Manesi wa Massana Hospital Mbezi Beach Wanasafisha Vyoo Vya Wagonjwa - Massawe nini??

Kama watu wetu wanalalamika hawana mikate, kwa nini wasile keki?

MKuu WoS, mtu akilalamika anapata shuruba na minyanyaso lukuki kazini huwezi kukimbilia suluhisho la kusema aacha kazi! Hiyo ni kuwa out of touch. Kuna shutuma za mazingira hatari ya kazi, kusafisha $#@& za wagonjwa bila gloves, mishahara inayoendana na kabila, kataka kulalamika hajakaa sawa wamem fire, wewe unamwambia atafute kazi pengine. Kuna haki za mfanyakazi ambazo anajaribu kuzitafuta ndugu yangu.

Kwanza hujui ugumu wa kupata hizo kazi. Pili, hata akiacha kazi, halafu mazingira ya kazi yakabaki hivyo hivyo ni kwamba miaka ya mbele ndugu yako au mtoto wako WoS na wangu wanaweza kuja kufanya kazi hapo. Tutafute haki za wafanyakazi wa nchi yetu, tusiwe out of touch kwa kuwaambia wasio na mikate wakale keki.


1. Naona quotation ya Mke wa King Louis wa Ufaransa kabla ya French Revolution...Marie Anttoinette!
Mimi ni mbangaizaji .. Quotation yako therefore hainihusu maana siko kwenye rulling class ndugu yangu.

2.Ugumu wa kupata kazi naujua sana..na vilevile kwa vile najua ndio maana nikipata kibarua sioni tija kubabaishana na kubishana na mwajiri.Vikinishinda huwa naanza!

3. Haki za mfanyakazi - kuna taratibu zake - akalalamike kuanzia ngazi ya Trade Unions na Labour..kwa kuja hapa wewe Dilunga umemsaidia nini mpaka sasa hivi? Hata mawazo tu hujampa.Bora hata mie nimempa ushauri hata kama kwako wewe na wengine haufai!
 
Ninavojua mimi nesi kamili aliyesoma miaka minne huwezi kumuambia asafishe choo, kuna wale nurse assistanta wamesoma mwaka moja hao mara nyingi ndo wanambiwa wasafishe choo na mambo mengine.
halafu kuna mchangiaji kasema manesi wamekuwa wengi mno, huo ni uongo manesi siyo wengi kabisa sema wengi wanataka kufanya kazi mjini, serikali kila siku inatangaza nafasi za manesi watu hawaapply, na hamna field nzuri kama nutrse kupata kazi.
Kuna hospital moja ya kanisa ipo dodoma ukienda unapewa nyumba ina maji umeme wa solar, vyote bure lakini wadada wakienda tu kidogo wanarudi eti siyo mjini, kuchagua sehemu za kufanyia kazi nalo ni tatizo.
 
1. Naona quotation ya Mke wa King Louis wa Ufaransa kabla ya French Revolution...Marie Anttoinette!
Mimi ni mbangaizaji .. Quotation yako therefore hainihusu maana siko kwenye rulling class ndugu yangu.

2.Ugumu wa kupata kazi naujua sana..na vilevile kwa vile najua ndio maana nikipata kibarua sioni tija kubabaishana na kubishana na mwajiri.Vikinishinda huwa naanza!

3. Haki za mfanyakazi - kuna taratibu zake - akalalamike kuanzia ngazi ya Trade Unions na Labour..kwa kuja hapa wewe Dilunga umemsaidia nini mpaka sasa hivi? Hata mawazo tu hujampa.Bora hata mie nimempa ushauri hata kama kwako wewe na wengine haufai!

Yaani kwa staili hiyo mengi yanayowekwa hapa JF ingebidi yasiwekwe kwa sababu kuna taratibu zake za kufuatilia. Labda hujanotice kwamba kutoa malalamiko hapa JF ni jambo la kawaida. Na pia zinasaidia kutoa habari za ambayo pengine yanawasibu wenzetu.

