Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,706
- 155,275
Manusura mwingine aokolewa Haiti
Kijana wa kike ameokolewa kutoka kwenye vifusi vya jengo moja katika mji mkuu wa Haiti Port-au-Prince , -siku kumi na tano baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi.
Tetemeko hilo liliharibu sehemu kubwa ya mji huo na kusababisha hasara kubwa.
Kijana huyo amefutwa kutoka vifusi hivyo na maafisa wa uokozi kutoka Ufaransa.
Waokozi hao wanasema alikuwa amekwama kwenye bafu ambako aliishi kwa kunywa maji.
Wamesema licha ya kuwa na mshangao na kupata jeraha la mguu alijawa na furaha.
Ameokolewa siku tano baada ya serikali ya Haiti kusimamisha rasmi shughuli zote za kuwasaka na kuwaokoa walionusurika.
Yamkini watu laki mbili walifariki katika tetemeko hili lilotokea Januari 12 na wengine 130 wakiokolewa kutoka vifusi vya majengo yalioharibika.
Wakati huo huo rais wa nchi hii Rene Preval ametangaza kuahirishwa kwa uchaguzi wa wabunge ambao ulipangwa kufanyika mnamo Februar 28.
Kijana wa kike ameokolewa kutoka kwenye vifusi vya jengo moja katika mji mkuu wa Haiti Port-au-Prince , -siku kumi na tano baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi.
Tetemeko hilo liliharibu sehemu kubwa ya mji huo na kusababisha hasara kubwa.
Kijana huyo amefutwa kutoka vifusi hivyo na maafisa wa uokozi kutoka Ufaransa.
Waokozi hao wanasema alikuwa amekwama kwenye bafu ambako aliishi kwa kunywa maji.
Wamesema licha ya kuwa na mshangao na kupata jeraha la mguu alijawa na furaha.
Ameokolewa siku tano baada ya serikali ya Haiti kusimamisha rasmi shughuli zote za kuwasaka na kuwaokoa walionusurika.
Yamkini watu laki mbili walifariki katika tetemeko hili lilotokea Januari 12 na wengine 130 wakiokolewa kutoka vifusi vya majengo yalioharibika.
Wakati huo huo rais wa nchi hii Rene Preval ametangaza kuahirishwa kwa uchaguzi wa wabunge ambao ulipangwa kufanyika mnamo Februar 28.