mwili wake kwa bwana Hagens, Picha zaidi nenda kwenye Photo GalleryThursday, September 17, 2009 8:03 AM
Mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu (Anatomy) wa nchini Ujerumani amezua mjadala mrefu kutokana na maonyesho yake ya maiti za binadamu zikiwa katika staili mbali mbali za kujamiiana. Gunther von Hagens mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu na wanyama (Anatomy) amezua mjadala mrefu nchini humo kutokana na maonyesho yake aliyoyaandaa ya maiti za binadamu zikiwa katika mikao mbali mbali ya staili za ngono.
Hagens anatumia njia aliyoigundua mwenyewe inayojulikana kitaalamu kama "plastination" ambapo maiti hutolewa ngozi yote na kisha majimaji yote kwenye maiti kukaushwa.
Hagens hutumia plastiki zilizotengenezwa kwa madini ya silicon kuziweka maiti hizo katika maumbile mbali mbali kuonyesha maisha ya kila siku ya mwanadamu.
Hagens na mkewe Angelina Whalley wameishafanya maonyesho kama hayo katika sehemu mbali mbali duniani na inakadiriwa watu milioni 27 toka sehemu mbali mbali duniani wameishahudhuria maonyesho yake.
Lakini katika maonyesho yake mapya yanayofunguliwa hivi karibuni Hagens ameamua kuziweka maiti zionekane kama zinajamiiana na kuzua mjadala mkali nchini Ujerumani.
Baadhi ya wanasiasa nchini Ujerumani wamesema kuwa maonyesho hayo hayaonyeshi heshima kwa maiti na wamesema hayakubaliki katika jamii.
Hagens alisema kuwa maiti anazozitumia kwenye kazi zake ni za watu waliojitolea miili yao kwake kabla hajafariki. Hagens aliongeza zaidi kuwa yeye mwenyewe ameishajitolea maiti yake itumike namna hiyo akishafariki.
Hata hivyo baada ya jumba lenye ukumbi ambao angefanya maonyesho yake hayo kukataa maiti zinazoonekana kama zinajamiiana, Hagens alisema kuwa atapeleka maiti zake zingine katika maonyesho hayo zikiwa katika hali tofauti kwa mfano kuna maiti zinazoonekana kama vile zinacheza drafti, soka na mpira wa kikapu. GONGA HAPA KWA PICHA ZA MAITI HIZO
www.nifahamishe.com