Sioni mantiki kwa nini huyu dada umkamie kooni. Maana kwa mantiki hiyo ya kwako, anayelalamika kuhusu Richmond kwamfano utamwambia ayapeleke PCCB kwa sababu kuna taratibu.

Nahisi tu kuna kitu dada wa watu amekukera, au ndio ule wivu wa kike.
 
Kwanini huyo Dada yako asiondoke akatafuta kazi mahali pengine maana ana ujuzi kuzidi kazi anayopangiwa? Kwani lazima afanye hapo Massana?


WB,

demand versus Supply ya manesi hailingani matokeo yake wanabanana katika kufanya kazi ambazo zinaangukia kwenye 'any other jobs as assigned by the management'.
 
. Haki za mfanyakazi - kuna taratibu zake - akalalamike kuanzia ngazi ya Trade Unions na Labour..kwa kuja hapa wewe Dilunga umemsaidia nini mpaka sasa hivi? Hata mawazo tu hujampa.Bora hata mie nimempa ushauri hata kama kwako wewe na wengine haufai!




HIVI WAKATI UKIANDIKA ULIKUWA UMEPATA KIDOGO NINI??
 
Nahisi tu kuna kitu dada wa watu amekukera, au ndio ule wivu wa kike.

This is ridiculous! Wivu? namjua au namwonea wivu kuajiriwa Missana kuosha vyoo badala ya unesi?Mbona watu wengien mnataka watu wasahau ustaarabu kwa posts zenu?
 
WB,

demand versus Supply ya manesi hailingani matokeo yake wanabanana katika kufanya kazi ambazo zinaangukia kwenye 'any other jobs as assigned by the management'.

This is an omnibus clause ambayo humaliza mzizi wa fitna kwenye ajira! Kwa positions za chini kuna hiki kipengele, na kama kawaida yetu Watz HATUSOMI NA HATA TUKISOMA SIJUI KAMA WATU WANAELEWA MAANA YA CLAUSE KAMA HII!wANASAINI halafu baadae wanawaendea akina Pididdy kulalamika!! Hilarious!
 
. Haki za mfanyakazi - kuna taratibu zake - akalalamike kuanzia ngazi ya Trade Unions na Labour..kwa kuja hapa wewe Dilunga umemsaidia nini mpaka sasa hivi? Hata mawazo tu hujampa.Bora hata mie nimempa ushauri hata kama kwako wewe na wengine haufai!




HIVI WAKATI UKIANDIKA ULIKUWA UMEPATA KIDOGO NINI??[/QUOTE]


Badala ya kukimbilia kuwa sarcastic..omba msaada upewe ukamsaidie huyo nduguyo anayeosheshwa vyoo!
 
WB,

demand versus Supply ya manesi hailingani matokeo yake wanabanana katika kufanya kazi ambazo zinaangukia kwenye 'any other jobs as assigned by the management'.

hospitali inaweza kukupeleka sehemu yeyote ndani ya hospitali kufanya kazi....

kwenye mikataba ya kazi huwa kuna hiki kitu huwa wanakitumia na kusema kampuni inaweza kukuhamisha na kukupeleka kwenye dept nyingine...

kitu ambacho nimekiona ni kuwa huyo principal anajali usafi na ni kitu muhimu sana kwenye hospitali...

labour cost - hospitali lazima zi control labour cost... kama nurse hayuko busy lakini mshahara wake unalipwa kwa nini asifanye usafi, unataka kusema kwamba nurse anahitajika kwenda kumtibu mgonjwa anaelia kitandani lakini principal wake anamuambia atoke aende akasafishe....
kama umeshaenda kwenye baadhi ya hizi private hospital mitaa ya saa nane mchana utakuta manesi wanapiga story hawana kazi..
je mgonjwa akijikojolea nesi ataenda kumwita mtu wa usafi ambaye ajasomea kuhudumia wagonjwa????

mwambie aangalie mkataba wake wa kazi kama unasema yeye kazi yake ni sehemu moja tu???
 
