Mambo ya kwa Babu LOLIONDO

Kama watu wanapona, muache atibu hadi hapo atakapofikia.
Hayo yakumpima kama ni hiki au kile maadam hatabiri huyo ni mtu wa mungu. Kabla ya dini zote hizi babu zetu walitibu kwa miti shamba.
Nenda ukanywe dawa mkuu!
 
Waacheni watu wa Mungu wapate uponyaji....ni wangapi wamefariki bila kupata tiba hii? Hii ni Neema na jina la Bwana litukuzwe! Kama tiba inasaidia na kuokoa uhai wa watu wengi tatizo ni nini? Nawatakia wote uponyaji mwema!
 
Nisawa kabisa watu waende wapate dawa na kama wanapona hapo hamna tatizo lakini pia si vibaya kutafakari usahihi wa tiba maana watu wanaweza wakaacha hata kutumia dawa za kurefusha maisha then baadae waje kuzikumbuka when it is too late kumbukeni na DECI walianza watu wa mungu mwisho wake ikawa kilio.
 
wewe uliyeleta mada inaonekana una imana haba sana.....yule babu toka mwaka 1991 june Mungu anamwambia kupita ndoto ..ponya watu wangu....toka 1991 umeelewa kaka...mpka mwaka jana agos ndo akaanza kutibu mtu mmoja mmoja..hajawahi kutangaza redion kama kina ndodi..ila wanaopona ndo wamesambaza habari hizo......

na mungu alimwambia kuwa gharma yake iwe mia tano tu......nenda kwa babu......angekuwa mwingine toka 1991 unaota kitu kile kile angekuwa ameshakurupuka mda mrefu...hivi hukumsikiliza wakati anahojiwa?

juice ya babu...iko poa sana..shemji kapona kisukari
 
Mimi sitaki kumkani huyu babu kwamba yeye ni wa Mungu lakini Neno la Mungu linasema tuzipime hizo roho.

rai yangu watu wa Mungu nisaidieni niweze fahamu ninyi ambao mmesha zipima hizo roho je ni kweli huyu ni mtu wa mungu na siyo anasaidiwa na Mizimu ya mahalia na ndiyo sababu hawezi amishia huduma yake sehemu nyingine? Na hivyo mizimu hii imekuja kwa Sura ya Malaika wa Nuru.

Wasi wasi wangu isije kuwa tunakwenda kwa Mganga wa Kienyeji tukuifikiri ni mtu wa Mungu, yaani nalataka ni watu wajue kuwa ile ni nguvu ya Mungu au la ingawa inaponya.

Nawasilisha
Mungu awabarikLi sana!

Yohana 9:
9:1 Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu mmoja, kipofu tangu kuzaliwa.
9:7 akamwambia, "Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu." (maana ya jina hili ni "aliyetumwa"). Basi, huyo kipofu akaenda, akanawa, kisha akarudi akiwa anaona.
9:8 Basi, jirani zake na wale waliokuwa wanajua kwamba hapo awali alikuwa maskini mwombaji, wakasema, "Je, huyu siye yule maskini aliyekuwa akiketi na kuomba?"
9:9 Baadhi yao wakasema, "Ndiye." Wengine wakasema, "La! Ila anafanana naye." Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, "Ni mimi!"
9:10 Basi, wakamwuliza, "Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?"
9:11 Naye akawajibu, "Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: `Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.` Basi, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona."
9:16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, "Mtu huyu hakutoka kwa Mungu, maana hashiki sheria ya Sabato." Lakini wengine wakasema, "Mtu mwenye dhambi awezaje kufanya ishara za namna hii?" Kukawa na mafarakano kati yao.
9:24 Kwa hiyo wakamwita mara ya pili mtu aliyekuwa kipofu na kumwambia: "Mpe Mungu utukufu; sisi tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi." 25 Naye (yule aliyekuwa Kipofu) akajibu: "Kama ni mwenye dhambi mimi sijui. Lakini kitu kimoja najua: Nilikuwa kipofu na sasa naona."
 
