nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
IJUMAA, 09 MACHI 2012 06:10 NA BAKARI KIMWANGA, DAR ES SALAAM
SAKATA la uuzwaji wa Shirika la Usafirishaji la mkoa wa Dar es Salaam (UDA), limechukua sura mpya baada ya Mwenyekiti wa Makampuni ya Quality Group Limited, Yusuf Manji, kuibuka na kukana hatua za kutaka kununua kampuni hiyo kinyemela.
Hatau hiyo ya Manji, imekuja siku moja baada ya kudaiwa na kufadhli harakati za kutaka kuing'oa kampuni ya Simon Group katika umiliki wa UDA.
Kwa mujibu wa taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana, Manji alisema hausiki na harakati za viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam katika sakata la kuing'oa Kampuni hiyo kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
"Mwalimu Nyerere, aliwahi kutuonya kwamba uongo ukiachiwa kuendelea kwa muda mrefu, unageuka kuwa ukweli na watu wanauamini, nilidaiwa kuwatumia Wenyeviti wawili wa Kamati za Bunge ili kufanikisha hilo ambao ni Dk. Abdallah Kigoda na Zitto Kabwe ili kulipata Shirika hili kwa mlango wa nyuma. Hivyo nimeonelea kutoendelea kukaa kimya wakati Taifa linapotoshwa.
"Ni ukweli ulio wazi mimi kama Kiongozi wa Quality Group, baada ya kusikia minong'ono na taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba UDA limebinafsishwa kwa Simon Group, niliamua kuwaandikia barua wenyeviti hao wa Kamati mbili za Bunge ambazo ndizo zenye jukumu la uangalizi wa mashirika ya umma.
"Lengo kubwa la kuandika barua hizo ni kuweza kuomba kupata ufafanuzi juu ya taratibu zilizotumika kulibinafsisha shirika hilo, niliwaeleza kwa kinagaubaga kwamba nimesikia kupitia vyombo vya habari kuwa uuzwaji wa hisa asimilia 51 za UDA umefanywa, na tayari Kampuni ya Simon Group imepewa," alisema Manji, katika taarifa yake.
Katika Barua hiyo Manji alikiri kushiriki katika tenda mbili za UDA ambapo ya kwanza ilifanyika mwaka 2005, ka kuzishirikisha kampuni tatu huku nyingine ikirudiwa tena mwaka 2007 ambapo kampuni ya Quality Group pekee ndiyo ilishiriki.
Barua hiyo kwenda kwa wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge ya Agosti 14, iliambatanishwa vivuli vya nyaraka za tenda hiyo na kutumwa kwa Mwenyekiti Mtendaji wa PPSRFC.
"Katika tenda ya mwaka 2007, tulieleza kuwa tuko tayari kuingia ubia wa shirika hilo kwa gharama ya Sh. bilioni 1.5 kwa ajili ya ununuzi wa hisa 49 za UDA.
"Na kama tungefanikiwa kupata tenda hiyo nilieleza wazi tungewekeza Dola za Marekani milioni 10, kwa ajili ya ukarabati wa karakana. Pia tulieleza kuwa tungeleta mabasi 150 chini ya utaratibu wa DART.
"Tulifanya hivyo tukizingatia ukweli kwamba tulikuwa na uzoefu wa miaka 30 katika sekta ya usafirishaji nchini kwa kushirikiana na makampuni makubwa ya usafirishaji na usafiti duniani kama vile Honda, ISUZU na Bridgestone, na tuliomba tenda hiyo tukiwa tayari na makubaliano na kampuni ya Hess kutoka Swatzerland," alisema Manji
Mwisho
Moja ya mabasi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA)
SAKATA la uuzwaji wa Shirika la Usafirishaji la mkoa wa Dar es Salaam (UDA), limechukua sura mpya baada ya Mwenyekiti wa Makampuni ya Quality Group Limited, Yusuf Manji, kuibuka na kukana hatua za kutaka kununua kampuni hiyo kinyemela.
Hatau hiyo ya Manji, imekuja siku moja baada ya kudaiwa na kufadhli harakati za kutaka kuing'oa kampuni ya Simon Group katika umiliki wa UDA.
Kwa mujibu wa taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana, Manji alisema hausiki na harakati za viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam katika sakata la kuing'oa Kampuni hiyo kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
"Mwalimu Nyerere, aliwahi kutuonya kwamba uongo ukiachiwa kuendelea kwa muda mrefu, unageuka kuwa ukweli na watu wanauamini, nilidaiwa kuwatumia Wenyeviti wawili wa Kamati za Bunge ili kufanikisha hilo ambao ni Dk. Abdallah Kigoda na Zitto Kabwe ili kulipata Shirika hili kwa mlango wa nyuma. Hivyo nimeonelea kutoendelea kukaa kimya wakati Taifa linapotoshwa.
"Ni ukweli ulio wazi mimi kama Kiongozi wa Quality Group, baada ya kusikia minong'ono na taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba UDA limebinafsishwa kwa Simon Group, niliamua kuwaandikia barua wenyeviti hao wa Kamati mbili za Bunge ambazo ndizo zenye jukumu la uangalizi wa mashirika ya umma.
"Lengo kubwa la kuandika barua hizo ni kuweza kuomba kupata ufafanuzi juu ya taratibu zilizotumika kulibinafsisha shirika hilo, niliwaeleza kwa kinagaubaga kwamba nimesikia kupitia vyombo vya habari kuwa uuzwaji wa hisa asimilia 51 za UDA umefanywa, na tayari Kampuni ya Simon Group imepewa," alisema Manji, katika taarifa yake.
Katika Barua hiyo Manji alikiri kushiriki katika tenda mbili za UDA ambapo ya kwanza ilifanyika mwaka 2005, ka kuzishirikisha kampuni tatu huku nyingine ikirudiwa tena mwaka 2007 ambapo kampuni ya Quality Group pekee ndiyo ilishiriki.
Barua hiyo kwenda kwa wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge ya Agosti 14, iliambatanishwa vivuli vya nyaraka za tenda hiyo na kutumwa kwa Mwenyekiti Mtendaji wa PPSRFC.
"Katika tenda ya mwaka 2007, tulieleza kuwa tuko tayari kuingia ubia wa shirika hilo kwa gharama ya Sh. bilioni 1.5 kwa ajili ya ununuzi wa hisa 49 za UDA.
"Na kama tungefanikiwa kupata tenda hiyo nilieleza wazi tungewekeza Dola za Marekani milioni 10, kwa ajili ya ukarabati wa karakana. Pia tulieleza kuwa tungeleta mabasi 150 chini ya utaratibu wa DART.
"Tulifanya hivyo tukizingatia ukweli kwamba tulikuwa na uzoefu wa miaka 30 katika sekta ya usafirishaji nchini kwa kushirikiana na makampuni makubwa ya usafirishaji na usafiti duniani kama vile Honda, ISUZU na Bridgestone, na tuliomba tenda hiyo tukiwa tayari na makubaliano na kampuni ya Hess kutoka Swatzerland," alisema Manji
Mwisho