Manyigu na nyuki: Shairi-Chombo chenda mrama

Mar 23, 2011
86
32
Chombo kii baharini, mawimbi yasukasuka
Waloshika usukani, manahodha moja hulka
Walikitoa ufukweni, baharini 'kiingika
Abiria mehamaki, chombo chaenda mrama!

Ilipoanza safari, kutapika walihisi
Kwa woga wayo bahari, majiye kuyaakisi
Taratibu wakakiri, hawakuwa nayo jinsi
Nahodha kawatuliza, kuikabili safari.

Injiniye yachemka, nahodhaye chamshinda
Abiria wanamaka, wamehisi kinapinda
Tobo 'megundulika, 'lotoboa sio kinda
Manahodha moja hulka, chombo chenda mrama.

Aloshika usukani, Cheka Jino mpole
Litia na tumaini, chombo lipopokea
'Biria lipata amani, wakidhani si gobole
lo! Kama walotangulia, huyu pia limbukeni!

Limbukeni 'jisifia, ajigamba yu mweledi
Jama namhurumia, ajifanya maridadi
Chombo kinajinukia, hata akipiga dobi
Ukubwani kaingia, ndevuze hazichomozi!

Mashauriano afanya, ya akidi na unywaji
Kila wakiyamaliza, wajipamba kwa uaridi
Maji ya vikao vyao, machozi ya abiria
Ndio! chombo ki baharini, maji chumvi hayanyweki!

Vya wengine vyaelea, bahari haivitishi
Matobo meyamendea, maji hayawaangushi
Makasia 'jipigia, kama bwana maangushi
Chetu kinajizamia, manahodha tubadili.

Toka kiwe baharini, nchi kavu kijaona
Kama vile harusini, manahodha hawaj'ona
Wisiki wazitamani, wa'giza bila amana
Machoziye abiria, ni kinywaji chao bora!

Abiria amkeni, kusanyeni zana zenu
Machoziyo hayanyeshi, hata mchicha wa menge
Tafuteni nazo nyundo, zibeni hayo matobo
Manahodha fukuzeni, mchukue usukani.

Kwa majigu jifunzeni, na kwa nyuki vilevile
Nyuki wao wafaidi, kwa asali ya sukari
'Nyigu mwisho ni masega, hivi asali wawezi?
Lakini kiwasikia, wajiita nao nyuki!






 
1. Chomboni kuna matundu, japo bado twaelea,
Ni kama tunalo gundu, nahodha anapwelea,
Nahodha hana utundu, hana cha kuelezea,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

2. Chombo si kama shilingi, ama sivyo tungezama,
Sio ndoto wala bangi, ufukwe nautazama,
Nahodha huyu mhangi, mpeni njia kina mama,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

3. Tukifika ufukweni, tumpe ridhaa makini,
Hawezi tuweka poni, bayana yake thamani,
Apandapo jukwaani, ni vitendo bila ghani,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

4. Kwa unahodha ameiva, tayari kwa kuongoza,
Jamani mpeni ridhaa, ili safari kuanza,
Magwanda ameshavaa, nuru kote kuangaza,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

5. Kosa lilofanya jana, kesho katu sirudie,
Takao kuwa vijana, kwa mdomo washuhudie,
Ni sherehe ya kufana, kwa sasa tuvumilie,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

6. Tujipe uvumilivu, tupeane taarifa,
Subira yetu ya mbivu, tazifikia tarafa,
Hatutakubali mbovu, tatumia maarifa,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

7. Mpeni ulinzi nahodha, huyo wetu mtarajiwa,
Changia hata kwa fedha, shughuli kufadhiliwa,
Shima tuondoe adha, nahodha wetu akitajwa,
Japo twaelekea kuzama, mbele naona nuru.

 
Heko MSEJA MWANDAMIZI!badili jina kaka kukienzi kiswahili.na kwani hutaki oa?
Ndoa jama ni tamu,kimpata muadhamu.
Ndoa mashamshamu,pendo likiwa timamu.
Ndoa mithili ya ndimu,mchuzi kunogesha hamu.
Ndoa siyo jahanamu,pendo kishika hatamu.
 
Heko MSEJA MWANDAMIZI!badili jina kaka kukienzi kiswahili.na kwani hutaki oa?
Ndoa jama ni tamu,kimpata muadhamu.
Ndoa mashamshamu,pendo likiwa timamu.
Ndoa mithili ya ndimu,mchuzi kunogesha hamu.
Ndoa siyo jahanamu,pendo kishika hatamu.

Pangu Pakavu,

Ulosema yote poa, moyoni yamenipenya
Japo naitaka ndoa, bado nafsi naifinya
Walo ndani waniboa, hasa kwa wanachofanya
Ndoa wazitia doa, utadhani ni mapanya.

Utafiti nimefanya, kuzihusu hizo ndoa
Walo ndani wanaminya, nje kujichomozea
Walo nje wanahenya, ndani kupakimbilia
Sitaiga tembo kunya, mwandamizi nabakia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom