Mambo ya Mohamed Dewji

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
Mohammed Dewji Blog » Blog Archive » MHUBIRI ALIYEFUNGWA KWA KULAWITI AONGEZEWA KIFUNGO KWA KUJARIBU KUTOROKA…!!!

Mhubiri mmoja nchini Kenya anayetumikia adhabu ya kifungo cha miaka 21 katika gereza la Kitui kwa kosa la kulawiti ameongezewa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu zaidi baada ya kujaribu kutoroka akiwa mikononi mwa sheria.

Mhubiri huyo ambaye kwa sasa ni mfungwa Jeremiah Munyoki wa Kanisa la Jesus Worship Centre lililopo Mathulini huko Kitui, alitoroka akiwa katika hospitali ya wilaya ya Kitui alikokuwa amelazwa kwa kipindi cha wiki moja akiugua Malaria.

Mwendesha mashtaka Inspekta Kenndy Apidi ameiambia mahakama kuwa mfungwa huyo alimtoroka askari magereza aliyekuwa akimlinda hospitalini hapo na kuruka fensi ya hospitali na kukimbia hadi katika kichaka kilichokuwa karibu.

Hata hivyo maafisa wa polisi jamii wa mji wa Kitui walimuona na kumtilia shaka kutokana na kuvaa sare za wafungwa, hivyo kumkimbiza na hadi kumkamata na kumkabidhi kwa wahusika.

Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama ya Kitui Beatrice Kimemia, ambaye hapo awali alimhukumu mhubiri huyo kifungo cha miaka 21 kwa kosa la kumlawiti mvulana wa miaka 13, amemuelezea mtuhumiwa huyo kama mtu asiyejutia makosa yake.


MO BLOG kwa mara nyingine inakemea tabia kama za mhubiri huyu, ambaye alipaswa kuwafundisha maadili watu ikiwa ni pamoja na watoto wanaokuwa akiwaonyesha njia iliyosahihi, lakini kinyume chake ndiye amekuwa baradhuli wa kuharibu vijana.

Wadau mnadhani nini kinawakumba hawa viongozi wetu wa kiroho hadi wanafikia hatua kama hii ??

Maana tunaamini ukiwa mcha Mungu toka moyoni huwezi kufanya kitendo kama hicho, au siku hizi wengi wanakuwa watumishi wa kiroho kwa sababu ya maslahi ??

Je wadau kwani utumishi wa Mungu unamaslahi yeyote ??

Maana inaonekana wengi hawana wito…….Tusaidieni hili jamani…!!!!
 
Nimeiona mkuu, nadhani ameama kutoka na muhadhara kwenye mtandao, tulieni mtaona badae itakavyokuwa!
 
Nimeiona mkuu, nadhani ameama kutoka na muhadhara kwenye mtandao, tulieni mtaona badae itakavyokuwa!

hata mimi sijaelewa kwa nini kaiweka kitu kama hii ukichukulia yeye ni mmbunge na blog yake angeitumia zaidi kwenye mambo ya jimbo lake , kwanza stori yenyewe ya Kenya kaiweka kwa kisa gani?
 
Naona wameanza kutoka na mihadhara! tatizo lao ni shule bora waende shule wakasome waachane na madrass ndo inwafanya wabaki mamburura tu!
 
Back
Top Bottom