Maonyesho haya yana maana gani kwetu

Malila

JF-Expert Member
Dec 22, 2007
5,149
4,674
Kuanzia tarehe 1/10/12 mpaka 10/10/12 kutakuwa na maonyesho ya ufugaji wa nyuki pale uwanja wa Nyerere Dar es Salaam. Haya maonyesho yana maana gani kwetu?

Mimi naona ni fursa nzuri ya kuunganisha nguvu zetu ili na sisi tuingie katika fursa hii na kuanzisha usindikaji wa asali. Mzinga mmoja ni Tsh 60,000/( top bar type), ina maana ukiwa na Tsh 300,000/ unakuwa na mizinga mitano.Tukiwa watano hivi ni kwamba tunakuwa na mizinga 25 ya kisasa.

Tunanunua shamba eka kumi kwa sh kama laki nne, na usafirishaji wa mizinga tuweke wastani wa laki mbili. Kununua pro polis kama sh 10,000/. Mzinga mmoja ukitoa debe moja na nusu sawa na lita 30 zidisha na mizinga 25 zidisha na bei la lita moja, Tsh 10,000/

Kila mwaka tunaongeza mizinga mitano mitano, nina hakika baada ya miaka mitano ni lazima tujenge kamtambo ketu.

Nawaomba nyie wenye hela na nafasi ya kwenda porini hamna, leteni hela hizo watu tuingie porini tutoke na nta. Nataka kusema, wewe kama uko b/ze sana na hela unayo, toa tufanyie kazi na wewe tutakupa gawio lako. Vinginevyo Wachina watajenga kiwanga cha pili sisi bado tunabonyeza key board kuilaumu serikali.
 
Good Idea Malila
Nina Maswali mawili matatu naomba unisaidie
1.Kwa mwaka unavuna mara ngapi asali katika mzinga mmoja?
2.Unaponunua Mzinga na kuuweka shambani una uhakika gani wa kupata nyuki?
3. Ni nini kinachowavuta nyuki kwenye mzinga?
4. Ni kila mahali ukiuweka mzinga nyuki watakuja? au kuna maeneo maalumu ambapo kuna uwezekano mkubwa wa kupata
Nyuki?
 
Mkuu heshima

Ni kweli kabisa tutaishia kulaumu Serikali mbona Shoprite wanaagiza Mchicha kutoka South huku wanao laumu wakiwa wamekaa ofisini tu kwenye AC
 
Good Idea Malila
Nina Maswali mawili matatu naomba unisaidie
1.Kwa mwaka unavuna mara ngapi asali katika mzinga mmoja?
2.Unaponunua Mzinga na kuuweka shambani una uhakika gani wa kupata nyuki?
3. Ni nini kinachowavuta nyuki kwenye mzinga?
4. Ni kila mahali ukiuweka mzinga nyuki watakuja? au kuna maeneo maalumu ambapo kuna uwezekano mkubwa wa kupata
Nyuki?

Kwa maeneo mengi mzinga wa nyuki unavunwa mara mbili kwa mwaka, lakini kuna maeneo unaweza kuvuna kila baada ya miezi mitatu. Kiasi cha asali kinategemea sana size ya mzinga, uwingi wa maua na ukubwa wa kundi la nyuki. Kwanza ni lazima kuwepo dalili chanya za kuwepo nyuki au makundi ya nyuki karibu na maeneo unayotaka kuweka mizinga yako, ukishapata uhakika huo, kuna kitu kinaitwa pro polis hupakwa ndani ya mzinga kuvutia nyuki, na wengine hutumia nta ya nyuki kupaka ndani ya mzinga, njia ya tatu ni kutegemea de-swarming kutoka ktk mizinga ya jirani.Hizi ni njia za kawaida kwa wafugaji wengi.

Kama nilivyosema, pro polis au deswarming ndio njia za asili zinazofanya nyuki wakaingia ktk mzinga mpya, lakini pia hali ya hewa ikiwa mbaya inaweza kuchangia nyuki kuhamia ktk mzinga/mazingira salama.

