Mansour Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
mansoor-448x272.jpg


Na Salma Said,


Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi kwa upande wa Zanzibar, Mansour Yusuf Himidi, amesema atasimamia mtazamo wake kuhusu muundo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unaofaa hata kama itapelekea kuvuliwa uwanachama.

Mwandishi wa DW Zanzibar, Salma Said, amefanya mahojiano na Mansour Yussuf Himidi, ambaye ni waziri katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na pia Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuhusiana na kauli za Katibu Mwenezi wa chama hicho, Nape Nnauye, na wajumbe wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi, kumtaka arudishe kadi ikiwa hakubaliani na sera ya sasa ya serikali mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Habari hii kwa kirefu na audio clip, soma post HII


Na Mwinyi Sadallah | 6th August 2012 | Nipashe


Waziri asiye na Wizara Maalum wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Mansoor Yussuf Himid, amependekeza kuwepo na Muungano wa mkataba kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

Mansoor alitoa matamshi hayo wakati akichangia hoja kwenye semina ya mjadala wa mchakato wa ukusanyaji maaoni ya uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muugano Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar.

Alisema ipo haja ya kuwa na Muungano wa mkataba ili kuondokana na malalamiko mengi ambayo yanalalamikiwa katika Muungano wa sasa.

Katika maelezo yake, Mansoor alisema bado ataendelea kuwa muumini wa mfumo wa serikali mbili chini ya mkataba na si kama ilivyo sasa ili kuipa fursa zaidi Zanzibar kujijenga na kujitegemea kiuchumi.

Alisema si dhambi Zanzibar na Tanganyika chini ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zote zikawa na viti viwili katika Umoja wa Mataifa (UN).

Alieleza kuwa kuna baadhi ya viongozi kwa malengo yao binafsi wanajaribu kuwajengea hofu wenzao na kuwazuia kutoa maoni yao kwa upana kama raia huru kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Aliongeza kuwa hajawahi hata mara moja kukataa Muungano, ila mara zote amekuwa akihimiza mabadiliko ya kimfumo katika Muungano huo na kwamba anaamini kuwa kufanya hivyo si uadui wala usaliti.

"Hata NEC ya CCM ilipoanzisha mchakato wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kulienezwa hofu kila mahali, nashukuru tumefanikiwa kuunda GNU, sasa imesimama na kusomga mbele, kila mmoja anaona fahari, faida na tija ya jambo hilo," alisema.

Hata hivyo, kauli ya Mansoour ya kutaka Muungano wa mkataba na suala zima la kila upande kuwa na kiti UN, inamaanisha kwamba Zanzibar inapaswa kuwa huru.

Alisema awali suala la kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa lilipoibuliwa na Rais Jakaya Kikwete, kulikuwa na mtazamo hasi kwa baadhi ya wanasiasa waliokuwa wakiamini kuwa kuundwa kwa GNU kungetoa mwanya wa kuwarejesha watawala waliopinduliwa Januari 12,mwaka 1964 na kulipizana visasi.

"Hata wenzetu wa CUF kabla ya GNU, walikuwa wakipinga kila kitu kizuri cha SMZ, baada ya kushirikishwa serikalini hata yale waliyokuwa wakiyapinga wakati ule, sasa wanayaunga mkono, kuyasimamia na kuyashangilia," alisema Waziri Mansoor.

Akizungumzia umuhimu wa dhana ya Muungano alisema hapendi uvunjike na kwamba mara zote amekuwa akitaka hoja na haja ya Muungano huo kufanyiwa marekebisho ya msingi na kuwa chini ya mkataba.

Waziri huyo wa SMZ ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki kwa tiketi ya CCM, aliongeza kuwa ikiwa maoni yake yatachukuliwa na chama chake kuwa ametenda dhambi, atakuwa tayari kukabiliana na adhabu yoyote atakayopewa.

"Niko tayari kuadhibiwa kwa kutoa maoni ninayoyaamini kama ni ya kujenga, nafikiri nimetumia haki yangu ya Kikatiba na kiraia, nataka Zanzibar iwe na nyenzo zake za kiuchumi kwa maendeleo ya watu wake, sijali na wala sitawasikiliza wanaoeneza maneno ya uzushi," aliongeza Waziri Mansoor.

