Managing Director - TANESCO

Tangazo na qualifications poa. Je hawajaweka mtu wao tayari na hii sio formality tu?
Mashirika mengine wanapewa kishkaji tu , mara Raisi kamteua fulani kuwa mkurugenzi shirika fulani .......na bla bla kibao.

Wakuu wa mashirika wanapaswa waombe kazi wafanyiwe interview na due diligence kabla ya kupewa ofisi. Waliopewa kishkaji ndio hao wameyaua yote. Kodemet

.........trust me..............hapo ni wewe tu ku-apply hakuna cha mtu wao wala nini, nashauri watu waombe.........uki-qualify utaitwa.......kwenye usaili.....sas ahapo kazi itakuwa kwako kuwa-convince.............
 
Katika magazeti ya jana jioni Badra Masoud ambaye ni afisa uhusiano na habari wa Tanesco amesema hatambui hilo tangazo limetoka wapi na kuyatahadharisha magazeti yaliyotoa tangazo kuwa wasitegemee malipo kutoka tanesco.
Ukweli ni kwamba Badra hakuwa anafahamu na si yeye tu kwani baadhi ya viongozi wa juu na wenyewe hawakuwa na taarifa kama vile Kiongozi wa chama cha wafanyakazi.

Bodi ya Tanesco iliweka jambo hili kama SIRI kubwa ili kuhepuka maneno ya upotoshaji ndani ya shirika na hasa majungu.

Ila Badra alipaswa kuwasiliana na viongozi wa Bodi na kupata taarifa sahihi na si kutoa taarifa kama hii kwani magazeti hayawezi kutoa tangazo bila ya order form.

Mkataba wa Dr. Rashid umemalizika ulikuwa ni wa miaka mitatu na yeye ameomba kutoendelea na mkataba jambo ambalo ni la kawaida kabisa. Naipongeza sana Bodi na Serikali kwa Kuonyesha mfano mzuri wa kutangaza nafasi nyeti kama hii hili ni jambo zuri kwani inaonyesha UWAJIBIKAJI NA UWAZI, sasa tunaona tunafaa tutume maombi na kutoa mawazo ya KUJENGA na si kendelea kulalamika kwani nchi haijengwi na malalamiko bali mawazo na mbinu za kuleta maendeleo.
 
Kwa kawaida MD Tanesco anaripoti kwenye Bodi, embu tujikumbushe hiyo taarifa hapo chini wakati alipo jiuzulu:
____________________________________________________________________________

Dr Rashid officially resumes duties at Tanesco

2007-11-27 15:12:39
By Judica Tarimo
The Board of Directors of the Tanzania Electric Supply Company (Tanesco) yesterday accepted the decision by the firm�s Managing Director, Dr Idris Rashid, to withdraw his resignation letter.

Rashid tendered the letter to the board on Wednesday last week, with sources saying he had differed with board members over plans to hike power tariff and service connection charges.

However, he changed his mind the very next day and notified the board accordingly in writing.

``The Tanesco board of directors discussed his (second) resignation withdrawal letter this morning and accepted it unanimously and unconditionally,`` said board chairperson Fulgence Kazaura in an exclusive interview with this paper yesterday.

``Initially, the MD had indicated that he had decided to withdraw his resignation without any conditionality. Now the board has also accepted his decision unconditionally,`` he added.

The official endorsement of Dr Rashid�s second letter came as an additional item on the agenda of a meeting of the board held in Dar es Salaam yesterday to deliberate on the company`s budget and corporate business plan for next year.

Elaborating, Kazaura explained that discussion of the MD`s letter was not among the meeting`s salient features or core businesses but was �an additional but important part of our agenda�.

The Tanesco MD�s resignation move touched off perhaps as many conflicting views from energy stakeholders and the public as did his follow-up decision. However, Kazaura pointed out that Dr Rashid had decided to resign �completely on his own volition and without any conditionality�.

He added: �We have received a letter from Dr Rashid in which he says he is retracting his resignation effective from today. The board members will decide on this second letter after going through it.�

The Energy and Water Utilities Regulatory Authority (Ewura) recently turned down a request by the power supply firm to hike power tariffs and service connection charges, insisting that wananchi publicly air their views on the matter first.