This is ridiculous! Wivu? namjua au namwonea wivu kuajiriwa Missana kuosha vyoo badala ya unesi?Mbona watu wengien mnataka watu wasahau ustaarabu kwa posts zenu?

Samahani nilishindwa kujipa explanation nyingine inayoleta sense. Reaction yako haikuwa na tofauti na ya mtu atakayemwambia mama anayejifungua barabarani akimbie hospitali ... kisa ni uzembe wake hakuwahi kutoka nyumbani. Yaani kwa maneno mengine reaction yako ilikosa chembe ya empathy. Na simaanishi kwamba ulikuwa unawajibu wa kumsaidia, la hasha! Lakini pia sidhani kwamba kumbeza mtu aliye na tatizo ni vizuri.

Na jinsi ulivyojisikia baada ya kuambiwa una wivu wa kike, ndivyo jinsi ambavye angejisikia angeambiwa "unalalamika lalamika nini, si ufuate taratibu". Yote matusi tu. Sema heri yako wewe unaweza ukapunguza hasira yako kwa ku-type na kupost hapa ... yeye pengine hata hajawahi kusogelea computer maskini ya mungu ... na kwa bahati mbaya yake kuna mtu at least mmoja ambaye hana uwezo wa kuona maumivu ya moyo wake.
 
mambo ya ajira inaonekana wanakubaliana na uhalisia wa mambo otherwise wangegoma!

Kama unamaanisha mtu akiendelea kufanya kazi huku aridhiki na mazingira ya kazi maana yake anakubaliana na uhalisia wa mambo, na kama "kukubaliana na uhalisia wa mambo" maana yake ni kuchukulia kwamba unachotendewa ni sawa na ni haki kwako, then nadhani hiyo sentensi inamatatizo ya kimantiki.
Umeasume mtu asipogoma maana yake anakubaliana na uhalisia wa mambo. Kitu ambacho si cha kweli all the time. Saa nyingine cost ya kugoma inazidi hasara unayopata kwa kuendelea na uhalisia wa mambo.

Unachosema hapo hakina tofauti na kusema "babu zetu watumwa walikuwa wanakubaliana na uhalisia wa mambo, otherwise wangegoma".

Na haina tofauti sana na wewe kuendelea kulipa kodi wakati ukilalamikia Richmond, EPA, etc. Inaonekana umekubaliana na uhalisia wa mambo, otherwise ungegoma kulipa kodi. Thubutu uone!
 
WB,

demand versus Supply ya manesi hailingani matokeo yake wanabanana katika kufanya kazi ambazo zinaangukia kwenye 'any other jobs as assigned by the management'.
You are right man.

This is an omnibus clause ambayo humaliza mzizi wa fitna kwenye ajira! Kwa positions za chini kuna hiki kipengele, na kama kawaida yetu Watz HATUSOMI NA HATA TUKISOMA SIJUI KAMA WATU WANAELEWA MAANA YA CLAUSE KAMA HII!wANASAINI halafu baadae wanawaendea akina Pididdy kulalamika!! Hilarious!

hospitali inaweza kukupeleka sehemu yeyote ndani ya hospitali kufanya kazi....

kwenye mikataba ya kazi huwa kuna hiki kitu huwa wanakitumia na kusema kampuni inaweza kukuhamisha na kukupeleka kwenye dept nyingine...

kitu ambacho nimekiona ni kuwa huyo principal anajali usafi na ni kitu muhimu sana kwenye hospitali...

labour cost - hospitali lazima zi control labour cost... kama nurse hayuko busy lakini mshahara wake unalipwa kwa nini asifanye usafi, unataka kusema kwamba nurse anahitajika kwenda kumtibu mgonjwa anaelia kitandani lakini principal wake anamuambia atoke aende akasafishe....
kama umeshaenda kwenye baadhi ya hizi private hospital mitaa ya saa nane mchana utakuta manesi wanapiga story hawana kazi..
je mgonjwa akijikojolea nesi ataenda kumwita mtu wa usafi ambaye ajasomea kuhudumia wagonjwa????

mwambie aangalie mkataba wake wa kazi kama unasema yeye kazi yake ni sehemu moja tu???

