Manispaa ya Moshi yaongoza kuwa na wasomi wengi Tanzania

afu Jirani yetu ana Walizi wawili wote wachanga,, pia housegirl wake ni Mmachame,

kwenye RED hapo! kweli watakaohesabu sensa wana kazi.Kama wachaga=wachanga, walinzi=walizi lazima mtoto utamwita baba na baba awe mtoto. Wote tukiwa maafisa wa TRA nako mtasema mnaonewa, kila kitu kunungunika tu.
 
Kama hii taarifa ina ukweli, nani wa kupongezwa? Chama cha Mapinduzi - chama dola na sera zake bora za elimu? Au juhudi binafsi za watu wa Moshi? Au ni taasisi mbali mbali zisizo za kiserikali kama za dini kwa michango na juhudi zao? Au ni vyama vya upinzani ambavyo vimeongoza Moshi kwa mihula kadhaa sasa? Na je, ni kwanini Moshi? Kinachoshindikana maeneo mengine ya nchi yetu ni nini?
Maswali yako ni ya msingi sana naomba magamba wayajibu
 
sijackia watoto wa kazi wakitolewa moshi kuja kufanya kazi dar bali nasikika wanatoka kule kwenye kilima kinachoua sana baada ya mikumi......................Infact Moshi kila kata ina shule mbili zasecondary ni ni vigumu kumkuta mtu hajampeleka mtot wake shule.Tatizo sas linakuwa ni ardhi.Nitafanya lobbying na watu angalau tuweze kuwahamisha baadhi wa watu tuwapeleke lindi mtwara pwani,rukwa ili waache kugombania ardhi

Watoto wa kazi kutoka Moshi wapo ila wanakuwa na malengo kimaisha kwa ushirikiano na familia wanazotoka. Halafu hata utendaji wao una tija kutokana na kisomo siyo sawa na wale ambao hawajaona darasa.
 
Hizi tafiti mbona zinatuchanganya. Kuna utafiti mwingine sikumbuki ulifanywa na shirika gani but it is about two months ago walitoa results, wao waliosema hivi about 60% ya wanawake wa Moshi hawajui kusoma na kuandika.

I can remember nikamsikia mbunge Lucy Owenya na MB yule CDM aliyekuwa manager wa keys Hotel (nimemsahau jina), katika mchango wa ofisi ya waziri mkuu waki quote hiyo statistics ya 60% illiteracy rate in women of Moshi district.

Elewa kilichoandikwa wewe usiwe limbukeni tafiti inaonesha " urban Moshi citizens"
 
Kama hii taarifa ina ukweli, nani wa kupongezwa? Chama cha Mapinduzi - chama dola na sera zake bora za elimu? Au juhudi binafsi za watu wa Moshi? Au ni taasisi mbali mbali zisizo za kiserikali kama za dini kwa michango na juhudi zao? Au ni vyama vya upinzani ambavyo vimeongoza Moshi kwa mihula kadhaa sasa? Na je, ni kwanini Moshi? Kinachoshindikana maeneo mengine ya nchi yetu ni nini?

Moshi kuna sheria ndogndogo zinazombana mzazi kuhakikisha mtoto anaenda shule akifikisha miaka saba. Nashauri na sehemu nyingine waige hili labda litasaidia huko kwingineko
 
unaposema uwongo unatakiwa kuwa na kumbukumbu vile vile! inakuja akilini kweli mtu una mahousegirl wawili(2), mmoja(1) atoke ROMBO na wawili(2) KIBOSHO? hiyo hesabu inakuwaje hapo,Isitoshe mchaga anafanya kazi kwa malengo usijeshangaa baada ya muda wakawa maboss wako kama ni kweli.

Hiyo ni kosa la uandishi tu.Sikatai kuwa wanafanyakazi kwa malengo,ila kuwa bosi wangu hilo hapana!Nakataa kwa nguvu zote labda aibe vyeti !
 
Moshi kuna sheria ndogndogo zinazombana mzazi kuhakikisha mtoto anaenda shule akifikisha miaka saba. Nashauri na sehemu nyingine waige hili labda litasaidia huko kwingineko

Wakiweza itakuwa vizuri japo vizuizi ni vingi sana - mila, desturi, tabia, mtazamo, imani, n.k. kama ifuatavyo (mifano michache):

MILA: Kuna wale wengine binti akishafikisha ule umri kinachofuata ni kufundwa/unyago na kufundishwa mambo ya kikubwa tayari kuwa Bi. Mdogo. Nguvu za ziada zinahitajika hapa.

DESTURI: Na wale wengine kwa desturi mtoto wa kike hapelekwi shule bali kutafutiwa mume - wengine wakiwa na miaka tisa! Kazi ipo. Na kwa wengine mtoto wa kiume ni kwa ajili ya kazi za kifamilia kama kuswaga mifugo, n.k.

MTAZAMO: Kwa wengine, elimu (ya darasani) ni mfumo wa kimagharibi. Upuuzi umezaa akina Boko Haram (maana yake ni Elimu ya Magharibi Haramu).

DINI: Hapa ndio balaa. Sote tunajua hili.

TABIA: Hayo mengine niliyoyataja huzaa tabia ambayo hatimaye huwa kama "sheria".
 
jamani kueweni specific.
mnaongelea manispaa yamoshi au halmashauri ya moshi?kama ni manispaa ya moshi, hiyo study itakuwa imewahusisha na wananchi wa halmashauri ya moshi na kwenye sensa idadi ya watu wa manispaa itakuwa ndogo sana na rahisi kuliko mnavyofikiri ,ninasema hivyo kwa sababu shughuli na biashara nyingi zinamilikiwa na wa halmashauri asubuhi wanakuja na jioni wanaenda kwao. mfano ukienda manispaa saa moja jioni au siku za sikukuu utakuta mji ni mkimya hauna watu .
hivyo siku ya sensa watahesabiwa huko halmashauri lakini kwa siku watatumia huduma za manispaa
 
Recent studies indicate that moshi urban district has the highest literacy rate for person over 15 years of age comapared to any of the other 128 districts in Tanzania.Therefore, Moshi will be the last place where census exersize is likely to run into problems.It is a town where every person is educated.
Source: Daily News - 6/8/2012
Inatusaidia nn katika maisha ya mtanzania wa kawaida?
 
NAONA SAIZI KASKAZINI MKO VIZURI YANI KILA KIZURI KASKAZINI HONGERENI SANA NAOMBA KUPATA MKE MCHAGA MIMI NI MKINGA NADHANI TUTAENDANA
 
so what!!!
Soma vizuri ni Urban district inawezekana utafiti huo unaousemea mi Moshi rural districts
Hizi tafiti mbona zinatuchanganya. Kuna utafiti mwingine sikumbuki ulifanywa na shirika gani but it is about two months ago walitoa results, wao waliosema hivi about 60% ya wanawake wa Moshi hawajui kusoma na kuandika.

I can remember nikamsikia mbunge Lucy Owenya na MB yule CDM aliyekuwa manager wa keys Hotel (nimemsahau jina), katika mchango wa ofisi ya waziri mkuu waki quote hiyo statistics ya 60% illiteracy rate in women of Moshi district.
 
Back
Top Bottom