Alisema kila Mzanzibari anayo haki ya kutoa maoni yake bila mtu mwingine kuzuia utashi wake huku akisisitiza kuwa hiyo ndiyo demokrasia anayoijua yeye ndani ya chama chake.

Hata hivyo, aliipongeza CCM kuwa ina mwelekeo, viongozi wake wana uwezo wa kuvumiliana na kupima mabadiliko ya nyakati.

"Ninakiheshimu sana chama changu, ninakipenda, ndicho kilichonilea, bado ni imara sana, kuna watu wanataka kukichafua, kufika kwetu hapa ni kutokana na utashi wa viongozi wake kuwa na dira na uvumilivu," alisema.

TUME YA WARIOBA YATUPIWA LAWAMA

Tume ya kukusanya maoni ya Katiba inayoongozwa na ya Jaji Joseph Warioba, imetupiwa lawama kwa kushindwa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya baadhi ya viongozi wa CCM wanaowatisha wanachama wasitoe maoni ambayo yanatofautiana na msimamo wa chama hicho.

Waziri wa Miundombinu na Mwasiliano wa Zanzibar, Rashid Seif Suleiman, alisema tume hiyo ina kila sababu za kuchukuliwa hatua za kisheria kwa sababu wanachofanya ni kosa chini ya Sheria ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Alisema kitendo hicho kinapora uhuru wa wananchi kutoa maoni juu ya aina ya mfumo wa Muungano wanaoutaka.

Seif alikuwa anachangia mada juu ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyowasilishwa katika semina ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Aboubakar Khamis Bakary, mjini hapa.

"Nadhani Sheria ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba inakataza mtu au taasisi kumzuia mtu mwingine kutoa maoni yake au kumlazimisha aseme anavyotaka yeye, sasa hawa viongozi wa CCM wanaotaka kuwanyang'anya kadi wawakilishi wao wanakiuka sheria hii," alisema Waziri Seif.

Alisema ataendelea kuishangaa Tume ikiwa itaendelea kushindwa kukemea au kuwachukulia hatua wale wote wanaotoa vitisho dhidi ya watu wenye mitazamo tofauti na ya CCM katika Katiba mpya.

Seif alisema kila mtu yuko huru kutoa maoni yake mbele ya tume hiyo na kwamba si haki kwa mtu au chama chochote cha siasa kuwakataza wanachama wake kutoa maoni yanayogusa mitazamo yao binafsi tofauti na ya vyama vyao.

Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Zanzibar, Asha Bakar Makame, aliwataka viongozi wenzake ndani ya CCM kutowatisha wanachama wenye maoni tofauti na chama hicho katika suala la mabadiliko ya Katiba.

Asha alisema ni jambo la kushangaza katika ukuaji wa demokrasia wanapojitokeza watu kuwazuia wengine kuwa na mawazo huru kwenye mchakato wa kupata Katiba mpya.

"Jamani tusitishane, kama CCM kila mtu ni CCM hapa hakuna mtu asiyenijua msimamo wangu kuhusu Chama, ninakipenda na nitakitetea, lakini si vizuri kuanza kutishana kwa kuambiana huyu hivi huyu vile, haifai jamani," alisema.

Asha alikumbusha kwamba wakati wa kutafuta maridhiano ya kisiasa Zanzibar, wapo wana-CCM na viongozi waliopinga suala hilo, lakini hakuna mtu aliyeadhibiwa kwa kuvuliwa uanachama na kuwataka viongozi kuwavumilia wanachama na wafuasi wengine wa CCM katika suala zima la maoni tofauti kuhusu Muungano.

Mwakilishi wa Kwamtipura, Hamza Hassan Juma, alisema Rais Kikwete, hajazuia kutoa maoni tofauti na msimamo wa CCM juu ya suala hilo na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano huo na kuwa wavumilivu.

Hamza aliongeza kwamba CCM bado ni bora, hivyo kisiogope mageuzi kama ilivyotokea wakati wa mageuzi kutoka demokrasia ya chama kimoja kuingia mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992.