Sina tatizo na logic zenu. Ila ninapowaona mnashangilia maumivu ya wenzenu (weather ni kwa uzembe wao au la) ndipo naanza kuhisi kuna kitu hakiko sawa.

Attitude mlizonazo ni typical attitude za waajiri wengi, na HR managers wao. Mnatumia ujinga wa watu, au kutokuwa kwao makini, kuwabana kwenye vipengele vya mikataba. Na mnaona hiyo ni sawa kabisa. Yes, mnashinda, mnapunguza cost, mnafanikiwa kuwafanyisha watu kazi ambazo walikuwa hwazitegemei, mnafanikiwa kuwafanyisha kazi watu kupita kiasi bila malipo ya ziada, etc na mwisho mnakula mabonasi. Halafu mnajiona wajanja kweli.

Unajua mnanishangaza wapi? Ni pale mnaposhangaa kwa nini ufanisi uko chini. Kwa nini wafanyakazi wenu hawajitumi, Kwa nini manesi wanapiga stori saa nane mchana. Kama wehu hivi. Mnaanza kulalammika tena kwamba watanzania wavivu, hawapendi kufanya kazi, etc. Na somehow upeo wenu unakuwa umefungiwa kwenye concrete yabisi yenye ugumu wa ajabu kuweza kuona kwamba pengine attitudes zenu ni moja ya chanzo cha tatizo. Yaani nyinyi ndio chanzo kimojawapo cha matatizo. Badala yake mnaona watu wengine tu ndio matatizo. Nyie akha! Nyie wafanyakazi bora kabisa!

Ng'ombe mtunze vizuri akupe maziwa mengi. Mvutishe bangi akupige pembe. Baadaye utamwambia "si nilikununua? mbona hunipi maziwa na huku wanipiga pembe?". Na unajua atakujibu nini? Atakujibu nothing. Kwa sababu unataka kumpa ng'ombe wako kazi yako ya kufikiri.
 
You are right man.





Sina tatizo na logic zenu. Ila ninapowaona mnashangilia maumivu ya wenzenu (weather ni kwa uzembe wao au la) ndipo naanza kuhisi kuna kitu hakiko sawa.

Attitude mlizonazo ni typical attitude za waajiri wengi, na HR managers wao. Mnatumia ujinga wa watu, au kutokuwa kwao makini, kuwabana kwenye vipengele vya mikataba. Na mnaona hiyo ni sawa kabisa. Yes, mnashinda, mnapunguza cost, mnafanikiwa kuwafanyisha watu kazi ambazo walikuwa hwazitegemei, mnafanikiwa kuwafanyisha kazi watu kupita kiasi bila malipo ya ziada, etc na mwisho mnakula mabonasi. Halafu mnajiona wajanja kweli.

Unajua mnanishangaza wapi? Ni pale mnaposhangaa kwa nini ufanisi uko chini. Kwa nini wafanyakazi wenu hawajitumi, Kwa nini manesi wanapiga stori saa nane mchana. Kama wehu hivi. Mnaanza kulalammika tena kwamba watanzania wavivu, hawapendi kufanya kazi, etc. Na somehow upeo wenu unakuwa umefungiwa kwenye concrete yabisi yenye ugumu wa ajabu kuweza kuona kwamba pengine attitudes zenu ni moja ya chanzo cha tatizo. Yaani nyinyi ndio chanzo kimojawapo cha matatizo. Badala yake mnaona watu wengine tu ndio matatizo. Nyie akha! Nyie wafanyakazi bora kabisa!

