Manumba: Polisi lipizeni kisasi

Me mwenyew jana nilipockia nilishangaa sana, sasa kama wao wanataka kulipiza kisasi sasa na huyu aliyekuwa anachukuliwa mke wake nae alipize kisasi kwa kwenda kula mzigo wa marehemu rpc? Hebu tuacha uvivu wa kufikir inachosha sana kuwa na nchi yenye ubovu kama huu'kwaiyo wao hili swala liliwauma sana mbona kwa mwangosi hawakulipiza kisasi??

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Katika hali halisi, Manumba amethibitisha kuwa Jeshi la Polisi ni la kulipiza visasi. Hata kifo cha Mwangosi kilitokana na yeye kumuuliza kamanda Kamuhanda, amfafanulie tofauti ya Internal meeting na Inside meeting, kutokana na kukerwa na swali hilo, ndiyo sababu iliyomfanya yeye Kamuhanda kusimamia ile 'OPERESHENI UA MWANGOSI' na kwa hali halisi, ile operesheni ilkuwa na baraka ya uongozi wote wa juu wa Polisi na Ikulu yenyewe,ushahidi wa wazi opo, ni kutokana na kuwa, pamoja na ripoti ya Jaji Manento kutamka waziwazi kuwa watuhumiwa 2 wakubwa wa mauaji ya Mwangosi ni Kamuhanda na Tendwa, kutokana na maagizo yao yaliyokiuka sheria za nchi, lakini hatujasikia yeyote kati yao kujiuzuru wadhifa wake, wala hatujasikia mkuu wa nchi aliyewateua, kuwawajibisha, badala yake tumemsikia mkuu wa nchi naye akisisitiza wauaji wa RPC wasakwe kwa nguvu zote, wakati wa mauaji ya Mwangosi, hakuwahi kutoa kauli yoyote. Kama Polisi wameamua kulipiza kisasi kwa kuwaua watuhumiwa wote wa Barlow, tutawashangaa sana, kwani wakubwa wengi wa Polisi wamesoma sheria, na wanaijua principle muhimu ya natural justice, inayosema kuwa 'man can not be a judge on his own case' kwa hiyo ni dhahiri wanachotakiwa kufanya ni kuwapeleka mahakamani na kuwasomea mashtaka, ili mahakama ndiyo iamue kama wana hatia au laa. Wakianzisha mfumo alioutangaza kamanda Manumba kuwa watalipiza kisasi kwa kuwarushia vitu vizito watuhumiwa wa mauaji ya kamanda Barlow, wanakaribisha jungle law nchini mwetu, ambayo tafsiri yake, nchi haitatawalika, kwa maana kila mtu atakuwa anachukuwa sheria mkononi mwake!!
 
Polis wanamjua aliye muua huyo kamanda na wanamuogopa ndiyo maana wanataka kulipiza kisasi.kama hawamwogope kwanini wasimkate?????
 
Sasa inapofikia mtu kama DCI anapohamasisha ulipaji kisasi tutegemee nini toka kwa wananchi mtaani?!! Ndio maana mob justice is the order if the day.

Tukio la juzi la 'waislamu' wa Mbagala kufanya fujo kuvamia kituo cha polisi, kuchoma makanisa n.k. kina tofauti gani na utekelezaji wa kauli ya DCI (kulipa kisasi)? Matukio ya madereva wa bodaboda kuvamia madereva wa magari wanaowagonga (iwe kwa bahati mbaya au kwa uzembe au pia kwa uzembe wa bodaboda) na kuwapiga hata kuua ni nini haswa kama sio mtizamo kama huu wa DCI? Halafu tunajiuliza kwa nini matukio ya watu kujichukulia sheria mikononi yanaongezeka kwa kasi ikiwa yule anayetakiwa kukemea ndie anatoa kauli tata namna hii mbele ya jamii.

Je wale ndugu ambao jamaa zao waliuwawa na polisi wachukue hatua gani? Nao walipize kisasi? Viongozi wetu wachunge sana kauli zao.
 