Local media reports had earlier reported that Tanesco had sought to have power connection charges and tariffs hiked by over 100 and 40 per cent, respectively.

Tanesco was out to hike the connection charges beginning this month and the tariffs by January but there have been nationwide calls against the plans, and hence Ewura�s intervention.

Following Ewura`s stance, Tanesco suspended the installation of new service lines and introduced an arrangement under which new customers would have to buy all the equipment needed for installing service lines.

Dr Rashid`s resignation threat came only days after the company`s plans had hit the wall, denied mandatory approval from Ewura.

It is widely believed that the MD, a former Bank of Tanzania governor, has won credit from the country`s development partners over the management of the company during the one year or so he has been in charge.

SOURCE: GUARDIAN
Comment on this article
 
Dk Rashid kuachia ngazi Tanesco

Source: Habari Leo

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Dk. Idris Rashid ataachia ngazi katika shirika hilo Novemba mwaka huu.

Dk Rashid amesema jana kuwa, hana mpango wa kuendelea kuiongoza Tanesco atakapomaliza mkataba wake, anahitaji kupumzika.

Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo imetangaza nafasi ya kazi ya Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, mwisho wa kuwasilisha maombi ni tarehe mbili mwezi ujao.

“Mimi sitaomba tena nafasi hii na sina interest (nia) kabisa ya kuendelea kuliongoza shirika hili”, amesema na kubainisha kwamba, umri wake ni wa kustaafu.

“Umri wangu ni zaidi ya miaka 60, huu ni muda wa kustaafu na ndiyo umeshafika nahitaji kupumzika” amesema kiongozi huyo aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT).

Kwa mujibu wa tangazo hilo lililochapishwa jana kwenye vyombo vya habari, Bodi ya Wakurugenzi imetangaza nafasi hiyo kwa mtu mwenye sifa ya shahada ya Uhandisi wa umeme au Uongozi na uzoefu wa kazi wa miaka si chini ya 15.

Kuna taarifa kwamba, kutangazwa kwa nafasi ya Dk. Rashidi kunatokana na shinikizo kutoka ngazi ya juu ikiwemo Wizara ya Nishati na Madini.

Chanzo cha habari kimeeleza kwamba, Dk. Rashid amekuwa na msimamo na kutokubali kuyumbishwa katika uamuzi asiokubaliana nao.

“Wizara (Nishati na Madini) imeishinikiza bodi itangaze nafasi hiyo ili aombe mtu mwingine katika nafasi hiyo ambaye ataonekana kukubaliana na maagizo kutoka juu”, kimesema chanzo hicho cha habari.

Dk Rashid ameakanusha kuwepo kwa shinikizo hilo na amesema “hizo ni ngonjera za mitaani hazina ukweli”.

Miongoni mwa msimamo uliowahi kuonyeshwa na Dk. Rashid ni pale alipojiuzulu wadhifa wake huo kutokana na kutokubali kubadilisha msimamo wake dhidi ya Kampuni ya Saruji Tanga ilipojipatia umeme kwa kupitisha pembeni ya mita ya Tanesco na kulipa kiasi kidogo cha fedha.

Katika uamuzi wake Tanesco iliipiga faini kampuni hiyo Sh milioni 55 na ilipokataa ikakatiwa umeme. Hali hiyo ilisababisha kuwepo shinikizo kumtaka Dk. Rashid arudishe umeme, alikataa lakini umeme ulirudishwa katika mazingira yasiyoeleweka kwa kisingizio kwamba hatua hiyo ingesababisha hasara.

Dk Rashid alipinga uamuzi huo, akajiuzulu.

Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Aloyce Tesha, amesema,hatua ya bodi kutangaza nafasi hiyo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco ni utaratibu wa kawaida na kwamba Dk. Rashid ana kazi ya kuomba nafasi hiyo tena.