Ng'ombe mtunze vizuri akupe maziwa mengi. Mvutishe bangi akupige pembe. Baadaye utamwambia "si nilikununua? mbona hunipi maziwa na huku wanipiga pembe?". Na unajua atakujibu nini? Atakujibu nothing. Kwa sababu unataka kumpa ng'ombe wako kazi yako ya kufikiri.


Sasa wewe mwenye kujua matatizo, mwenye empathy, mwenye akili ya kujua tatizo ni sisi...umefanya nini??
 
You are right man.

Sina tatizo na logic zenu. Ila ninapowaona mnashangilia maumivu ya wenzenu (weather ni kwa uzembe wao au la) ndipo naanza kuhisi kuna kitu hakiko sawa.

Attitude mlizonazo ni typical attitude za waajiri wengi, na HR managers wao. Mnatumia ujinga wa watu, au kutokuwa kwao makini, kuwabana kwenye vipengele vya mikataba. Na mnaona hiyo ni sawa kabisa. Yes, mnashinda, mnapunguza cost, mnafanikiwa kuwafanyisha watu kazi ambazo walikuwa hwazitegemei, mnafanikiwa kuwafanyisha kazi watu kupita kiasi bila malipo ya ziada, etc na mwisho mnakula mabonasi. Halafu mnajiona wajanja kweli.

Unajua mnanishangaza wapi? Ni pale mnaposhangaa kwa nini ufanisi uko chini. Kwa nini wafanyakazi wenu hawajitumi, Kwa nini manesi wanapiga stori saa nane mchana. Kama wehu hivi. Mnaanza kulalammika tena kwamba watanzania wavivu, hawapendi kufanya kazi, etc. Na somehow upeo wenu unakuwa umefungiwa kwenye concrete yabisi yenye ugumu wa ajabu kuweza kuona kwamba pengine attitudes zenu ni moja ya chanzo cha tatizo. Yaani nyinyi ndio chanzo kimojawapo cha matatizo. Badala yake mnaona watu wengine tu ndio matatizo. Nyie akha! Nyie wafanyakazi bora kabisa!

Ng'ombe mtunze vizuri akupe maziwa mengi. Mvutishe bangi akupige pembe. Baadaye utamwambia "si nilikununua? mbona hunipi maziwa na huku wanipiga pembe?". Na unajua atakujibu nini? Atakujibu nothing. Kwa sababu unataka kumpa ng'ombe wako kazi yako ya kufikiri.

hamna mtu anayefurahia, wewe umeleta mjadala lazima usikilize watu wenye view zingine na uondoe emotions zako

tunachokuweleza hapa ni mikataba ya kazi ndio ilivyo, hata bank unaweza ukaajiriwa dept nyingine lakini wakiwa wamezidiwa sehemu moja ukapelekwa sehemu nyingine

hiyo hospitali ni charity????

kuna mawili huyo mwenye hospitali ampunguze kazi ndugu yako na ajiri watu wa usafi ambao ni cheap zaidi na watafanya kazi au awe na manesi wawe wanafanya kazi sehemu zote....

ngojea nikupe darasa la ku run bussiness kidogo
1.hospitali ikiwa kubwa unaweza ukawa na watu special kwa ajili ya usafi ambao ni watakuwa 24/7.
2.hospitali ikiwa ya kawaida inaweza ikawa na watu wa usafi wanakuja kufanya usafi asubuhi na kuondoka, alafu baadae wafanyakazi wengine wanapokezana kufanya usafi kwa ajili hospitali inatakiwa iwe clean saa zote na si asubuhi tu ili kuzuia mlipuko wa magonjwa
3.hospitali ikiwa ndogo inabidi na watu wajibane

kwa hiyo ndugu yako atakuwa ameangukia kwenye 1, 2 au 3....
 
Sasa wewe mwenye kujua matatizo, mwenye empathy, mwenye akili ya kujua tatizo ni sisi...umefanya nini??

Nothing! Kama wewe umefanya kitu, kudos!

