MNDEE
JF-Expert Member
- Jul 10, 2009
- 491
- 68
Kwa kuwa mila yenyewe huijui sana (maelezo yake na sababu zake), jaribu jkuulizia kule nyumbani wakueleze sababu ya katazo hilo: yawezekana ni sababu nzuri na nzito kabisa, huwezi kujua. Wakishakueleza - ukiona ni sababu isiyo na uzito - unaweza pia kuwaelimisha wazazi na wana-ukoo juu ya kilicho cha kweli: kwamba kutoka sehemu moja si kizuizi cha ndoa kama si undugu wa damu. Wakikuelewa utakuwa umepata pasi ya kuingia ndoa bila bughudha au kuwatia simanzi wazazi wako. Huenda katazo hilo linasababishwa na kutaka kuzuia tabia fulani mbovu au ugonjwa fulani wa kurithi ambao eneo lenu upo. Kwa hiyo kwa kutaka kutomeza polepole tatizo hilo wazee wakaweka katazo hilo ili kuwafnya watu wa eneno lenu waende mbali kuoa na kuchanganya damu na watu wengine wasio na athari hizo mbaya za eneo lenu. Huu ni mfano tu.
Tawire mkuu, kuna jamaa mmoja alitaka kuoa binti mmoja wazee including baba yake wakamkatalia katu katu na hakuna sababu ya maana wanampa, kijana akagangamala akao, baadae akagundua kumbe baba yake alizaa na shangaza wa yule binti aliyeoa. Wazee hawakuipenda ile picha, kijana yuko na mkewe mpaka leo.