Halafu ukitaka kujua binadamu wanamkashifu Mungu, kwenye ibada ya mazishi ya huyu marehemu mtasikia eti Sisi tulimpenda sana lakini Mungu alimpenda zaidi! Yaani utembee na mali za watu uuwawe halafu eti Mungu alimpenda sana???:frusty:
Na Gwaride la mazishi km hawatapiga mizinga basi risasi kibao, RPC wetu alikuwa mtu mzuri sana na alikuwa akimsindikiza Dada yake bahati mbaya ikamkuta.
Lakini yakhe akifumaniwa na mke wa mtu au km yule Askari wa Uahamiaji Du yule jambazi aliingia katika Target bahati yake, ss POLISI katika kazi huwa hatuna utani
 
Manumba katoa kauli hiyo kwa sababu anatambua RPC kauwawa katika tukio la kulipiza kisasi na sio uambazi. Polisi wana silaha kemkem na mabomu kama walivyomlipua Mwangosi, lakini ukimkuta polisi yuko peke yake ni mwoga kama mbwa koko na ndipo hapo fursa inapatikana ya kisasi. Hata yeye Manumba akipita kwenye anga za majita hatoki.......

mkuu hicho ulichokiandika nimejikuta nacheka peke yangu. . . .
 
Tuueni tu wote kwa visasi vyenu mbaki wenyewe muone nani atalipa kodi mlipwe hiyo mishahara inayowafanya muwe na jeuri. ni kauli ya kitoto sijui lini tutakuwa na viongozi wenye busara
 
Katka kile ambacho hata mm ckutarajia kukisikia kutoka kiongozi mkubwa kama Manumba n kauli yake ya jana wakati wa kukumuaga marehem Barlow kua watalipiza kisasi kwa yeyote aliyehusika!....

kama police wataanza kujichukulia sheria mkonon tena kwa kutanganza hadhari kuua raia n dhahiri kua hatuna viongoz wala sheria hazifuatwi tena hapa TZ

Manumba hakustahiri hicho cheo, kumbuka matamshi aliyotoa wakati wa mauaji ya Songea, Iringa Morogoro na arusha. Huyu jamaa ni mwehu na hastahili kabisa katika huo wadhifa
 
Watatuua lakini wao pia tutawaua,jeshi lenyewe dhaifu linazidiwa na sungusungu,kamanda wa polisi eti wa mkoa mwenye dhamana ya ulinzi na usalama mkoa mzima anauawa kizembe namna hii,hakuna cha kisasa wala nini wataua lakini watauawa

hasitaili kutwa kamanda kwani kweli kafa kizembe sana, alafu ataendaje uchochoni bila ulinzi au alijishisha cheo, ndiyo kama yale ya Chenge na kibajari na gari bovu lisilo na bima. Mwanza mpooo mtatobolewa matundu kama mashimo ya nyamongo
 
Tanzania tunakwenda wapi sasa duh! na hii kauli ingetolewa na kiongozi wa m4c tayar kingenuka, ila sababu wametoa wenye nchi itapozewa tu, mkuki kwa nguruwe eeenh!
 
Sasa naanza kuamini ya kwamba viongozi wetu wengi nchini HUZUNGUMZA kwanza jambo na KUFIKIRIA juu ya jambo alilokua akizungumzia pasipo kujali kitu madhara yake.

Umwamba kwanza na busara baadaye.
 
Wakuu jf,

Hii ya Manumba kali zaidi, ila sishangai maana washika dola walishaamua 'liwalo na liwe'.

Kama ndugu wa marehmu Mwangosi wataamua kulipiza kisasi; jamaa za waliouawa Arusha nao hivyo; makanisa hivyo...God forbids.
 
Kwa hili lilotokea Zanzibar na kauli ya Manumba ya kulipiza kisasi napata shaka na hatima ya nchi yetu in a year to come......
 
Kauli ya askari wa jeshi la polisi wa ngazi ya juu kabisa ya kuwataka askari walipize kisasi kwa mauaji yaliyotokea ya RPC MWANZA. Je aliiongea kwa hasira au vp, nikweli kila mpenda HAKI NA AMANI amelaani mauaji hayo yaliyotokea huko mwanza,lakini swala la kuwataka askari walipize kisasi hiyo kauli iangaliwe upya,maana hata waandishi wa habari wangeweza kusema kama alivyosema MANUMBA kutokana na kifo cha muandishi mwenzao MWANGOSI.Wapenda amani na haki hii ni sawa sawa kwa kauli hii katika Taifa letu ambalo kwa sasa wananchi wake ambao wanaonekana kuchoshwa na vitendo uvunjifu wa amani vinavyo fanywa na walinzi wa raia na mali zao?
 
Back
Top Bottom