Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,488
- 86,004
MUNGU Baba, wewe uliyetukuka sana, wewe ustahiliye kuabudiwa na kila kiumbe, wewe MUNGU wa mababa zetu, tuko mbele zako wana wako, tuko mbele zako leo Baba, tunakuja tena kwa kulia na kuomboleza, tukiililia Nchi yetu, Nchi ambayo wewe MUNGU ndie ulieamua sisi tuzaliwe hapa.
Tunakuomba sana kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa nchi yetu 2010, tujalie utuongoze katika kufanya uchaguzi wa haki na huru, waaibishe na kuwafedhehesha wale wote wenye mapenzi mabaya na nchi yetu BABA.
Tunamchagua mwanadamu tena mwenye mapungufu Baba, tunaomba ulinzi wako uwe juu yetu, tubariki na utuvushe katika kipindi hiki, wengi walilia na bado wengi wanalia, nchi zinaomboleza, maafa, damu, vita kila mahali Baba, tuponye tunakuomba Baba.
Mbinu zote chafu, mawazo yote machafu dhidi ya wagombea hawa nazifunga katika DAMU ya YESU Kristo, wewe MUNGU uliewavusha wana wako katika matatizo mbali mbali katukumbuke na sisi leo Baba, sikia maombi yetu Baba, Wewe ni MUNGU unaejibu maombi, wewe ni MUNGU ulie HAI, tunakusihi Baba, tunakuomba Baba yetu, tuponye na machafuko na vita ili sisi tukaseme siku moja kwa ushuhuda kwamba "Kama si wewe BWANA...mwanadamu na aseme sasa".
Nawaombea wooote watakaosoma na kuielewa sala hii, si katika hali ya kupinga bali katika hali ya kuelewa, uwape kibali mbele yako, wao na familia zao na ndugu zao, na wale wooote MUNGU watakaopinga sala hii, kwa namna moja au nyingine Wabariki pia
Ni katika JINA la YESU KRISTO tunaomba.....Na wote mseme AMEN
Tunakuomba sana kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa nchi yetu 2010, tujalie utuongoze katika kufanya uchaguzi wa haki na huru, waaibishe na kuwafedhehesha wale wote wenye mapenzi mabaya na nchi yetu BABA.
Tunamchagua mwanadamu tena mwenye mapungufu Baba, tunaomba ulinzi wako uwe juu yetu, tubariki na utuvushe katika kipindi hiki, wengi walilia na bado wengi wanalia, nchi zinaomboleza, maafa, damu, vita kila mahali Baba, tuponye tunakuomba Baba.
Mbinu zote chafu, mawazo yote machafu dhidi ya wagombea hawa nazifunga katika DAMU ya YESU Kristo, wewe MUNGU uliewavusha wana wako katika matatizo mbali mbali katukumbuke na sisi leo Baba, sikia maombi yetu Baba, Wewe ni MUNGU unaejibu maombi, wewe ni MUNGU ulie HAI, tunakusihi Baba, tunakuomba Baba yetu, tuponye na machafuko na vita ili sisi tukaseme siku moja kwa ushuhuda kwamba "Kama si wewe BWANA...mwanadamu na aseme sasa".
Nawaombea wooote watakaosoma na kuielewa sala hii, si katika hali ya kupinga bali katika hali ya kuelewa, uwape kibali mbele yako, wao na familia zao na ndugu zao, na wale wooote MUNGU watakaopinga sala hii, kwa namna moja au nyingine Wabariki pia
Ni katika JINA la YESU KRISTO tunaomba.....Na wote mseme AMEN