Ni kweli kwamba mgonjwa yeyote pamoja na wanaomjali hujaribu kupata tiba yoyote na kwa namna yoyote ili kutibu gonjwa linalomsumbua mgonjwa na jamii yake. Hata kama uwezo wa tiba hiyo haijathibitishwa, bado itatumika tu. Desparation inaweza kumfikisha mtu mzima na akili zake katika situations za ajabu kama simulizi za huko Loliondo.

Wiki mbili zimepita sasa tangu ndugu yangu mmoja yalipomkuta mikasa katika hospitali kubwa tu, Dar es Salaam. Katika hospitali ya kwanza alipewa rundo la mividonge baada ya kudundwa pia sindano nne za kuzuia maumivu na kutapika. Maabara wakasema iko malaria mbili.
Ilipobidi kwenda kwingine baada ya mgonjwa kuzidiwa, na pale wataalamu wakafanya mavipimo yao na kugundua malaria moja pamoja na kitu ingine, ati labda utumbo umejikunja!!! Very contradictory. Hospitali ya tatu (in 36 hours) hata kabla ya kufanya vipimo wakataka kumdundika QUININE 9 based on lab report ya wengine! Baada ya kukataa hayo na kusisitiza vipimo kamili, mgonjwa akakutwa hana malaria hata chembe moja ila alihitaji kuongezewa maji mwilini, kwa maana ilikuwa case ya dehydration!!! Huduma mbovu kama hizi haziwezi kuwa pendeleo la mgonjwa yeyote. Na hii ndo hali halisi unless upo uwezo wa kwend kwa makaburu pale Trauma Centre.

Ya Loliondo yawezekana kabisa kuwa siyo kipimo cha watu kujazwa UJINGA bali ni kile cha watu kukata tamaa na huduma mbovu katika nyanja mbalimabali.
Rundo la watu wanaomiminika kwa matumaini kwenda Loliondo si tukio la kwaida hata kidogo. Nini mindset ya watu wote hao kufuata NENO tu?
Je inawezekana ku-speculate kwamba ni matokeo ya kukata tamaa baada ya miaka 50 ya ubabaishaji wa mijizi ya MAFIA waliomo ndani ya CCM? Leo hii yule Babu mchungaji akiibukia kunadi sera za CDM kama dawa ya matatizo mengine ataitwa mhaini?
 
wkt mwingine Mungu hutumia vinyonge ili kuleta ukombozi mahali fulani!!
 
well its true what youve just said. Lakini sukari huponyeshwa na nini?
Fahamu kwamba Arusha ni Cdm dam damu. Wakeleta hizo haijalishi kitu
 
Dalili za watanzania kujikatia tamaa na maisha yalivyo magumu na hatimaye kupungua uwezo wa kufikiri,hivyo kuamini kila wasikiacho wakitafuta shortcut, ni hatari kwa taifa kufikia hapa.
 
Mimi nakushauri uende kama kweli una matatizo sugu wewe nenda huwezi jua. MUNGU anayo miujiza yake; hakuna mwenye uwezo wa kutibu ila Mungu pekee; hivyo babu kama amepewa uwezo huo ni kutoka kwa MUNGU! Maana nasikia hata UKIMWI anatibu!
 
nakubaliana na wewe japo siwezi kusema ni kwa kiasi gani! Watz wengi sasa tumekata tamaa na tunaamini ushirikina (Story ya CITIZEN of Sunday 27th Feb) na kwa vile 'waumini' hawapendi kujulikana huko, wamejitokeza kwa huyu maana ni MCHUNGAJI! Trends zinaonyesha kuwa uvumbuzi juu ya elimu ya udaktari principles zake ni zile zile na maendeleo ya technology yameiboresha zaidi. SWALI: Ikiwa unaumwa na vipimo viko wazi na ukaambiwa kuchagua kwenda kutibiwa na specialist (say UK/EU, USA, India, SA nk) au kwenda LOLIONDO utachagua nini???
 