 
Watu kama huyo Yusufu Himid ndo ndumila kuwili, kutumikia mabwana wawili na kujaribu kufaidi kote.
Aondoke katika gari kubwa la CCM kabla ya kutoswa kwa aibu.
Kama hakubliani na ser za CCM si aingie Uamsho tu na aandamane?
 
Huyu Mh kaamua kuwa wazi kuwa mfuasi wa uamsho alie madarakani!heri yake ameonyesha sura ya ukweli kuliko wanafiki wanajificha sura zao kiwiliwili kiko wazi nje ...sasa wanajificha nini??ukweli haujifichi kamwe!
 
kama uamsho wazanzibari sote ni uamsho. mmemsikia Nassor Moyo, waziri wa sheria wa Jamhuri ya mungano wa mwanzo, mama Fatma Karume mke wa muasisi wa dola ya zanzibar, makamo wa CCM zanzibar na Rais mstaafu Karume, mwanasheria mkuu zanzibar, DPP zanzibar, wawakilishi zanzibar na wengineo.

kwa sasa hakuna anaeweza kuzuia nguvu ya wimbi la mabadiliko


wimbo ni mmoja tu kwa sote:

"tunataka nchi yetu sasa tumechoka "
 
Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
 
Mheshimiwa Nape,
Kwanza kabisa nikusihi usijibu hoja za matusi kama za huyo mtu wa pwani, matusi ni dalili za ukosefu wa hoja kwahiyo achana na wanaotukana, wewe jikite katika hoja zenye mantiki.

Nikirejea katika maswali niliyo nayo, labda nikuulize je ni busara kuandika katiba ya JMT ili hali kuna sintofahamu juu ya hatima ya muungano?

Swali la pili, kwa vile chama chako CCM kipo madarakani kwa zaidi ya miaka 40 kuanzia muungano(TANU/ASP) na hakikuweza kutatua malalmiko ya muungano, unadhani kuna njia gani mbadala itakayotumika kuhimili vishindo vya serikali 2 ikiwa hiyo imeshindikana siku za nyuma?

Tatu, Unadhani ni nini tatizo kubwa linaloutikisa muungano kwa sasa.

Shukran
 
Umenena vyema mkuu, Nnauye Jr, kuna wanaodhani tunalazimisha muungano.

Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
 
Last edited by a moderator:
Mheshimiwa Nape,
Kwanza kabisa nikusihi usijibu hoja za matusi kama za huyo mtu wa pwani, matusi ni dalili za ukosefu wa hoja kwahiyo achana na wanaotukana, wewe jikite katika hoja zenye mantiki.

Nikirejea katika maswali niliyo nayo, labda nikuulize je ni busara kuandika katiba ya JMT ili hali kuna sintofahamu juu ya hatima ya muungano?

Swali la pili, kwa vile chama chako CCM kipo madarakani kwa zaidi ya miaka 40 kuanzia muungano(TANU/ASP) na hakikuweza kutatua malalmiko ya muungano, unadhani kuna njia gani mbadala itakayotumika kuhimili vishindo vya serikali 2 ikiwa hiyo imeshindikana siku za nyuma?

Tatu, Unadhani ni nini tatizo kubwa linaloutikisa muungano kwa sasa.

Shukran

Ni masuali matatu yaliyotulia,ndani ya maswali hayo ndo sababu iliyomfanya mtu wapwani atukane matusi juu ya nape kwasababu sera ya ccm ni serikali 2 kwenda 1 na matatizo yake yameshaonekana njia za kuondoa hata watoto wadogo wanaelewa cha kushangaza nape na wenzake unapowaelekeza wanakubali juu ya matatizo hayo njia mbadala ipo lakin sera ya ccm ndo inayokandamiza suluhsho hlo.

Hapo inaonesha wazi sera na ilani ya CCM hata kama inamatatizo juu ya utawala nape hawezi kuizungumzia kwasababu yeye ndo msimamiaji wa sera hzo na hapo ndo sababu yakutukanwa kwa nape.swali lakujiuliza,je nikweli nape atakuwa mstar wa mbele na kukubali juu muundo wa serikali tatu?

