Ndugu zangu,
Nimekuwa nikisikia na kusoma mengi kuhusu mambo mabaya ( hasi) yaliyotendwa na JK au chini ya utawala wake kiasi kwamba unaweza kujiamnisha kuwa huyu ni rais wa mambo mabaya tu.
Nadhani kuna umuhimu pia wa kumpa pongezi au kutambua mambo mazuri aliyoyafanya. Naomba tusianza kubeza kama huoni jambo zuri basi usichangie: naanza na machache:
Nimekuwa nikisikia na kusoma mengi kuhusu mambo mabaya ( hasi) yaliyotendwa na JK au chini ya utawala wake kiasi kwamba unaweza kujiamnisha kuwa huyu ni rais wa mambo mabaya tu.
Nadhani kuna umuhimu pia wa kumpa pongezi au kutambua mambo mazuri aliyoyafanya. Naomba tusianza kubeza kama huoni jambo zuri basi usichangie: naanza na machache:
- Kawafikisha mahakamani ''WALIOKUWA HAWAGUSIKI'' BASIL & CO
- Shule za kata zimejengwa
- kajenga na kuboresha UDOM
- Kaboresha (improve) hospital mbalimbali
- Kaendeleza/kaanzisha ujenzi wa barabara
- Kaonyesha ukomavu na kutokuwa na kinyongo angalau kwa mahasimu wake; MFANO KUMTEUA Nagu, Mwandosya, Njoolay etc
- Kajitahidi kuruhusu uhuru wa kujieleza (maana duu wakati fulani tunampaka hadi tunapitiliza- washkaji hapa sio Marekani hii ni Afrika JK mvumilivu sana