Haya, Umeshinda kwa hili mama. Sincerely, samahani kwa kukuudhi.

hamna mtu anayefurahia, wewe umeleta mjadala lazima usikilize watu wenye view zingine na uondoe emotions zako

Asante kwa ushauri mzuri. Na natumaini sisi sote tutaufuata.

tunachokuweleza hapa ni mikataba ya kazi ndio ilivyo, hata bank unaweza ukaajiriwa dept nyingine lakini wakiwa wamezidiwa sehemu moja ukapelekwa sehemu nyingine

Mimi sijawahi sign mkataba wa kazi unaoniambia kwamba naweza kuhamishiwa sehemu yoyote, ila nakubaliana na wewe kwamba wapo wanaopewa mikataba ya aina hiyo. Emotions aside, pengine utakuwa umekosea kama unamaanisha "mikataba ya kazi ndivyo inavyotakiwa iwe" au "mikataba yote ya kazi inakuwa na vipengele hivyo". Kama ulikuwa humaanishi hivyo ni vizuri, lakini nadhani argument yako inaweza kum-misslead mtu na kumwambia ategemee mkataba wake utakuwa hivyo, na kwamba hiyo ndiyo kawaida, na kwamba hana budi bali kukubali tu.

hiyo hospitali ni charity????

Hapana sio charity muheshimiwa. Ila, emotions aside, kutokuwa charity hakuhalalishi unyonyaji. Na kumbukumbu yangu hafifu inaniambia hata wakoloni hawakuwa wanafanya charity mitaa hii. Lakini kunawatu walidhani walichokuwa wanafanya mitaa hii si sawa.

kuna mawili huyo mwenye hospitali ampunguze kazi ndugu yako na ajiri watu wa usafi ambao ni cheap zaidi na watafanya kazi au awe na manesi wawe wanafanya kazi sehemu zote....

Sincerely, ninadhani you will make a good manager. Na nadhani una akili ya ujasiriamali ambayo wengi tuliikosa, na wanatupigia kelele kila mahali sikuhizi lakini wapi! Inakuwa ngumu kuipata. :)

Sitanii kwa hili.

ngojea nikupe darasa la ku run bussiness kidogo
1.hospitali ikiwa kubwa unaweza ukawa na watu special kwa ajili ya usafi ambao ni watakuwa 24/7.
2.hospitali ikiwa ya kawaida inaweza ikawa na watu wa usafi wanakuja kufanya usafi asubuhi na kuondoka, alafu baadae wafanyakazi wengine wanapokezana kufanya usafi kwa ajili hospitali inatakiwa iwe clean saa zote na si asubuhi tu ili kuzuia mlipuko wa magonjwa
3.hospitali ikiwa ndogo inabidi na watu wajibane

kwa hiyo ndugu yako atakuwa ameangukia kwenye 1, 2 au 3....

Asante mkuu. Kama nilivyosema, you will make a good manager. Na nikipata fadhila yakufanya kazi chini yako, nita-sign tu huo mkataba. Ili mradi tu usiweke kipengele cha kunifanyisha kazi yoyote.

PS: kuweka kumbukumbu zetu sahihi, huyo jamaa sio ndugu yangu, maana naona unarudia-rudia "ndugu yako, ndugu yako, ndugu yako ...". Pia mimi sio niliyeleta hii mada. Asante kwa kuelewa.
 
Nothing! Kama wewe umefanya kitu, kudos!

Haya, Umeshinda kwa hili mama. Sincerely, samahani kwa kukuudhi.



Asante kwa ushauri mzuri. Na natumaini sisi sote tutaufuata.