Si kila sehemu unaweza kufugia nyuki kwa ajili ya asali, kuna maeneo yenye vivutio kwa nyuki na huko ni rahisi zaidi kuwapata kwa ajili ya mizinga mipya. Nyuki pia hupenda mahali salama ili waweze kujenga koloni lao vizuri, sehemu hatarishi kwao kunapelekea nyuki kuhama mzinga. Ila nyuki wanaweza kuishi sehemu kubwa sana ya mazingira yetu ili mradi kuwe na chakula chao cha kutosha.
 
kwenye huu mkutano nitakuwepo nataka nipate uzoefu wa biashara hii ya fuata nyuki ule asali...nilipata taarifa zake ni biashara nzuri na inayolipa hasahasa kama ukipeleka mzigo nje.,lakini haya maonyesho yatakuwa ni mwanga wa kujua zaidi juu ya biashara hii ya nyuki na asali
 
kwenye huu mkutano nitakuwepo nataka nipate uzoefu wa biashara hii ya fuata nyuki ule asali...nilipata taarifa zake ni biashara nzuri na inayolipa hasahasa kama ukipeleka mzigo nje.,lakini haya maonyesho yatakuwa ni mwanga wa kujua zaidi juu ya biashara hii ya nyuki na asali

natamani sana nishiriki japo siku moja. Kama utashiriki jitahidi upate anuani za watengeneza mashine za kuchuja asali zile ndogo.
 
Malila,

Naomba ainisha changamoto kwanza tujue hizo risk zilizopo.

Niliahidi kuleta changamoto za uwekezaji ktk ufugaji nyuki, ni kama zifuatazo;

1. Changamoto ya kwanza ni ubora wa asali sawa na soko la kimataifa, wengi hawajui asali bora itapatikana vipi na wapi,wateja wa kimataifa hawataki asali yenye chembe za madawa ya kuulia wadudu mashambani, kwa hiyo usifuge nyuki ktk maeneo yenye uwezekano wa nyuki kutumia maua yenye mabaki ya dawa hizo.

2. Ukame, ukame ukitokea unaathiri sana uzalishaji, na wakati mwingine nyuki huhama na mizinga yako ikakaa muda mrefu bila nyuki.

3. Moto, moto huharibu makazi ya nyuki, ni lazima kuzungushia firebreak kama unafugia porini, kwa wale wanaofuga ktk vibanda tatizo hili laweza kupungua kidogo.

4. Paka pori/siafu huharibu sana makazi ya nyuki na kufanya nyuki kuhama. Kuna njia za kudhibiti uharibifu huu kitalaamu.

5. Vibaka, upo wizi wakati wa msimu wa uvunaji, au wizi wa mizinga, mzinga mmoja sasa hivi wenye nyuki si chini ya Tsh 50,000/ kwa hiyo vibaka wanaweza kuiba kwa lengo la kuuza au kupata asali, hapa suluhisho ni kupata mbia anayeishi karibu na shamba lako.

6. Usindikaji/packaging, ni lazima asali isindikwe vizuri na ihifadhiwe vizuri tayari kwa kuuzwa.

7. Gharama za mizinga, mizinga bora huhitaji mbao, sehemu zinazofaa kwa ufugaji wa nyuki hakuna mbao, au mbao ni ghari sana. Suluhu hapa ni kushirikiana ili kupunguza gharama.


Changamoto hizi zinamalizwa zaidi na uchaguzi sahihi wa sehemu ya kufugia nyuki wako. Mtalaamu mmoja aliniambia ili nifanikiwe ktk kufuga nyuki ni vizuri niungane na mfugaji mwenyeji ili yy atoe " site nzuri" na nitumie mizinga yake ya kienyeji kupata makoloni ya nyuki na mimi nimpe mizinga ya kisasa. Hapo suala la ulinzi/management na usalama wa shamba letu utakuwa mzuri.Yaani mbinu shirikishi, halafu wote wawili tunatoka kiulainiiiii.
 