Jamani hapa issue ni kupona na si kujadili nani amekuponya.
Labda tusubiri tupate watu watakaoshuhudia kwamba baada ya kutumia ile dawa hawakupona. lakini kama wamepona tatizo liko wapi? Je kuna mgonjwa anahangaika mwaka nenda rudi ambaye hataki kupona?
Tuwaache wale wanaohitaji kupona waende kwa Babu wakapate tiba kwa imani yao bila kuwakatisha tamaa.

''KWAMBA ANATOKA KWA MUNGU AU KWA SHETANI MIMI SIJUI, NINACHOJUA NILIKUWA MGONJWA NA SASA NIMEPONA
 
nakubaliana na wewe japo siwezi kusema ni kwa kiasi gani! Watz wengi sasa tumekata tamaa na tunaamini ushirikina (Story ya CITIZEN of Sunday 27th Feb) na kwa vile 'waumini' hawapendi kujulikana huko, wamejitokeza kwa huyu maana ni MCHUNGAJI! Trends zinaonyesha kuwa uvumbuzi juu ya elimu ya udaktari principles zake ni zile zile na maendeleo ya technology yameiboresha zaidi. SWALI: Ikiwa unaumwa na vipimo viko wazi na ukaambiwa kuchagua kwenda kutibiwa na specialist (say UK/EU, USA, India, SA nk) au kwenda LOLIONDO utachagua nini???

LOLIONDO mwanakwetu
 
nakubaliana na wewe japo siwezi kusema ni kwa kiasi gani! Watz wengi sasa tumekata tamaa na tunaamini ushirikina (Story ya CITIZEN of Sunday 27th Feb) na kwa vile 'waumini' hawapendi kujulikana huko, wamejitokeza kwa huyu maana ni MCHUNGAJI! Trends zinaonyesha kuwa uvumbuzi juu ya elimu ya udaktari principles zake ni zile zile na maendeleo ya technology yameiboresha zaidi. SWALI: Ikiwa unaumwa na vipimo viko wazi na ukaambiwa kuchagua kwenda kutibiwa na specialist (say UK/EU, USA, India, SA nk) au kwenda LOLIONDO utachagua nini???[/B]


Inategemea na ugonjwa unaokusumbua, babu anatibu magonjwa sugu yasiotibika kisayansi.
 
Hii habari ya Loliondo, kwa sasa imechukua mtazamo wa aina yake!!
Watu sasa wamesahau kila kitu wanaelekea Loliondo!!! Kuna maneno yasemwayo kuwa na vigogo wengi tu wanamiminika huko kutibu ngoma...!!!
 
"Kanyaga Babu wa Loliondo, Sambaratisha Babu wa Loliondo, kazi za babu saga"
Nukuu ya Mwananchi Leo 7.3.11 ikimnukuu Kakobe akimwaga maombi dhidi ya Mch. wa Loliondo.

Kakobe aache kumwonea wivu Babu wa watu, mbona yeye anapodai anaponya huo UKIMWI hakuna mtu amejitokeza kumzuia?
 
Inategemea na ugonjwa unaokusumbua, babu anatibu magonjwa sugu yasiotibika kisayansi.

... inasemekana!! Yawezekana ni kweli au ni uzushi mtupu. Ile kitu inaitwa placebo
huponyesha pia lakini at the end si dawa.
Hivi kweli karne hii watu wazima na akili zao wanywe dawa amabayo haina uthibitisho? Au eti, ...tiba aya magonjwa sugu yasiotibika kisayansi na siyo... tiba ya magonjwa sugu ambayo tiba yake haijapatikana? Kisukari? Hypertension?

21st century!! Au hawa ni wale waliodanganyika?
 
Maelezo yako iko kama una uchungu fulani,hasira frustrution n.k. Loliondo ni tiba ya ukweli ''ni tiba mbadala'' na hakika 100% nimempima mtu mara 3 kweli kapona............je? Ulitaka tiba hii ipatikane nje ya tz ndo uamini?????????
 
Back
Top Bottom