...Umemaliza, lakini hapo kwenye umbumbumbu ungeongeza pia na NJAA zetu!! Si unamkumbuka marehemu Gulamali. Alfikia hatua ya kutaka kadi za Yanga ziwe na Picha yake na baadhi ya wanachama kwa kuendekeza njaa wakawa tayari kupigana ili hili likubaliwe! likakwama tu kutokana na ujasiri wa mtu mmoja kwa jina la George 'Castro' Mpondela ambaye baaadae wenye njaa zao wakafanikiwa kumuondoa madarakani kama walivyofanikiwa kumuondoa Amani Mahugila Madega.
Ingawaje baadae 'shujaa' huyu ndiye aliyekuja kuwa kinara wa kiupinga mabadiliko ndani ya yanga na hasa uanzishwaji wa kampuni na hivi tunavyoongea yeye ni miongoni mwa watu wanaolamba miguu ya Manji.