Wana JF taarifa tulizozipata ni kuwa sasa hivi kuna vita kali ya chinichini kati ya madiwani wa Manispaa ya Moshina Mkurugenzi wao kuhusu ugawaji wa viwanja uliofanywa kinyemela na Mkurugenzi maeneo ya Majengo block R.Inasemekana eneo hilo lilikuwa eneo wazi katika kata ya Majengo lakini kwa hila eneo hilo limebatizwa na Mkurugenzi na ofisa ardhi kuwa ni eneo baki (reserve)na limegawanywa viwanja vitano na pia inasemekana aliyepewa ni mtu na mkewe tena matajiri wa kutupwa ndio wamepewa hivyo viwanja.Inasemekana pia katika kikao cha juzi cha Mipango miji hoja hiyo iliibuka na kuletaa mtafaruku mkubwa kati ya madiwani na Mkurugenzi wao na hata kutishia kikao kuvunjika lakini kwa kuwa hoja hiyo ilikuwa katika mengineyo kiliisha salama lakini bado ikaamriwa kamati ndog ipate majibu ya hoja hiyo siku ya jana .Ikumbukwe pia Baraza hilohilo liliunda kamati ya uchunguzi kuhusu viwanja vinavyotolewa kiholela wakati kuna kesi nyingi za madai ya ardhi inayoikabili Manispaa hiyo katika mahakama za ardhi. na madai mengine ya kutoa vibali holela vya ujenzi na ukarabati ambayo pia Mkurugenzi huyo alilalamikiwa pia na Mbunge PhilemonNdesamburo katika vikao vya bunge.Mlio karibu na Mwenyekiti wa mipango miji hebu mtujuze nini kinaendelea baada ya kikao cha jana.