Maombezi ya Padri yazua balaa Mwanza

Mongoiwe

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
524
263
Katika gazeti la Mwananchi toleo la Jana na Leo (Jumatano Oktoba 5 na Alhamisi Oktoba 6, 2010) kuna habari imeandika na waandishi Frederick Katulanda na John Dotto ikielezea kuwa Kuna Padri amekuwa akiwaombea mapepo waumini kwa kuwashika sehemu nyetu.

Watu wengi wamekuwa wakimiminika katika ofisi za Padri Pius Tulanalwo Bilulu wa kanisa Katoliki Parokia ya Bugando jimbo kuu la Mwanza, kwa ajili ya maombezi yanatolewa Uchi.


Maombezi ya Padri huyo yamejizolea umaarufu mkubwa kwa waumini wa dini mbalimbali katika mkoa wa Mwanza na na ile ya jirani kutokana n aimani kuwa kila anayeombewa hufanikiwa shida yake.


Gazeti hilo limenukuliwa likieleza kuwa waumini hao wamekuwa wakiombewa uchi kutokana na mapepo mengine kukaa semu nyingi, na wakati sehemu za siri.


Katika habari hiyo waandishi hao walijifanya mmoja wao kuwa anayo mapepo na kwenda kuombewa ambapo alivua nguo na kifanyiwa vitendo vyote vya maombezi, lakini wakati padri huyo akiendelea na maombezi hayo waliweza kumpiga picha na mwandishi huyo akiwa uchi.


OM. 1.jpg
Mwandishi akiombewa kutolewa mapopo akiwa kabaki na nguo ya ndani tu.
 
Back
Top Bottom