Mambo 6 yasiyoweza kusameheka kirahisi katika ndoa/mahusiano

@Mzee Madoshi. I feel you. Hata mie nashangaa sana "mtoto wa nje" kuwa namba wani, wakati mie naona ni faida tu wakiletwa na mie nikawalea. Au weye ni bagheshi ndo kuwa hawajali haya mambo.
 
Mzee Mwanakijiji imetosha baba tufumbulie basi fumbo hili. Naona wote tu wakosaji,hatujamwelewa mtoa maswali yamkini yeye hajalenga katika majibu yote yaliyotolewa.Kwani umesema "ulitarajia kutoa maswali matano sasa kumbe umetoa sita ? Na hivyo ndivyo waalimu huwafelisha wanafunzi" Wengi wamejibu maswali sita huu ni ukosaji wa kutozingatia maelekezo ya mtoa maswali!!
 
Jaribu kuangalia mambo haya sita na uyapange kwa uzito wake wa kusameheka - yaani namba 1 likiwa ni zito kabisa kusameheka hadi 6 jepesi zaidi kusameheka. Yaani lile la kwa 1 kimsingi linaweza kabisa kuvunja uhusiano (definitely) na lile la 6 laweza kushtua au kutikisa kidogo (most probably) lakini linaweza likapita katika historia na watu wakadumu. Ukipenda unaweza ukaelezea kwanini namba zako zivyo hivyo vilivyo.


Kimada/affair nje ya uhusiano (extramarital affair/cheating)
Akaunti za siri (mipango isiyomshirikisha mwenza) - undisclosed accounts
Mtoto wa nje/mtoto wa bwana mwingine
Kupiga au kumuumiza mtu kwa kipigo (domestic violence)
Ulevi/Matumizi ya madawa ya kuleva
Kuingiliwa na wakwe (in-laws intrusion)

Unaweza kupanga yote 6 au kupanga makubwa matatu (your top three). Siji kama wanaume na wanawake tunashindwa kusamehe vitu vile vile au la.

MMM

Kwangu mimi...

Kuingiliwa na wakwe (in-laws intrusion)
Kupiga au kumuumiza mtu kwa kipigo (domestic violence)
Akaunti za siri (mipango isiyomshirikisha mwenza) - undisclosed accounts

...............................
 
Inaonekana suala la "mtoto wa nje" limekuwa katika top 3 za watu wengi sana... labda tuulize kwanini kama mambo yote ni mazuri katika familia lakini hili limetokea mtu yuko tayari kuvunja ndoa? Na hili ni muhimu kwenye level tatu...

a. Labda wanawake wanaona kama mume alienda nje huko kuna uwezekano akapata watoto, na siri kubwa hapa iko ni kwamba mara nyingi mume akizaa nje hakuna dalili ya mwili kwake so wanaume wanaweza siyo tu kuzaa nje lakini hata kulea watoto huko kwingine bila mke kujua. Mara nyingi hili limekuwa likiumbuliwa sana kwenye misiba... ndipo watoto "mnakutana".. Na wapo wanawake ambao wanalichukulia hili kama sehemu ya maisha ya wanaume... hivyo naona wapo wanawake ambao hili likitokea linaweza kutetemesha nyumba bila kuivunja.

b. Sijui ni kwa kiasi gani kwa upande mwingine mwanamme kulea mimba ambayo anajua si yake. Fikiria kwa mfano, ulikuwa safari ya muda mrefu na unaporudi unakuta mwenzako ana mimba - hii ni rahisi kujua kuwa mimba si yako na hivyo kuwa na uchaguzi wa kuendelea na mwenzako au hata kumlazimisha abortion au kuachana naye. Je katika mazingira hayo mwanamme anaweza kukubali ujauzito huo kwa sababu ya mapenzi yake kwa mke wake?

c. Hili la level ya tatu nitaanzishia mada kuamkia kesho kwa sababu litagusa mahali fulani very delicate na "penyewe" hasa...
 
mi naweza samehe yote inategemea tu nimejulishwa wakati gani na je nimegundua mwenyewe au amenitubu kwangu mwenyewe na sababu za yeye kufanya alichofanya ila kitu sitakaa nisamehe ni dharua kwangu

mimi ni

Cheating........kwani ndiyo ianyoleta mtoto wa nje
Undisclosed accounts
Intrusion ya wakwe na hii wakati mwingine inafanyika bila hata wao kujua kuwa wanaingilia ; mathalani kumwita kikao cha siri nyumbani mwanenu hata kama mna nia njema lazima mtajenga picha mbaya kwa mwenzie

