Kisusi Mohammed
JF-Expert Member
- Aug 10, 2009
- 563
- 468
Habari za majukumu waungwana, natumai Mungu anatujaalia hali njema na afya za uhakika mpaka tunapata fursa za kupita huku jukwaani na kuweka hisia zetu.
Ni muda mrefu nimekuwa nikiamini ya kwamba ndege ni usafiri wa haraka na hurahisisha shughuli za kijamii hasa kwa wafanyabiashara na watu wenye kufanya kazi zao kwa kujali muda, bila kusahau makundi yote yanayokwepa usumbufu wa usafiri wa aina tofauti na ndege kwa kuikimbilia ili kupata huduma bora na za uhakika.
Hivi karibuni nimekuwa nikisiskia abiria wengi wanaopanda Precision ya kuelekea Mwanza wakilalamika kuwa mara wanacheleweshwa, mara ndege zinaahirishwa kienyeji, mara wanacheleweshwa kwa kupitishwa route ndefu bila kupewa taarifa, ila kwa sababu nahisi kuwa route ya Mwanza imekosa usafiri wa uhakika kwa muda mrefu hasa wa ndege kwa hiyo Precision wameamua kuitumia fursa hii kuwanyanyasa abiria wake.
Wadau naamini sauti za wengi ni sauti zenye mshindo, hebu wahanga na wenye maoni juu ya hili wafunguke hapa tujaribu kutafakari na kutafuta suluhisho ili pesa zetu zisiendelee kutunyanyasa!
Nna uchungu, nimesafiri toka Dar leo 11/10/2012 tumeondoka Dar saa 12 na dkk 10 jioni, tumeingia Mwanza saa 3 na dkk 10 usiku, si aheri ningepanda ungo wa bibi nikawahi!
Inauma sana
Ni muda mrefu nimekuwa nikiamini ya kwamba ndege ni usafiri wa haraka na hurahisisha shughuli za kijamii hasa kwa wafanyabiashara na watu wenye kufanya kazi zao kwa kujali muda, bila kusahau makundi yote yanayokwepa usumbufu wa usafiri wa aina tofauti na ndege kwa kuikimbilia ili kupata huduma bora na za uhakika.
Hivi karibuni nimekuwa nikisiskia abiria wengi wanaopanda Precision ya kuelekea Mwanza wakilalamika kuwa mara wanacheleweshwa, mara ndege zinaahirishwa kienyeji, mara wanacheleweshwa kwa kupitishwa route ndefu bila kupewa taarifa, ila kwa sababu nahisi kuwa route ya Mwanza imekosa usafiri wa uhakika kwa muda mrefu hasa wa ndege kwa hiyo Precision wameamua kuitumia fursa hii kuwanyanyasa abiria wake.
Wadau naamini sauti za wengi ni sauti zenye mshindo, hebu wahanga na wenye maoni juu ya hili wafunguke hapa tujaribu kutafakari na kutafuta suluhisho ili pesa zetu zisiendelee kutunyanyasa!
Nna uchungu, nimesafiri toka Dar leo 11/10/2012 tumeondoka Dar saa 12 na dkk 10 jioni, tumeingia Mwanza saa 3 na dkk 10 usiku, si aheri ningepanda ungo wa bibi nikawahi!
Inauma sana