dogojanja 87
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 882
- 213
mpenzi wa mama ni baba.mi ntakuanamuita baba huyo jamaa.
Naomba kuuliza kwa sababu wengine tuna uhusiano na wanawake wenye watoto wanaolingana umri na sisi au wanatuzidi kidogo au tunawazidi kidogo
kama Baba yako labda alifariki au ulilelewa na single parent au wazazi wako wameachana halafu ikatokea unaishi na mama yako au unamtembelea mara kwa mara na ikatokea kuna lijamaa mara nyingi linakuwa na mama yako beneti,yaani muda wote wamegandana japo huambiwi chochote kuhusu huyo jamaa lakini common sense itakuambia huyu jamaa ananitafunia mama yangu
utafanya nini utamchukia jamaa utampiga mkwara kama mama hayupo au utamweshimu au utamezea na kujifanya hakuna kitu kinaendelea?
kama una ndugu zako wengine wa kuzaliwa na nyie wote ni mature utaongea nao either kuwapigia au kwa kutania na kuuliza huyu jamaa anayekuwa na mama ni nani?
je utaendelea kumweshimu mama yako?halafu ikitokea siku ukaamka usiku ukasikia miguno kutoka chumbani mwa mama utafanya nini???da!
Naomba kuuliza kwa sababu wengine tuna uhusiano na wanawake wenye watoto wanaolingana umri na sisi au wanatuzidi kidogo au tunawazidi kidogo
kama Baba yako labda alifariki au ulilelewa na single parent au wazazi wako wameachana halafu ikatokea unaishi na mama yako au unamtembelea mara kwa mara na ikatokea kuna lijamaa mara nyingi linakuwa na mama yako beneti,yaani muda wote wamegandana japo huambiwi chochote kuhusu huyo jamaa lakini common sense itakuambia huyu jamaa ananitafunia mama yangu
utafanya nini utamchukia jamaa utampiga mkwara kama mama hayupo au utamweshimu au utamezea na kujifanya hakuna kitu kinaendelea?
kama una ndugu zako wengine wa kuzaliwa na nyie wote ni mature utaongea nao either kuwapigia au kwa kutania na kuuliza huyu jamaa anayekuwa na mama ni nani?
je utaendelea kumweshimu mama yako?halafu ikitokea siku ukaamka usiku ukasikia miguno kutoka chumbani mwa mama utafanya nini???da!
mimi mm yangu alitengana na bb yangu wkt mimi nikiwa mdogo sn less than 5 years. baba akaoa ila mama hakuolewa aliishi mwenyewe sisi tulibaki kwa baba..mama yangu alikuwa ni mfanyakazi kwa ivo wk end tulikuwa tunaenda kumtembelea. aliishi maisha ya upweke sn, sijamuona akiwa na mwanaume wala nini..
kwa jinsi alivyokuwa mpweke nilitamani mama yangu aolewe tena, walau awe na mtu wa kumsapoti na kuongea n.k
nilitamani kumuuliza kwa nini haolewi au kuwa na mtu lkn sikuweza.. nilivyokuwa nampenda mama yangu sikupenda awe mpweke kwani niliona km kuna kitu anakosa hivi(hasa kampani)..lkn mama yangu hakuolewa wala sijamuona na mtu mpaka alipofariki dunia miaka mingi baadae..leo hii baada ya kuwa mtu mzima na kuwa na familia ndio ninaona busara na hekima aliyokuwa nayo mama yangu na jinsi alivyotunza heshima yake na yetu..kwani hakuna mtu anayeweza kusema mama yenu alikuwa hivi na hivi..