Mkuu mleta mada,

Naomba na mimi nichangie japo kwa uchache kuhusu ufugaji nyuki. Mimi sio mtaalam ila niko "interested" na eneo hili kama shughuli mojawapo ya kujipatia kipato. Kiufupi ufugaji nyuki ni fursa ambayo ipo katika maeneo mengi nchini lakini haijatumika.

Umechanganua mengi ila niongezee tu kuwa katika ununuzi wa mizinga pia kuna aina nyingine ya mizinga "commercial beehives" ambayo hii pia ni mizuri kama unaplan kufanya shughuli hii kibiashara. Mizinga hii ni mikubwa (inabebanishwa) na ina uwezo wa kutoa 40lts za asali. Faida yake ni kwamba malkia na sehemu ya mazalia wametanganishwa hivyo sehemu inayovunwa ni sehemu ya juu (mizinga ya juu), hii hupelekea kuimarisha kundi na kutoa muda mchache wa utengenezaji asali baada ya kuvuna. Kwa uzoefu wangu mdogo katika eneo nililopo uzalishaji asali kwa top bar hives ni kati ya 15lts na 23lts kutegemeana na dimension ya mzinga / uimara wa kundi / eneo la ufugaji.

Kila la kheri.
 
Mkuu mleta mada,

Naomba na mimi nichangie japo kwa uchache kuhusu ufugaji nyuki. Mimi sio mtaalam ila niko "interested" na eneo hili kama shughuli mojawapo ya kujipatia kipato. Kiufupi ufugaji nyuki ni fursa ambayo ipo katika maeneo mengi nchini lakini haijatumika.

Umechanganua mengi ila niongezee tu kuwa katika ununuzi wa mizinga pia kuna aina nyingine ya mizinga "commercial beehives" ambayo hii pia ni mizuri kama unaplan kufanya shughuli hii kibiashara. Mizinga hii ni mikubwa (inabebanishwa) na ina uwezo wa kutoa 40lts za asali. Faida yake ni kwamba malkia na sehemu ya mazalia wametanganishwa hivyo sehemu inayovunwa ni sehemu ya juu (mizinga ya juu), hii hupelekea kuimarisha kundi na kutoa muda mchache wa utengenezaji asali baada ya kuvuna. Kwa uzoefu wangu mdogo katika eneo nililopo uzalishaji asali kwa top bar hives ni kati ya 15lts na 23lts kutegemeana na dimension ya mzinga / uimara wa kundi / eneo la ufugaji.

Kila la kheri.
Mkuu Asante kwa much angina maada hii.
 
Mkuu Malila hii project ya bee keeping ilifanikiwa???
Tunaomba mrejesho mkuu, japo tuwe motivated kuingia porini kusaka niti.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Malila hii project ya bee keeping ilifanikiwa???
Tunaomba mrejesho mkuu, japo tuwe motivated kuingia porini kusaka niti.

Nimefanikiwa mwaka huu baada ya kupata location ambako naweza kupata asali nyeupe, nimeshapeleka mizinga 35,ili niingie sokoni na brand ya asali nyeupe, asali nyeupe ni adimu kidogo.

Mizinga yangu ilikaa miaka miwili bila kutundikwa shambani sababu ya kukwepa uharibifu wa mizinga na wizi, ila sasa kiroho kiko safi, plan ni kufikisha mizinga 500 by 2016 ktk location hiyo niliyopata. Na kwingine kwenye asali ya kawaida niwe na mizinga 500 pia by 2016.
 
Nimefanikiwa mwaka huu baada ya kupata location ambako naweza kupata asali nyeupe, nimeshapeleka mizinga 35,ili niingie sokoni na brand ya asali nyeupe, asali nyeupe ni adimu kidogo.

Mizinga yangu ilikaa miaka miwili bila kutundikwa shambani sababu ya kukwepa uharibifu wa mizinga na wizi, ila sasa kiroho kiko safi, plan ni kufikisha mizinga 500 by 2016 ktk location hiyo niliyopata. Na kwingine kwenye asali ya kawaida niwe na mizinga 500 pia by 2016.


Mkuu malila nitakutafuta kwa fujo, kuna kitu namalizia hapa, mungu akijalia by 2016 nahisi tutakua pa1...
 
Back
Top Bottom