Maoni yangu dhidi ya "Baadhi ya wananchi wahuni" wa Arusha kujaribu kuzuia wanahabari wa TBC

Kwa mtazamo wangu waliofanya hivyo wapo sahihi kabisa kwa hicho ni chombo kinachoendeshwa na kodi za watanzania. Kweli tbc kwa sasa inaboa sana. Wapo kimasilahi sana.
 
Dotto, ulikuwa wapi muda wote huu? Nimefurahishwa sana na hitimisho lako ama kweli wewe ni think tank, kama kuna mtu atashindwa kukubali kwa hiyo post ya mwisho basi huyo ni mahututi wa mawazo. Nakushauri ujiunge na chadema wewe ni asset muhimu sana pale bungeni. Good to go utafika mbali sana ukiendelea kuwa visionary wa sina hii.
 
tumsameejamani coz yeye anaitwa Doto nafikiri kurwa wake atakua na akiri kwani mapacha wazaliwapo mmoja lazima awe mjinga na nadhan huyu doto ndio anamatatizo.
 
Dotto, ulikuwa wapi muda wote huu? Nimefurahishwa sana na hitimisho lako ama kweli wewe ni think tank, kama kuna mtu atashindwa kukubali kwa hiyo post ya mwisho basi huyo ni mahututi wa mawazo. Nakushauri ujiunge na chadema wewe ni asset muhimu sana pale bungeni. Good to go utafika mbali sana ukiendelea kuwa visionary wa sina hii.

si umesema umefunga mjadala mbona unarudi kwa ID nyingine?
 
R.I.P TBC. Kwa kweli toka mtaaluma TIDO alipoondoka naona hiki chombo kinaelekea kuleeeeee TVT. Taarifa kukatika katika, vipind vingi vimechachuliwa kama "Usiku wa habari". Jenerali ulimwengu aliwahi sema "Kama wewe ni mwandishi wa habari unaetumia weledi wako, huna budi wa kuweke picha yako na Jina kamili. Don hide bro. Nyie saizi mmekuwa zaidi ya wanafiki. I hate TBC.
 
Soma vizuri maelezo acha kupindisha maelezo yangu.

Fikia kwa kutumia kichwa na sio makalio.Kwani CDM ndiyo hawaipendi TBC?.Siku zote unauma, tuliwaona Arumeru mkifanya covarage ya CCM kwani TLP,SAU na wengine hamkuwaona..TBC na CCM yenu sawa ila ni haramu kwa vyama vingine..Hilo shirika linaongozwa na kodi zetu kwa hiyo ni ya Watanzania wote na sio ya TBC peke yake. Ukiona unakosolewa inakubidi ujue tatizo liko na limeanzia wapi.Acha kukurupuka...
 
Unaongea kama vile wewe ndiye msemaji boss wa TBC tatizo hii nchi kila mtu msemaji si shangai kauli zako
 
"Wananchi Wahuni". Kimsingi Dotto we ni wale wasiojua wanachokifanya hasa kwa kuangalia upande mmoja. Kumbuka KAZI ZETU ZA TBC hass kwenye chaguzi zinavyo kuwa za upendeleo. Niliona siku moja, katika uchagunzi wa Arumeru Mashariki TBC ilikuwa ya CCM na CCM ya TBC hata ikakosewa taarifa ya habari kwa kuweka mgombea wa CDM badala ya wa CCM. Sijui wakubwa wenu wanawapa nini???????????????????????????????
 
Pamoja na changamoto zinazoikabili tasnia ya habari nchini bado watanzania wanapaswa kuheshimu na kuthamini huduma ambayo wote tunajua mazingira yalivyo si tu Tanzania lakini bara zima la Afrika linapokuja suala la Uhuru wa vyombo vya habari. Kitendo kilichoripotiwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa, baadhi ya wakazi wa jiji la Arusha ambao kwangu nawaona ni "wakazi wahuni" kujaribu kuwazuia waandishi kutoka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kufanya kazi yao kwa kigezo kuwa wanatoa taarifa za kupotosha hazina msingi na walipaswa kutafuta njia nyingine ya kuonyesha kwao kutoridhishwa na utendaji wa shirika hilo. Nachelewa kusema kuwa tabia iliyoanzishwa na baadhi ya wafuasi wa CHADEMA kuwaona kila wasio waunga mkono ni wasaliti haifai na wala haileti picha ya uvumilivu wa kisiasi ambao tungetarajia kuuona ukihubiriwa kwa vitendo na yoyote anajipambanisha na chama au jumuiya makini.

NB: Huu ni mtazamo wangu binafsi kama mwanahabari, wala hakuna mahusiano na itikadi au maslahi ya shirika lolote.

Kwa tulikofikia hakuna haja ya kupoteza muda.. Kuna haja gani ya mwandishi kukuomba utoe maoni ambayo mwishowe wanaishia kupotosha tu.