Mimi sijawahi sign mkataba wa kazi unaoniambia kwamba naweza kuhamishiwa sehemu yoyote, ila nakubaliana na wewe kwamba wapo wanaopewa mikataba ya aina hiyo. Emotions aside, pengine utakuwa umekosea kama unamaanisha "mikataba ya kazi ndivyo inavyotakiwa iwe" au "mikataba yote ya kazi inakuwa na vipengele hivyo". Kama ulikuwa humaanishi hivyo ni vizuri, lakini nadhani argument yako inaweza kum-misslead mtu na kumwambia ategemee mkataba wake utakuwa hivyo, na kwamba hiyo ndiyo kawaida, na kwamba hana budi bali kukubali tu.



Hapana sio charity muheshimiwa. Ila, emotions aside, kutokuwa charity hakuhalalishi unyonyaji. Na kumbukumbu yangu hafifu inaniambia hata wakoloni hawakuwa wanafanya charity mitaa hii. Lakini kunawatu walidhani walichokuwa wanafanya mitaa hii si sawa.



Sincerely, ninadhani you will make a good manager. Na nadhani una akili ya ujasiriamali ambayo wengi tuliikosa, na wanatupigia kelele kila mahali sikuhizi lakini wapi! Inakuwa ngumu kuipata. :)

Sitanii kwa hili.



Asante mkuu. Kama nilivyosema, you will make a good manager. Na nikipata fadhila yakufanya kazi chini yako, nita-sign tu huo mkataba. Ili mradi tu usiweke kipengele cha kunifanyisha kazi yoyote.

PS: kuweka kumbukumbu zetu sahihi, huyo jamaa sio ndugu yangu, maana naona unarudia-rudia "ndugu yako, ndugu yako, ndugu yako ...". Pia mimi sio niliyeleta hii mada. Asante kwa kuelewa.

naona umeamua kunijbu Sarcastically, lakini mimi sina nia mbaya

ndugu yangu watu wengi wakiwa wana sign mikataba ya kazi wanakuwa na furaha, na mara nyingi huwa wana tick tuu, halikadhalika manager wengi unakuta hawawafafanulii watu kazi zao vizuri....
kwa ajili hata mimi kazi yangu ya kwanza nili tick tu kwa furaha nilipoanza kupewa kazi ambazo sizipendi nikaanza kulalamika manager mbaguzi, niliposoma mkataba wangu nikagundua makosa niliyofanya lakini bado nikawa naendelea kulalamika mpaka nilipopata kibarua kingine
kama ana uhakika mkataba wake wa kazi unasema haruhusiwi kufanya kazi sehemu nyingine basi aende kwenye trade union aliyojiandikisha kama hana trade union apambane
 
naona umeamua kunijbu Sarcastically, lakini mimi sina nia mbaya

Watu wabishi utawajua tu :). Yaani kwa sababu tu tunatofautiana kwenye vitu viwili vitatu unataka nipinge tuuu vyote unavyovisema hatakama vingine nakubaliana navyo au at least naona vina-make sense. Mimi sipo hivyo. Kama ninadhani argument yako imekaa mshazari ntakwambia, ikiwa imekaa sawa ntaikubali. Nikiona hakuna discusssion ya issue tena ila inakuwa only peronal, then nina-exit gracefuly. Na kama niliteleza pia nitakuwa mpole.

Nilidhani nikiongeza "sincerely" nitafanikiwa kuonyesha kwamba ninamaanisha hivyo, na kwamba sikuwa na lengo la kutupa sarcasm. Well, looks like it didn't work. Samahani sana.

ndugu yangu watu wengi wakiwa wana sign mikataba ya kazi wanakuwa na furaha, na mara nyingi huwa wana tick tuu, halikadhalika manager wengi unakuta hawawafafanulii watu kazi zao vizuri....
kwa ajili hata mimi kazi yangu ya kwanza nili tick tu kwa furaha nilipoanza kupewa kazi ambazo sizipendi nikaanza kulalamika manager mbaguzi, niliposoma mkataba wangu nikagundua makosa niliyofanya lakini bado nikawa naendelea kulalamika mpaka nilipopata kibarua kingine
kama ana uhakika mkataba wake wa kazi unasema haruhusiwi kufanya kazi sehemu nyingine basi aende kwenye trade union aliyojiandikisha kama hana trade union apambane

Naamini kila mmoja anawajibu wake, na kiwango cha mafanikio yetu kinaendana na kiwango ambacho kila mmoja wetu anatimiza wajibu wake na majukumu yake. Mmoja wetu akishindwa, basi hiyo inashusha kiwango cha mafanikio yetu; hata kama kuna excuse ya maana ya yeye kushindwa kutimiza wajibu wake.