Kukiri kosa ndio raha ya msamaha....................na si kusameheana tu pasipokujua unasamehe kitu gani na athatri ni kubwa kiasi gani; mfano; cheati mwenzi atakuomba msamaha kumbe cheating ameifanya na mtu wako wa karibu................ama cheating hiyo imezaaa matunda yaani kuna mtoto amepatikana au ujauzito ambapo wewe huambiwi wakati uombwapo msamaha.......................tusameheane kwa hekima
 
Si mpaka huyo kimada akubali umchukue mtoto wake wa mwaka mmoja umlee wewe. Haya mambo ni more complicated than you think.

God forbid; hata mimi mtoto wa nje atakuwa ni kikomo cha ndoa yangu.


Hizo bold nyengine ni utata; yani unataka kuiba upendo wa mtoto kwa mamaye (mwanamke mwenzio) ufaidike na nini? Jiweke kwenye position ya mwenye mtoto. Hakuna mtu mwenye haki ya kuiba umama wa mwenzie bana hata awe mgumba.

1. Ulevi/matumizi ya madawa ya kulevya,ni kero na uwezekano wa kuwa responsible unapungua. Ni tatizo sana kwangu, labda sababu situmii kilevi cha aina yeyote, hasameheki kabisa.

2. Account za siri(mipango isiomshirikisha mwenza), Kamwe halisameheki sababu atakuwa anaplan kujenga palestina wakati mie najenga Israel, tutakuwa hatuna common oblectives kimaisha.

3. Kimada/affair za nje, hili litategema msimamo wake ni nini juu yangu. Kama ananitambua na kuniheshimu as a wife na kimada ananiheshimu, I can take it na kuendelea kuishi naye. So its 50/50 kuetegemea na tabia ya mwenza wangu

4. Kuingiliwa na wakwe, halisumbui hata kidogo, piga marufuku kija kwangu ni kuwatembelea huko waliko wao na kuwasaidia wakiwa huko huko. No problem at all.

5. Mtoto wa nje, sioni tatizo liko wapi, ni kumchukua haraka akiwa na mwaka mmoja namchanganya na wakwangu na kuwalea kwa mapenzi yote. Inasaidia kwa mwenza kutulia kimawazo akiona watoto wake wote pamoja na kuua connection na mzazi mwenzie. Kuiba upendo wa mtoto wa nje kutoka kwa mama yake mzazi kuja kwangu. Kufanya watoto wote wajione kitu kimoja sabaabu hata ukimkataa mtoto wa nje wa mumeo hauwezi badili ukweli ni wake na ataendelea kuwa wake na ana haki zake. Hata wazazi tukifa watoto watakuwa kitu kimoja na wasaidiana wao kwa wao. Mara nyingi vitu hivi huleta shida sana kwenye mirathi wanaishia kuuza mali zote kwa kutoelewana au kuona wengine ni intruders.
 
1. Ulevi/matumizi ya madawa ya kulevya,ni kero na uwezekano wa kuwa responsible unapungua. Ni tatizo sana kwangu, labda sababu situmii kilevi cha aina yeyote, hasameheki kabisa.

2. Account za siri(mipango isiomshirikisha mwenza), Kamwe halisameheki sababu atakuwa anaplan kujenga palestina wakati mie najenga Israel, tutakuwa hatuna common oblectives kimaisha.

3. Kimada/affair za nje, hili litategema msimamo wake ni nini juu yangu. Kama ananitambua na kuniheshimu as a wife na kimada ananiheshimu, I can take it na kuendelea kuishi naye. So its 50/50 kuetegemea na tabia ya mwenza wangu

4. Kuingiliwa na wakwe, halisumbui hata kidogo, piga marufuku kija kwangu ni kuwatembelea huko waliko wao na kuwasaidia wakiwa huko huko. No problem at all.

5. Mtoto wa nje, sioni tatizo liko wapi, ni kumchukua haraka akiwa na mwaka mmoja namchanganya na wakwangu na kuwalea kwa mapenzi yote. Inasaidia kwa mwenza kutulia kimawazo akiona watoto wake wote pamoja na kuua connection na mzazi mwenzie. Kuiba upendo wa mtoto wa nje kutoka kwa mama yake mzazi kuja kwangu. Kufanya watoto wote wajione kitu kimoja sabaabu hata ukimkataa mtoto wa nje wa mumeo hauwezi badili ukweli ni wake na ataendelea kuwa wake na ana haki zake. Hata wazazi tukifa watoto watakuwa kitu kimoja na wasaidiana wao kwa wao. Mara nyingi vitu hivi huleta shida sana kwenye mirathi wanaishia kuuza mali zote kwa kutoelewana au kuona wengine ni intruders.

