Maoni ya Mh. Zitto Kabwe juu ya kuondoa mgawo wa umeme

Zitto katoa hoja yake na kaijenga; jukumu la wengine wasiokubaliana naye ni kuonesha mapungufu ya hoja hiyo pasipo ulazima wa kumuita majina mbalimbali kwani kwa kuitana majina hakuthibishi nguvu ya hoja bali udhaifu wake. Je, hoja ya Zitto ina nguvu kiasi gani au ina upungufu kiasi gani? Kusema "Zitto hana credibility" haisemi lolote juu ya uzito wa hoja yake. Hoja hujibiwa kwa hoja.
 
Zitto katoa hoja yake na kaijenga; jukumu la wengine wasiokubaliana naye ni kuonesha mapungufu ya hoja hiyo pasipo ulazima wa kumuita majina mbalimbali kwani kwa kuitana majina hakuthibishi nguvu ya hoja bali udhaifu wake. Je, hoja ya Zitto ina nguvu kiasi gani au ina upungufu kiasi gani? Kusema "Zitto hana credibility" haisemi lolote juu ya uzito wa hoja yake. Hoja hujibiwa kwa hoja.

Mkuu ukiona watu wamefika hapo ujue kuwa walikuwa na matumaini makubwa sana juu yake, lakini baadae wakaona anaanza kuwaacha na kulekea katika mwelekeo tofauti, hata baada ya kujaribu kwenda naye hoja kwa hoja, wakaona imekuwa ni kazi bure kwani mtu sasa anaangalia zaidi kesho yake badala ya jamii iliyopana aliyodai awali anaipigania.
Hali ikifika katika hatua hiyo hapo mtu hata aongee vipi ataishia kubezwa tu, kwani kila afanyalo ni kucheza na au kuchezea akili za watu.
So mkuu acha tu watu wajipatie psycho therapy kwa kumpuuza, hiyo itasaidia kupunguza matokeo mabaya ya hasira za watu baada ya kuhisi wamesalitiwa.
 
issue kubwa pia ni mzigo wa bei anaotupiwa mwananchi hata kama ni dharura,upo umuhimu wa kuhusisha wataalumu ya fani tofauti kutafiti na kushauri namna ya ku balance uchumi ktk mazingara tuliyonayo sasa.
 
mfano ni juzi tu tumeshusha bei ya mafuta huku shilingi ikaanguka mno kufikia Tsh 1620/usd! While movement za currency yetu kuna mkono direct wa BOT through devaluation policy! Tutumie vizuri wataalamu wetu jamani.
 
natumia simu ndo maana naandika post fupi ila maoni yangu si upatikanaji wa umeme in short and long term tu bali pia kubalance uchumi watu wasiumie mno kama huu usanii wa mafuta bei kupanda kisa tsh kuporomoka!
 
Kuna mapungufu nayaona katika mpango mzima. Ukuaji wa matumizi ya umeme kwa mwaka ni 15%. Tunaambiwa kuna mkakati wa dharura kuondoa upungufu na utakamilika mwaka 2012. Kuna short term plan ambayo ndiyo aliyoitaja na sina uhakika ikifika 2012 itabidi tuwe na plan ya dharura tena!

Katika long term plan(kama ndiyo) ni pamoja na kuiwezesha Kiwira na hapo hapo ameshauri kuwepo na PPP ili kupata umeme haraka na tusisubiri. Nadhani hii inakuwa ni short term plan pia ingawaje inaonekana kama long term palan

Muda wa miaka miwili ukiisha mashirika yaliyoleta mitambo bado yatataka uhaba ili yaendelee kufanya kazi. Hapo tunaweza kusikia mgao usio na maelezo kujenga mazingira mazuri ya kazi. Unajua unapokuwa na funeral home kuna wakati unaomba watu wafariki ili business iendelee. Hata kama hatukubali huu ndio ukweli, sasa nikishawishiwa kuwa hayo mashirika yatang'oa mitambo na si kujenga mazingira ya upungufu nabaki niki tweta.

Mipango ya dharura ya umeme imekuwa jambo la kawaida tangu JK aingie madarakani na nashangaa kwanini inaitwa dharura. Tulikuwa na Richmond, Songas, Dowans, Aggreko n.k na dharura haijaisha hadi leo.
Hizo trilioni 1.2 ni sehemu tu ya mapesa yaliyopotea kwa mipango ya dharura ambayo si dharura ni ya kawaida na giza lipo pale pale.

Kama tuna 1.2 trilion za kukopa tumeshindwa vipi kukopa ili tujenge Stiegler gorge itakayotupa umeme wa uhakika kama kidatu, mtera, pangani, nyumba ya mungu? Ni kiasi gani ukiongeza na trilion 1.2 zimetumika kwa umeme wa dharura na tungeweza kujenga hydro dam ngapi!

Sioni sustainable project, ninachokiona ni ' budget ipite project'. Tutaishi kwa mipango ya dharura hadi lini? na kama taifa dharura ndiyo ukomo wetu wa mipango na kufikiri. Sijui lini tutajifunza kufikiri mbele ya wakati.
 
Tatizo letu hapa Tz ni kuwa na viongozi na wanasiasa wenye upeo mdogo sana. Sijui ni kwanini serikali na washauri wake wote wanaona njia ya kuondoa mgao ni kuwekeza kwenye miradi midogo midogo ya 400MW? Kwa mtindo huu, hata Rais atakaye ingia baada ya JK tatizo lake la kwanza litakuwa umeme!!! Ni kipofu tu asiyeweza kuona hili.

Nini kinaitajika kufanywa?

Kwa sababu taifa limepata tatizo la umeme kwa miaka 20 sasa, basi tutekeleze miradi mikubwa itakayokidhi mahitaji yetu ya miaka mingi ijayo. Miradi ya kuzalisha kama megawati 4000! Yes i mean 4000MW. Ukiangalia hizo pesa tunazotumia kwenye dhalura kila mwaka zinatutosha kutekeleza miradi mikubwa kama hiyo. Nasikitika kusikia tutatumia 1.2trion na mwisho wa siku tutapata 450MW. Kizazi kijacho kitatulaani kwa maamuzi mengi ya sasa!

TAFAKARI!
Kayumba!
Hapo kwenye red sijakuelewa. Unasemaje? Umefanya utafiti gani ukagundua kuwa ni hivyo, au akili yako imechanganywa ikawa inaona the opposite? Sasa nikupe siri: fanya hivi: tafuta ofisi yoyote ambayo ina maandishi haya: "Eneo hli hatupokei Rushwa", halafu jidai unahitaji huduma ya msingi sana pale, kama unaweza, au jaribu kupeleleza hali pale ikoje. Ukipata jibu, tumia the same principle ku-iconfirm hiyo stataement yako hapo juu, kama iko sahaihi au la. Ila kwa kukusaidia tu ni kwmba wewe ndiyo upeo wako ni mdogo. Hakuna mtu yeyote mwenye upeo mdogo ndani ya system yetu, na kama wangekuwepo, tungekuwa tuko mbali sana sasa hivi kimaendeleo, sababu angalau vitu vingine tungekuwa tunafanya kwa kubahatisha halafu tunajikuta tumepatia kwa bahati mbaya. System ikiwa corrupt halafu ikiwa na watu ambao ni wajanja, vitakosewa vitu vyote kwa makusudi, na hakuna hata kimoja ambacho mnaweza mkajikuta mmepatia walau kwa bahati mbaya. halafu mliolala usingizi manasituka na kuanza kubwabwaja "upeo mdogo". Watu wamesoma kabla yako halafu wewe unadanganyika kirahisi namna hii?
 
Back
Top Bottom