Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Maonesho ya kimataifa ya Dar, sabasaba 2010 yanategemewa kufunguliwa tarehe 28 Juni 2010. Nimekuwa na kawaida ya kutembelea maonesho hayo huko nyuma lakini nakatishwa tamaa na baadhi ya bidhaa zinazokuwepo pale. Yaani watu wengine wanaleta zile takataka za Kariakoo na kuweka kwenye mabanda yao. Hata hivyo kuna makampuni yanakuwa na vitu vya maana. Mfano, mwaka jana (2009) nilifurahishwa na banda la Wizara ya Maliasili na Utalii. Walikuwa na vitu vizuri sana kwa watu wengi ambao hawana nafasi ya kwenda mbugani. Wanyama wazuri sana waliletwa kwenye banda lao.
Naomba mwenye kuona kitu ambacho wadau tunaweza kufaidi atujuvye. Niko mbali kidogo lakini week ijayo lazima niwapeleke vijana wakashangae shangae kidogo!
Naomba mwenye kuona kitu ambacho wadau tunaweza kufaidi atujuvye. Niko mbali kidogo lakini week ijayo lazima niwapeleke vijana wakashangae shangae kidogo!