Kwangu mie hilo ndio naona gumu, kuna wakwe wanaweza kukufanya ukaiona ndoa chungu. Unaanzia wapi kuwafukuza wazazi wa mumeo au kuwapuga marufuku kufika kwenu?
 
Kwa mie siwezi hata kujua nita react vipi maana hiyo kwangu itakuwa shock ya century.

Ila kwa sasa nikiongelea kinadharia tu; ntadai talaka basi. Simchukii mtoto nachukia process nzima ilomleta mtoto duniani (cheating) na kwa kuwa kuna mtoto maanake hata nikisamehe sitasahau kamwe kwani the kid is there to remind me.

Hivi mnavyosema hamuwezi samehe mtoto wa nje inamaanisha ukiletewa huyo mtoto utadai talaka au utatimua mtoto?
 
Inaumiza sana kuona neno 'mtoto wa nje' linakipaumbele sana katika sababu sita za MMJ
Inaumiza kwa sababu mimi ni 'mtoto wa nje'
Je 'mtoto wa nje' sio mtoto kama walivyo watoto wengine?
Je 'mtoto wa nje' hana haki ya kuwafahamu watoto nusu yake wa baba yake?
Je 'mtoto wa nje' ndiye aliyepelekea baba/mama kufanya aliyofanya
Je haiwezekani kabisa ni sababu ya 'udhaifu' wako wewe ndio ikapelekea baba/mama kuwa na 'mtoto wa nje'
Kwa hali ilivyo siku hizi, magonjwa ya kifo, mpaka kuwe na 'mtoto wa nje' lazima kuwe na sababu ya msingi ya kujadiliwa katika familia
Wazo langu, Suala la affair nje litenganishwe kabisa na 'cheating (hiki kinaweza kuwa kitendo cha haraka sana au hata oral au dhamira tu kama busu ndani mdomoni kabla hata ya tendo), lakini inapofikia kuzaliwa kwa sisi kina 'karume-kenge' mtupe heshima yetu hivyo basi 'mtoto wa nje' iongezwe kama namba 7.

Pole mzee Madoshi...sio nia ya yeyote hapa kuwafanya watoto ambao ni wa nje wajisikie vibaya au kuonyesha hawafai ila ni kwamba tu watu hawakubaliani na wakati/pia namna waliyokuja duniani maana mahusiano yao yanakua yameingiliwa. Sioni kama ni haki kumtaka mtu aliyedanganywa na mtu aliyempenda na kumwamini akubali tu kwamba mwenzake amemdanganya na ushahidi aupokee na kuupenda kama hawezi. We huoni kwamba ni bora mtu akachagua kuondoka badala ya kubaki alafu akupokee huku akiwa amejawa na chuki dhidi yako?Ndo mwanzo wa manyanyaso hao ujue (japo sio wote wanafanya hivyo ila wapo)...wanatabasamu na kusema nimesamehe mkaribishe mtoto nyumbani alafu adhabu ya wazazi wako unapewa wewe.

Kujibu maswali yako....Mtoto wa nje ni mtoto kama mwingine ila sio lazima awe na nafasi nzuri kwa mama aliyedanganywa sawa na watoto wa huyo mama....given the circumstances.

Anayo haki....sidhani kama kuna mtu ameshauri ''mtoto wa nje'' azuiwe asiwafahamu ndugu zake wengine, maana hata huyo mama mwenyewe nyumba akiamua kuondoka haina maana atawaficha hao wengine.

Sio yeye na ndio maana hamna anaesema anawachukia, ila huyo mtoto anakua kumbukumbu ya kudumu ya kilichotokea mpaka yeye kuja duniani. Kwahiyo mtu anapokimbia mahusiano yake anaikimbia hiyo kumbukumbu kwasababu hawezi kuishi nayo.

Heheheheh....hicho ni kisingizio cha wengi wanaotoka kwenye mahusiano yao ila ukweli ni kwamba asilimia kubwa udhaifu upo kwa yule anaetoka nje kwa kushindwa kumweka mwenzake sawa kama ndio tatizo, kwa kuikosea heshima ndoa na mwenzi wake n.k.
 