Na moja ya wajibu wa mwajiriwa ni kuangalia mkataba wake na kuhakikisha anakubaliana na hayo atakayo-sign kwamba amekubaliana nayo. Na ninadhani pia ni wajibu wa mwajiri kujiridhisha kwamba mwajiriwa wake anaelewa alichokikubali. Mara nyingi wote wawili wanapata hasara inapotokea mwajiriwa anapokutana na mazingira ambayo hajui kama alikubaliana nayo. Sawa pengine utafanikiwa kumlazimisha akubaliane na hayo mazingira kwa sababu kisheria ndiyo aliyokubaliana nayo (hata kama hakujua hivyo), lakini usisahau kwamba hicho kinaweza kuwa chanzo cha ufanisi mbovu, kutokujituma, etc. Mwisho wa siku sote tunakula hasara.

Sasa jinsi wewe utakavyomwabia huyu mfanyakazi "si uache kazi" pale anapolalama, ndivyo jinsi ntamwabia mwajiri wake "si umfukuze kazi" pale anapolalama kwamba mfanyakazi wake huyo hajitumi.

Jinsi wewe utakavyomwambia mfanyakazi huyo "si uende trade union" pale anapolalama, ndivyo jinsi ntakavyo mwambia huyo mwajiri "si umfukuze kazi" pale anapolalama mfanyakazi huyo hajitumi.

Kwa kifupi ni kwamba, wewe unaona mwajiriwa ndio wa kulaumiwa, mimi naona wote ni wa kulaumiwa.

Na nadhani kunatatizo la msingi pale waajiri wengine wanapofukia ndani ndani ya mkataba vipengele kama hivi ambavyo wanahisi au kujua kwamba mfanyakazi hatovipenda, wakiwa wanatamani sana visionekane until its too late. Na mfanyakazi huyu anapo-sign bila hata kuusoma huo mkataba, waajiri hawa ndio wanafurahi kabisa.

Kama mfanyakazi haridhiki na anacholipwa, na bado unakufanyia kazi, kuna uwezekano mkubwa wote mtakula hasara. Kwetu inakuwa rahisi kumwambia mfanyakazi anayelalamikia hasara yake "si ulisign mwenyewe", lakini vigumu kumwambia mwajiri anayekula hasara yake "pengine unamyonya mwenzio".

Yaani hii inanikumbusha kale kamsemo "They pretend to pay us, we pretend to work".

Siwezi kukuambia kwamba if they prentend to pay you, then you have the right to prentend to work. Ila nitakwambi work hard. Na pengine mwajiri mwerevu anajua kwamba if they pretend to work, you probably are pretending to pay for it.
 
ngojea nikupe darasa la ku run bussiness kidogo
1.hospitali ikiwa kubwa unaweza ukawa na watu special kwa ajili ya usafi ambao ni watakuwa 24/7.
2.hospitali ikiwa ya kawaida inaweza ikawa na watu wa usafi wanakuja kufanya usafi asubuhi na kuondoka, alafu baadae wafanyakazi wengine wanapokezana kufanya usafi kwa ajili hospitali inatakiwa iwe clean saa zote na si asubuhi tu ili kuzuia mlipuko wa magonjwa
3.hospitali ikiwa ndogo inabidi na watu wajibane

kwa hiyo ndugu yako atakuwa ameangukia kwenye 1, 2 au 3....


QWI QWI QWI QWI QWI QWI.........
 
Back
Top Bottom