Na kama atakubali yupo tayar kuikana ilani ya chama chake?kama hayupo tayar juu ya maswali hayo 2 hakuna jema ila ni maneno mabaya juu ya wananchi
 
Mheshimiwa Nape,
Kwanza kabisa nikusihi usijibu hoja za matusi kama za huyo mtu wa pwani, matusi ni dalili za ukosefu wa hoja kwahiyo achana na wanaotukana, wewe jikite katika hoja zenye mantiki.

Nikirejea katika maswali niliyo nayo, labda nikuulize je ni busara kuandika katiba ya JMT ili hali kuna sintofahamu juu ya hatima ya muungano?

Swali la pili, kwa vile chama chako CCM kipo madarakani kwa zaidi ya miaka 40 kuanzia muungano(TANU/ASP) na hakikuweza kutatua malalmiko ya muungano, unadhani kuna njia gani mbadala itakayotumika kuhimili vishindo vya serikali 2 ikiwa hiyo imeshindikana siku za nyuma?

Tatu, Unadhani ni nini tatizo kubwa linaloutikisa muungano kwa sasa.

Shukran

aongezee na hili.

1. Ni sababu gani zilitumika kuchagua serikali mbili ya tanzania na ya mapinduzi ya zanzibar?
2. Ni kwa nini serikali ya tanganyika iliuwawa kikatili na hivyo kutuondoshea heshima yetu mbele ya mataifa?
3. Iwapo wazanzibar wanulalamikia muungano ili hali wana serikali na wanafaidika mara mbili kwamba wanaweza kuongoza bara na visiwani, Je sisi watanganyika maumivu yetu mliyapima na kujua ni kiasi gani tunaathirika kwa kukosa serikali yetu?
4. Hivi ni sahihi ukoloni mamboleo ukatekelezwa na watu kiduchu wazanzibar, tena wasiotuzidi kwa lolote? iweje watutawale lakini sisi tusiwatawale?
 
Mtazamo wangu kuhusu hilo la Tanganyika kuuawa kinyemela ni kuwa, Aliyekuwa anataka muungano ni Mwl. Nyerere na ili wazanzibar wakubali ikabidi akubali kupoteza taifa lake alilolipigania hadi uhuru.

Hapa ndipo usaliti wa Watanganyika ulipo. Sasa kwakuwa TANU iliwasaliti watanganyika na kuamua ife izaliwe CCM. CCM sasa lazima ilinde usaliti wake wa Watanganyika.

Lamsingi wakubali mjadala na kuheshimu mawazo ya wananchi.
 
Mheshimiwa Nape,
Kwanza kabisa nikusihi usijibu hoja za matusi kama za huyo mtu wa pwani, matusi ni dalili za ukosefu wa hoja kwahiyo achana na wanaotukana, wewe jikite katika hoja zenye mantiki.

Nikirejea katika maswali niliyo nayo, labda nikuulize je ni busara kuandika katiba ya JMT ili hali kuna sintofahamu juu ya hatima ya muungano?

Swali la pili, kwa vile chama chako CCM kipo madarakani kwa zaidi ya miaka 40 kuanzia muungano(TANU/ASP) na hakikuweza kutatua malalmiko ya muungano, unadhani kuna njia gani mbadala itakayotumika kuhimili vishindo vya serikali 2 ikiwa hiyo imeshindikana siku za nyuma?

Tatu, Unadhani ni nini tatizo kubwa linaloutikisa muungano kwa sasa.

Shukran

mkuu tegemea majibu mepesi kwa maswali mazito.!
 
ZIwe serekali Moja ,Mbili au Kumi si tunachotaka ni sera dhabili za kuendeleza uchumi na siyo blabla tu.Muungano ujadiliwe kwenye ngazi zote ,mapungufu yawekwe sawa yafanyiwe kazi tuendelee na shughuli za maendeleo.Kuna watu wanapinga Muungano lakini cha ajabu ukiwauliza wanapinga hasa nini hana jibu tunakuwa washabiki tu!Mimi sidhani hakuna kitu ambacho hakishughulikiwi ila kinashughulikiwaje!na huwezi kumridhisha kila mtu hata kama chama kingine kitatawala.
 
Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
Kumbe kijana wa changanyikeni umo katika wale wanaotaka serikali tatu. Ila usiwe mkali sana kwa haya madudu mengine humu JF, utapasuka mishipa ya damu bure.
 
ZIwe serekali Moja ,Mbili au Kumi si tunachotaka ni sera dhabili za kuendeleza uchumi na siyo blabla tu.Muungano ujadiliwe kwenye ngazi zote ,mapungufu yawekwe sawa yafanyiwe kazi tuendelee na shughuli za maendeleo.Kuna watu wanapinga Muungano lakini cha ajabu ukiwauliza wanapinga hasa nini hana jibu tunakuwa washabiki tu!Mimi sidhani hakuna kitu ambacho hakishughulikiwi ila kinashughulikiwaje!na huwezi kumridhisha kila mtu hata kama chama kingine kitatawala.

Upopo hatari.
 
aongezee na hili.

1. Ni sababu gani zilitumika kuchagua serikali mbili ya tanzania na ya mapinduzi ya zanzibar?
2. Ni kwa nini serikali ya tanganyika iliuwawa kikatili na hivyo kutuondoshea heshima yetu mbele ya mataifa?
3. Iwapo wazanzibar wanulalamikia muungano ili hali wana serikali na wanafaidika mara mbili kwamba wanaweza kuongoza bara na visiwani, Je sisi watanganyika maumivu yetu mliyapima na kujua ni kiasi gani tunaathirika kwa kukosa serikali yetu?
4. Hivi ni sahihi ukoloni mamboleo ukatekelezwa na watu kiduchu wazanzibar, tena wasiotuzidi kwa lolote? iweje watutawale lakini sisi tusiwatawale?
Namkumbuka Mtikila, "saa ya ukombozi ni sasa" Uzuzu umetuzidi watanganyika. hakuna mjadala hapa. hatukushirikiswa kukolonisha Tanganika kwa Tanzania, Tanganyika ni koloni. Muungano huu wa hovyo ndio unaofanya dhahabu yetu ichimbwe kwa asilimia 3%. Tanganyika itakaporudi, hakika wote walioiba dhahabu na Tanzanaite watalipa.
 
Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!

Nyinyi ndio mnaolazimisha Muungano ,nyinyi mnajua fika kuwa Muungano huu ukivunjika basi vyeo vyenu vyote vinaanguka ,Nyinyi mnajua fika kuwa Muungano ukivunjika serikali ya Muungano inapoteza uhalali wa kuwepo,Nyinyi mnajua fika kuwa Muungano ukivunjika mnapoteza haki ya kuwa Chama tawala ,Nyinyi mnajua fika kuwa Muungano ukivunjika uhalali wa Bunge unavunjika ,Nyinyi mnajua kwa undani kabisa Muungano ukivunjika CCM ndio mwisho wake.

Mnaofilisika kimawazo ni ninyi mnaoelekea ukingoni ,Hivi huwajui wanaolazimisha Muungano ? Mbona unajifanya kipofu wewe ,ni akina nani wanaosema wataulinda Muungano kwa njia yeyote ? Pole sana ukisikia kuchamba kwingi.
 
MUUNGANO WA SERIKALI MBILI MWISHO CHUMBE 2015 – WAZANZIBARI

NIMESIKILIZA kwa makini sana maelezo ya Mhe Mansour Yussuf Himid na maelezo ya Nape Mnauye, nikarudia kusikiliza tena kwa mara ya pili ili kuweza kujiridhisha na kufahamu kwa undani hoja za kila mmoja. Hata hivyo, mawazo ya Nape, yamepitwa na wakati.


Kwa ufupi nimegundua kwamba viongozi wa CCM kwa upande wa Bara, yaani Tanganyika bado wanakasumba ile ile ya Nyerere, kutaka kuimeza Zanzibar. Kwa kauli ya Nape, si kweli kuwa Chama chao kina wigo wa kweli wa Demokrasia na uhuru wa kutoa maoni.


Aidha, nimegundua kuwa wanaamini Zanzibar ni mali yao waliyorithi kutoka kwa Nyerere na kusahau wajibu wao wa kuitetea Tanganyika yao na kuimarisha zaidi utawala wa Taifa la Tanganyika, kama wanavyofanya baadhi ya viongozi wa CCM wanaoumizwa na Zanzibar.