Hivi mnavyosema hamuwezi samehe mtoto wa nje inamaanisha ukiletewa huyo mtoto utadai talaka au utatimua mtoto?

Kila mtu anafanya kadiri anavyoweza.
Mtu akiamua kwamba anaweza kusamehe na kuendelea na mahusiano yake anaweza kumpokea mtoto au kufanya mtoto asiishi pale (which is the best thing to do in my opinion...kwa wote)....yani sioni kwanini mama mtu atataka kuja kumdump mtoto wake kwa mama wa kambo wakati aliamua mwenyewe kuwa nae na anaweza kumuangalia. Swala la matunzo baba anaweza kuwa anapeleka na kumuona mtoto huko huko....na kama umri wake unaruhusu nae anakuja kusalimia kwa muda mfupi.

Asiyeweza kusamehe anaondoka!!!Kumfukuza mtoto hakubadilishi chochote...
 
Jaribu kuangalia mambo haya sita na uyapange kwa uzito wake wa kusameheka - yaani namba 1 likiwa ni zito kabisa kusameheka hadi 6 jepesi zaidi kusameheka. Yaani lile la kwa 1 kimsingi linaweza kabisa kuvunja uhusiano (definitely) na lile la 6 laweza kushtua au kutikisa kidogo (most probably) lakini linaweza likapita katika historia na watu wakadumu. Ukipenda unaweza ukaelezea kwanini namba zako zivyo hivyo vilivyo.


Kimada/affair nje ya uhusiano (extramarital affair/cheating)
Akaunti za siri (mipango isiyomshirikisha mwenza) - undisclosed accounts
Mtoto wa nje/mtoto wa bwana mwingine
Kupiga au kumuumiza mtu kwa kipigo (domestic violence)
Ulevi/Matumizi ya madawa ya kuleva
Kuingiliwa na wakwe (in-laws intrusion)

Unaweza kupanga yote 6 au kupanga makubwa matatu (your top three). Siji kama wanaume na wanawake tunashindwa kusamehe vitu vile vile au la.

MMM

Kimada/affair nje ya uhusiano (extramarital affair/cheating) - 2
Akaunti za siri (mipango isiyomshirikisha mwenza) - undisclosed accounts - 6
Mtoto wa nje/mtoto wa bwana mwingine - 1
Kupiga au kumuumiza mtu kwa kipigo (domestic violence) - 4
Ulevi/Matumizi ya madawa ya kuleva - 3
Kuingiliwa na wakwe (in-laws intrusion) - 5

 
Asante kwa ku share ilo dokezo maana nilkuwa naumiza kichwa na kujiuliza hawa wanaosamehe yote wametokea dunia hii hii au Jupiter. Kumbe ni suala la ideal na real (theory na practice)

Kuna mtu kadokeza kuwa wengi ambao wanasema "yote yanasameheka" ni kuwa hawajawahi kuingia kwenye hizi issue!
 
jaribu kuangalia mambo haya sita na uyapange kwa uzito wake wa kusameheka - yaani namba 1 likiwa ni zito kabisa kusameheka hadi 6 jepesi zaidi kusameheka. Yaani lile la kwa 1 kimsingi linaweza kabisa kuvunja uhusiano (definitely) na lile la 6 laweza kushtua au kutikisa kidogo (most probably) lakini linaweza likapita katika historia na watu wakadumu. Ukipenda unaweza ukaelezea kwanini namba zako zivyo hivyo vilivyo.



Kimada/affair nje ya uhusiano (extramarital affair/cheating)
akaunti za siri (mipango isiyomshirikisha mwenza) - undisclosed accounts
mtoto wa nje/mtoto wa bwana mwingine
kupiga au kumuumiza mtu kwa kipigo (domestic violence)
ulevi/matumizi ya madawa ya kuleva
kuingiliwa na wakwe (in-laws intrusion)

unaweza kupanga yote 6 au kupanga makubwa matatu (your top three). Siji kama wanaume na wanawake tunashindwa kusamehe vitu vile vile au la.

Mmm
mkuu mmm umesahau
...kunyimana unyumba hili nalo kusameheka ni ngumu zaidi ya hayo 6..na ndilo linachangia wengi kuyafwata hayo 6 ulioweka.wengi wamekuwa wakiteseka kawaida na kufikiria soln ni kunyimana unyumba la hasha utaletewa mwenza si mda mrefu na mgongo wa sita tunalala kama kawaida
pepo mchafu toka na isiwe hii kwako unaesoma ;wish you ndoa njema yenye misukosuko
 
Back
Top Bottom