MAONI ya Upinzani Bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais; Muungano; A MUST READ

Ukiisoma hotuba mwanzoni utaona amewatetea WZN kuwa kuna mambo hayakuwemo katika mkataba.Ametaja machache na kusema yaliongezwa kimakosa. Yote aliyosema ni yale yanayowagusa WZNZ kwahiyo ametetea Tanganyika kwa kutumia shule. Ana maana basi tuondoe hayo ya ziada yanayowasaidia wao.

Halafu kaongelea kuwa kuna amiri jeshi wa vikosi maalumu. Vikosi hivyo ni vya ulinzi na usalama. Hapa ana maana ZNZ ina jeshi linalohudumiwa na Tanganyika na kama ni hivyo kwanini wao wasibebe mzigo wa vyombo vyao vya usalama?

Halafu kuna mahali kasema Tanganyika irudi ili tuwe sawa katika muungano. Kwamba kile walicho nacho WZNZ Watanganyika wawe na chao. Hapa ana maana Tanganyika iwe na uwezo wa kuwaambia WZNZ mnaweka nini mezani katika mambo kama elimu, usalama na ulinzi, ardhi, ajira na biashara.

Kwa muktadha huo Tanganyika itakuwa na uwezo wa kusema hakuna ruzuku kutoka Hazina za asilimia 7, tunafanya biashara lipeni umeme, kwa vile hamtaki watu wapate ajira kwenu basi na wakwenu hawapati kwetu n.k.
Tanganyika itauliza kama Mtanganyika anakwenda ZNZ kama mwekezaji basi na MZNZ aje kama mwekezaji.

Nilisema kama kuna karata mbovu waliocheza WZNZ ni hii ya kutaka Tanganyika irudi.
Hili litawasaidia sana WZNZ kujitoa na kuwa kama Malaysia au Dubai kama anavyodai Ahmed Rajabu!!!!

Amesema kitaalam kuwa iwepo kura ya maoni kwa Watanzania. Ukisoma kwa umakini hakusema ZNZ lakini ametolea mifano kama ya Sudan kusini, Eritria n.k kwa ufundi. Hapa ana maana moja, WZNZ wapewe nafasi ya kura ya maoni.

Halafu anasema kama watakubali muungano basi iamuliwe ni wa aina gani. Wakati huo huo amesema Tanganyika irudi.
Mtoa mada ameondoa uwezekano wa mkataba, serikali 3 au mahusiano kwasababu kila nchi itataka kujua itafaidika na nini katika hayo mahusiano. Definite Tanganyika itauliza wenzetu mna nini cha kuchanga na sisi?

Nina uhakika wabunge wote wa Tanganyika bila kujali itikadi zao wanakubaliana na hoja za Lissu.
Siku kama ya leo kama kuna watu wanahofu na hatima yao katika muungano ni wananchi wa kawaida wa ZNZ si wananchi wa Tanganyika.

LET ZNZ GO!
 
...QUOTE...
[Mheshimiwa Spika,

Kama ilivyo kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba katika mazingira ambayo upande mmoja wa Muungano umejitangazia uhuru kama ambavyo tumeonyesha hapa, huu ni wakati muafaka kuanzishwa tena kwa Serikali ya Tanganyika.

Katika mazingira ambayo upande mmoja wa Muungano sio tu una Serikali kamili, Bunge kamili, Mahakama kamili, wimbo wa taifa, bendera ya taifa, na sasa una nchi kamili yenye mipaka na eneo la bahari linalojulikana, una majeshi yake na Amiri Jeshi Mkuu wake, huu ni muda mzuri kwa Serikali ya Tanganyika kuzaliwa upya. Katika mazingira kama haya, Mheshimiwa Spika, upande wa pili wa Muungano unatakiwa kuwa na vitu vyote hivyo pia ili uweze kujadiliana na upande wa kwanza katika hali ya usawa.

Huu ni wakati wa kurudishwa tena kwa Serikali ya Tanganyika kama ilivyopendekezwa na Tume ya Rais ya Chama Kimoja au Vyama vingi mwaka 1991 na Tume ya Kissanga mwaka 1998, na kama ilivyopendekezwa na Kundi la Wabunge 55 wa Bunge hili tukufu na kuungwa mkono na Serikali ya Rais Ali Hassan Mwinyi kabla ya hoja hiyo kutunguliwa na Baba wa Taifa mwaka 1993!]
....QUOTE...

My Take: Hio Quote hapo juu kutoka katika Hotuba ya Lissu, inanifanya nianze ku-connect dots toka kwenye last thread ya member anaeitwa HUTAKI UNAACHA humu jamvini, Kwamba Rais Kikwete alikutana na Mbowe(M/kiti Chadema), Kwamba tume ya Jaji Warioba hatimaye itapendekeza kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika na itapitishwa hio 2015, Kwamba Rais Shein ataendelea kuongoza SMZ kama Rais hio 2015, Kwamba Lowassa atakuwa Rais wa Muungano hio 2015, Kwamba Dr.Slaa atakuwa Rais wa Serikali ya Tanganyika ambayo haina maamuzi hio 2015.....Just my thought...




Kamanda umetafuta hoja yako kisha ukaamua kuijengea hoja, kisha ukahitimisha. Kama ulivyosema...just ure thought. Pole kwa kuzungumzia/kuunganisha kitu kimoja kilichopo na kingine kisichokuwepo.
 
Back
Top Bottom