“Muda wake (Dk. Idris) unamalizika, hivyo ndiyo maana nafasi imetangazwa. Alikuwa na contract (mkataba) ambao unamalizika mwisho wa mwezi huu. Anayo fursa ya kuomba kama atapenda,” alisema Tesha na kuongeza:

“Huu ndio uwazi na ndio utaratibu wa sasa wa Serikali kwa nafasi kama hizo za Mkurugenzi Mtendaji, Kamishina…kutangazwa na Watanzania wenye sifa kugombea nafasi. Hakuna uhusiano wowote na Bodi kumkataa au Wizara.

“Na uteuzi ukifanyika majina yanakwenda kwa Rais ambaye anachagua anayefaa. Lakini akiridhia, anaweza kuendelea aliyekuwepo.”
 
Duh! balaa.
yaani u-emudii tanesco wameamua watangaze?au ni formalities zinazingatiwa?
 
Huu ni ukweli wa mambo na hakuna kificho. Hii ndiyo inayotakiwa kwa kila nafasi ya juu yaani itangazwe na siyo kupeana chini ya uvungu. Tumesiki ya TANESCO halafu ikafuatia SUMATRA na sasa mashirika mengine ya umma yote yaliyosalia nayo habari iwe ni hii hii.

Nauliza, mbona kule TIB nafasi haikutangazwa ila akateuliwa tu jamaa mmoja toka BOT kule kwa viongozi MAFISADI namba moja. Sasa tunasubiri tusikie kule Benki ya posta maana em-dii wao naye ana miaka 15 sasa ya mkataba tangu aingie madarakani anapewa tu kila mkataba ukimalizika. Wakuu tunasubiri kwa hamu naye tumwone.
 
Lakini tangazo lenyewe mbona limekaa ndivyo sivyo? linasema muombaji awe na digrii ya uhandisi AU utawala,hii imekaaje wadau,yaani inayumkinika umwambie mwombaji awe na digrii ya udaktari au sheria kwa kazi hiyo hiyo moja? inakuja kweli au iko namna ili xyz atengenezewe ulaji hata kama hana sifa? kwa nini wasiseme tu kwamba mwombazi awe na digrii ya uhandisi na shahada ya uzamili ya utawala (MBA au Msc Management)?

I don't anything wrong with the advert may be ur reading a different text. PhD is not a basic qualification. Lazima utofautishe basic qualification na added qualification katika maombi ya kazi na ukisoma kwa makini hilo tangazo liko sawa katika kutofautisha hizo sifa.
 
Ngoja nijitose nipambane interview!! Ila pale kuna changamoto nyingi sana kikazi. Inahitaji moyo mkuu.
 
Sijapata maelezo ya kina kwamba nini kilimsibu Dr Idris huko TANESCO? Je ni majungu au kashindwa ku deliver?
 
Yaani nafasi ya MD wa kampuni (taasisi) kubwa kama hii inapewa muda wa kutangazwa wa mwezi mmoja tu?! Aliyekuwepo amepotea ghafla? Ameondolewa ghafla au amejiuzulu ghafla?

Ni cheo kikubwa na ni taasisi muhimu. Nafasi kama hii inatumia zaidi ya miezi 3 kupata a reliable candidate. Au basi si wateue mwingine tu kama ilivyo kawaida... kwani aliyepo sasa hivi nafasi yake ilitangazwa?!
 
Sijapata maelezo ya kina kwamba nini kilimsibu Dr Idris huko TANESCO? Je ni majungu au kashindwa ku deliver?
Mkuu Jibu lako hili hapa chini na kwa wengine wenye utata na mabadiliko makubwa yanayokuja ndani ya shirika:
---------------------------------

Ufisadi TANESCO wamtisha Ngeleja

Source: Tanzania Daima

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amesema ameshtushwa na taarifa za ufisadi mwingine unaodaiwa kufanyika ndani ya Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO), na kwamba anakusudia kuunda tume kuchunguza tuhuma hizo, huku akiahidi kuchukua hatua kali dhidi ya watakaobainika kuhusika.

Akizungumza na Tanzania Daima katika mahojiano maalumu, Waziri Ngeleja alisema taarifa za ufisadi huo amezipata kupitia vyombo vya habari na kuahidi kuzifanyia uchunguzi wa kina mara moja na baadaye kutoa matokeo kamili.

"Nilikuwa safari jimboni kwangu, ndiyo nimerudi, nitalifuatilia kwa kina na kulitolea majibu haraka, kama ni kweli wamejiingiza katika mkataba kama huo ni kosa.

"TANESCO inafanya kazi kupitia bodi na mkono wa serikali, pale ni hiyo bodi, kama kuna maamuzi yamefanyika nje ya maamuzi ya kikao halali cha bodi, tutajua," alisema Ngeleja.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyoripotiwa hivi karibuni, mmoja wa wajumbe wa bodi ya TANESCO anadaiwa kuwa ni mkurugenzi katika Kampuni ya Strategies Insurance Limited and PharmaAccess International iliyopewa zabuni nono.

Taarifa hiyo ilidai kuwa kuna harufu ya ufisadi ndani ya shirika hilo wa sh bil 1.4, ambapo TANESCO imeingia mkataba wa bima ya afya wenye thamani ya sh bilioni 3.7 na kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi wake kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Taratibu zinataka kama mjumbe wa bodi ana mahusiano na shirika au taasisi inayoomba zabuni ya kutoa huduma au mali, atoe taarifa kwa maandishi ya kuelezea maslahi yake ili asihusishwe na mchakato unaohusu kampuni yake.

Mkataba huo ulisainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Dk. Idris Rashid na Sanjay Suchak kwa niaba ya Kampuni ya Strategies Insurance Limited na Consortium of Alexander Forbes (T) Ltd.

Baadhi ya watu walioshuhudia utiaji saini mkataba huo, ni pamoja na mwanasheria wa TANESCO, Godson Makia na Dominic Osumo, ambaye aliiwakilisha Strategies Insurance Limited and PharmaAccess International.

Hii itakuwa tume ya pili kundwa ndani ya shirika hilo baada ya ile inayoendelea kuchunguza tuhuma zilizoanikwa na Mbunge wa Sumve, Richard Ndasa kuwa kuna ubadhirifu wa zaidi ya sh bilioni 1.4 ndani ya shirika hilo la umma.

Ndasa alisema shirika hilo limetumia kiasi hicho kikubwa cha pesa kwa ajili ya kukarabati nyumba 17 zilizopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, fedha ambazo kimahesabu, zinatosha kujenga nyumba kama hizo zaidi ya 20.

Alizitaja nyumba hizo zenye harufu kali ya ufisadi kuwa ni pamoja na ile iliyopo katika kiwanja namba 13, Mtaa wa Pore ambayo ilikarabatiwa kwa sh milioni 600 na imeuzwa kwa kigogo mmoja wa TANESCO kwa sh milioni 60.

Nyumba nyingine ni namba 89 iliyopo katika barabara ya Guinea, ambayo imekarabatiwa kwa sh milioni 250, nyumba namba 65 iliyopo Oysterbay iliyokarabatiwa kwa zaidi ya sh milioni 195 na nyumba namba 459 iliyopo katika Mtaa wa Mawenzi ambayo imekarabatiwa kwa zaidi ya sh milioni 130.
 
Hivi mtu ukisoma lazima uwe fisadi? hivi kwa nini kusiwepo na sheria ya kuwa funga maisha wale wote wanaofanya ufisadi? kina niuuma sana
 
hawa wanaojiita strategies insurance ni mafisadi wakutupwa nashangaa wanaoperate vipi hapa tanzania.mfano mzuri hapa kazini kwetu kila mfanyakazi amekatiwa bima ya matibabu milion 10m kwa mwezi, pamoja na dependants wako kama wanne!! halafu kuna mashrti kama million namana ya kutibiwa na hiyo hela! hapo well tunajua umetembea ufisadi hapa,si haba,mimi na familia yangu 40million per yr,ukiugua ukakatwa laki 1 unaitwa kutoa maelezo,sasa ndo maana yake nini,so hata Tanesco kama ndo hivyo.
 
Back
Top Bottom