Hawa dawa yao ni kuwakimbiza tu.
 
boya kweli kweli, we unafurahishwa na hiyo tanzania biased corperation, ngoja anguko lenu linakuja
 
Mkuu mi sipo hapa kujadili habari zinazoletwa na TBC, na wala siko hapa kulitetea shirika hilo maana hiyo si kazi yangu na wala sihusiki. Inawezekana nimetumia kauli iliyowaudhi wengi lakini hii hainifanyi niwe mdogo na kukubali matusi yanayoletwa kishabiki. Mimi ni binadamu, nina hisia na pia sio malaika hivyo kama mtu akinilitea maneno ya Kunya na mimi nayajua. This is where we dare to speak openly, nimeyapokea matusi yote bila jazba na wenzangu nao wayapokee ya kwangu kwa mikono miwili.

Ebu tuambie ndugu
 
Mkuu mi sipo hapa kujadili habari zinazoletwa na TBC, na wala siko hapa kulitetea shirika hilo maana hiyo si kazi yangu na wala sihusiki. Inawezekana nimetumia kauli iliyowaudhi wengi lakini hii hainifanyi niwe mdogo na kukubali matusi yanayoletwa kishabiki. Mimi ni binadamu, nina hisia na pia sio malaika hivyo kama mtu akinilitea maneno ya Kunya na mimi nayajua. This is where we dare to speak openly, nimeyapokea matusi yote bila jazba na wenzangu nao wayapokee ya kwangu kwa mikono miwili.

Ebu tuambie ndugu wangetumia njia gani?
 
Dotto, baada ya kusoma kwa makini hoja yako, nimegundua maneno matatu kama ifuatavyo:

Kwanza, kama kweli wewe ni mwandishi wa habari ulivyojitambulisha, basi utakuwa kanjanja. Nasema hivyo kwa sababu nimegundua uelewa wako wa mambo yanayotokea duniani ni mdogo kupita kiasi hata kile kinachotakiwa kwa mwana habari mwanafunzi. Haihitajiki darubini kupima na kuelewa kwamba TBC ni shirika la umma linalogharamiwa kwa kodi ya wote bila kujali itikadi, dini wala jinsia za watz.

Kwa mukhtadha huo, chombo hicho kinapaswa na hakika kinawajibika kuwa fair kwa wote bila kujali dini wala itikadi. Lakini ukweli ni kinyume chake inapofikia suala la kuripoti habari za CCM na vyama vingine vya upinzani. TBC hujikuta wakiripoti habari za CCM kama ilivyotakiwa kuripoti Radio au gazeti la Uhuru ambavyo ni vyombo vya propaganda vya CCM

Tema hali imekuwa mbaya zaidi baada ya Clement Mshana kurejea TBC kama Mkurugenzi. Ukereketwa na uelewa mdogo wa Mshana ulidhihirika kwa kipindi kifupi alichokaa Idara ya Habari Maelezo ambapo alitumiwa na CCM na serikali yake kujaribu kudhibiti uhuru wa vyombo vya habari kwa kuviandikia barua za onyo, karipi au kusudio la kuvichukulia hatua magazeti yaliyoripoti habari za ukweli ambazo hazikuwafurahisha watawala. Yaliyotokea utakuwa unayajua kama kweli wewe ni mwandishi wa habari.

Jambo la pili nililogundua ni kwamba uwezo wako wa kujenga hoja ni mdogo. Haki siku zote huenda pamoja na wajibu. Je, kama waandishi wa habari wa TBC wana haki ya kuhudhuria na kuripoti habari za makundi yote katika jamii, basi pia wanayo wajibu wa kuzingatia taaluma, ukweli na ueledi katika utendaji wao. Wasitumike na CCM, Chadema, TLP, NRA, NCCR-Mageuzi...........nk.

Tatu na mwisho, kwani ni lazima waandishi wa habari wafuatilie na kuripoti habari kutoka kwa source asiyewahitaji. Kwanini TBC wang'ang'anie kwenda kwenye matukio ya Chadema wakati wahusika hawawahitaji? Lazima wawe na hila iliyojificha, nalo siyo lingine bali 'KUWALIMA' kwenye story

Nakushauri usionyeshe uwezo wako mdogo au mishiko unayopata kutoka CCM kupitia kwa bosi wako anayekufundisha kazi (kutoka moja ya vituo vya Tv nchini) ambaye ni roboti ya kufanikisha baadhi ya mapenzi ya wana CCM kudhalilisha fani ya habari kwa kuleta jamvini hoja zisizo na mashiko. TBC waache kulazimisha kuhudhuria matukio wasiyotakiwa wala kualikwa, habari ziko tele siyo lazima za Chadema. Kuna vyama zaidi ya 17 vya siasa nchini na kingine kipya kiko njiani wacave huko.
 
Back
Top Bottom