Nape, kauli yake iko wazi katika kudai kuendeleza kuitawala Zanzibar, ikibidi hata kwa mabavu na nguvu. Kwa mujibu wa kauli ya Nape, ni wazi kwamba Chama cha CCM, hakina nia njema kwa Zanzibar, kuona ina utawala wenye mamlaka yake kamili.


Nilipokuwa namsikiza nimejiuliza, hivyo kwanini Viongozi wa CCM Tanganyika, wanaumizwa na Zanzibar kuliko Tanganyika yao? Na hapa nimepata picha kwamba hata hizi vurugu na uonevu wa wananchi wa Zanzibar, unasimamiwa na CCM Tanganyika.


Nape Mnauye, anajaribu kuwatisha baadhi ya viongozi wa CCM wa Zanzibar kwa madai ya kupingana na sera za Chama chao. Mansour Yussuf Himid, amesema wazi kuwa sera za CCM si Katiba ya nchi wala si Sheria za nchi ni utaratibu wa Chama tu.


Nakumbuka mwanzoni mwa miaka ya 1980 Julius Nyerere, alisema kuwa Katiba si MSAAFU kwamba haibadiliki. Nape, anashikilia kwamba suala la Muungano kwa sera ya sasa ya CCM ni Serikali mbili.


Mansour, anakubali hilo na wala hakatai, ila anazungumzia mustakabali wa Zanzibar, kufuatana na mabadiliko ya Katiba mpya, hapo baadae. Hapa nimeamini CCM Tanganyika ni mafisadi wa kauli na imani zao.


Nape, anasema mwenye mawazo au maoni wayapeleke katika vikao halali vya CCM, ili yajadiliwe badala ya kuzungumza barabarani. Nape, amesahau kuwa Mansour amekuwa akizungumza kauli hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu ndani ya Baraza la Wawakilishi.


Mansour, amezungumza hayo katika mjadala wa rasimu ya Katiba chini ya Samuel Sitta, mwaka jana 2011 na amekuwa akirudia kauli yake ya kukataa Muungano wa Serikali mbili mara kwa mara ndani ya Baraza la Wawakilishi, hadi kudiriki kusema kuwa Muungano huu wa sasa ni BUTU.


Mansour kwa mara ya mwisho nimemsikia tena juzi katika Kongamano lililodhaminiwa na Norway, akisema kuhusu Muungano na muundo wa muungano wenye maslahi kwa Zanzibar. Inashangaza kuwa sehemu zote hizo Nape Mnauye, anaziona ni barabarani.


Nape, anavyo amini sehemu halali iliyotoharika kwa viongozi wa CCM kuzungumzia na kuujadili Muungano ni katika vikao vya CCM tu, wala si mahali pengine. Kumbe jamaa huyu ni mjinga sana na viongozi wote wa CCM Tanganyika wenye mawazo kama ya Nape, nawaweka kapu moja ya wajinga.


Na hapa nazidi kupata picha kwamba matatizo ya muda mrefu kwa Zanzibar, yamekuwa yakichangiwa na Tanganyika, kwa ushirikiano wa baadhi ya Viongozi wachache wa CCM Zanzibar, wanaokubali kuburuzwa na kutawaliwa na Tanganyika.


Kwa taarifa yenu mwaka huu mmeula na chua ‘JINGA LIKIEREVUKA MWEREVU YU MASHAKANI’ ikiwa tuliweza kufikia maamuzi ya kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, naamini na uwezekano wa kuipata Zanzibar yetu, iliyo-huru upo, kupitia viongozi na nguvu ya wananchi wa Zanzibar.


Nape Mnauye, kazi waliyofanya Jumuiya ya Uamsho, ilikuwa kazi ya kigoma cha kuamsha kula daku, ilikuwa ni kazi maalumu waliyopewa na Wazanzibari. Tunakuhakikishia muda si mrefu kwamba Muungano wa Serikali mbili utakuwa mwisho CHUMBE.


WATUACHE TUPUMUWEE..
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom