Mambo ya techsupport tumetoka mbali

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Kuna wakati tuliwahi kutembelea na rundo la CDs bila kusahau Floppy Discs ambazo ndani yake kuna programu mbalimbali za kutumia Kwenye komputa au ni programu zinazotumika kusaidia katika kuifanya HDD ionekane wakati unapotaka kuinstall Windows wakati huo ni windows 9x .

Ukitaka kuinstall windows kwa mfano ulihitaji programu ya kuboot ambayo ilipatikana Kwenye floppydisc hivi bootable floopydisk ziliweza kutengenezwa kutumia Komputa yenyewe ukishamaliza kuinstall au kutumia nyingine ambayo imewahi kuwa installed na wale wenye kuweza kutumia mtandao waliweza kuzishusha kutumia mtandao .

Hapo bila kusahau cd iliyokuwa na operating system kama ni windows 9x au chini yake au aina nyingine ya operating system lakini nitaongelea zaidi windows ndio maana natumia 9x wakati mimi naanza masuala haya nilikuta windows 9x , kwahiyo bila bootable floppy disk huwezi kutumia cd ya windows 9x kwa ajili ya kuinstall hata windows NT na Windows Me na 2000

Baada ya kuinstall windows ulihitaji drivers za vitu mbalimbali Kwenye komputa hiyo kama modem wakati huo mtandao haukupanuka sana ulihitaji modem kwa lazima kwahiyo driver zake lazima uwe nazo nakumbuka tulitakiwa kuwa na cd mbalimbali zenye driver za modem ili ikitokea tu uweze kutumia cd hizo .

Muda ulibadilika sasa ikaja windows 98 sp2 ambayo ilikuwa inauwezo wa kuboot yenyewe bila kutumia msaada wa floopydisk na hapa ndio mabadiliko makubwa yalipoanzia , kuanzia hapo vitu na mambo hayajawahi kuwa sawa tena kama ilivyo mwanzo .

Sasa tuna mpaka dvd unazoweza kuhifadhi operating systems kuanzia windows vista mpaka windows 7 na programu nyingine nyingi nyingi sana tatizo na drivers hakuna sana kwa sababu kampuni zote zinazotengeneza bidhaa hizi zinaweka driver za bidhaa zao bure Kwenye tovuti zao kwa ajili ya kuchukuwa na kwenda kutumia

Kuna hata baadhi ya programu kama driver magician ambayo inauwezo wa kutafuta driver stahili za komputa yako na kukupa linki ya moja kwa moja kwenda katika wavuti unaoweza kupata driver hiyo ukiwa na mtandao unaweza kuzishusha na kuzitumia hapo hapo bila shida yoyote .

Hata mtandao umesambaa sana na kutokana na kuunganishwa na mkonga wa mawasiliano uliopita baharini hakuna tena hadithi za drivers na hata programu zingine ndogo ndogo ukiongelea drivers wengi wanaweza kukushangaa kwa sababu zinapatikana kwa urahisi zaidi kuliko wakati wowote ule .

Enzi hizo kulikuwa na watu wachache sana wanaofanya shuguli za ICT haswa masuala ya ufundi pamoja na vifaa vya kufanyia kazi kuanzia programu mpaka aina nyingine ya vifaa vidogo vidogo na hata wakati mwingine vifaa hivyo vilikuwa ni bei kubwa kuweza kuvipata na kutumia na zaidi ni kwa wataalamu hawa kulipwa hela kidogo kuliko ilivyosasa hivi fani hii ilivyopanuka na kuwa na vitengo mbalimbali pamoja na kampuni nyingi kuanzishwa haswa za kimataifa .

Hii ni pamoja na kuwa na kampuni nyingi zaidi zinazotoa kwa mfano huduma ya mtandao kwa wateja , makampuni ya simu ambayo yanahuduma mbalimbali na nyingi zinazohitaji watu wa ICT Kwenye kushugulika nazo pamoja na kuwa na chombo cha kusimamia masuala mengi ya mawasiliano nchini hii imesaidia sana katika kuweka mambo mengi sawa Kwenye suala zima la mawasiliano .

Ukija Kwenye masuala ya programu na kadhalika enzi hizo kulikuwa na programu chache sana na ambazo hazikuhitaji mfano memory kubwa Kwenye komputa katika utendaji hata nafasi kubwa ya kuhifadhi Kwenye komputa kwahiyo mambo mengi yaliweza kufanyika .

Tukija Kwenye masuala ya programu za ulinzi kama antivirus na firewalls pamoja na spyware enzi hizo ni antivirus zilizokuwa na soko kubwa sana , firewalls hazikuhitajika sana haswa kwa watu ambao walikuwa hawajaunganishwa Kwenye mtandao

Hizi antivirus zilikuwa nyingi na uwezo wa kufanya kazi 3 tu nayo ni kuscan virus , kuondoa na kulinda tu , enzi hizo hakukuwa na matishio kama spyware na aina nyingine ya matishio kwa njia ya mtandao nakumbuka nilitumia sana Norton antivirus na updates zake niliweza kuhifadhi Kwenye floppydisk au zippdrive wakati huo ilikuwa ni mb chache tu .

Wale waliokuwa wanatumia bidhaa za mcafee wanakumbuka jinsi ilivyokuwa rahisi kuweka updates Kwenye floppydisk lakini ilivyokuwa kazi kuhifadhi stinger Kwenye floppy hizo hizo kwa ajili ya kuscan virus na kuondoa Kwenye kompyuta wakati huo jina lake lilikuwa ni hilohilo stinger na ilikuwa maarufu sana kwa sasa stinger imebadilishwa jina kutokana na kutengenezwa virus zilizokuwa na uwezo wa kuharibu programu hiyo kwa sasa sijui nani anatumia stinger toka mwezi wa 10 mwaka jana sijaona updates zake .

Hivi ninavyoandika sasa hivi update ya mcafee virus scan 8.7 imekuwa na ukubwa wa zaidi ya mb 110 na kila siku ukubwa wake unazidi kuongezeka kwahiyo kuna vifaa zaidi ya kuweza kuhifadhi update hii unaweza kuamua kuichoma Kwenye cd au kuhifadhi Kwenye flashdisk na aina nyingine ya vichomeka ambavyo ni vikubwa zaidi vya kuhifadhi vitu hivyo .

Unapohifadhi Kwenye flashdisk napo kunaweza kuwa na madhara yake kama unaenda kuitumia Kwenye komputa yenye virus , virus hao wanaweza kuathiri update hiyo kwahiyo ni bora kuhifadhi Kwenye cd ambayo virus haina uwezo wa kujiandika Kwenye cd hiyo .

Wakati huo pia hakukuwa na shida kubwa kwenye masuala ya leseni za baadhi ya programu pamoja na operating system kwa sasa unahitaji sana leseni ambayo ni yako kwa ajili ya kila programu iliyoko Kwenye komputa yako unayotumia hili ni lazima hata zile programu za bure zote zina leseni yake utaona wakati unaingiza imendikwa leseni yake na ni lazima kukubaliana na maazimio yaliyoandikwa kwenye leseni hiyo .

ITAENDELEA
 
umesema kweli kabisa, last week machine yangu moja xp pro ili-crash. nadhani bios zilikuwa corrupted or something, recovery ya kawaida ikashindika ikabidi nifanye clean install.

lakini ilikuwa rahisi kwangu ku-receover data kwasababu ya back up niliyokuwa nayo, lakini future iko simplified. ukiwa na usb thumbdrive unatembea na OS unayopenda mfukoni. i like your posts, ziko tofauti na jamaa zangu wa ku-lift magazetini.
 
Back
Top Bottom