Mama Salma Kikwete atesa na ndege ya Rais,JK aikwepa...

Chifu Ihunyo,
maana yangu ni kwamba mumetumbukia katika mtego wa wana-mtandao. mtego wa kulaumu wengine kwa uzembe na ubadhirifu wa Jakaya Kikwete.

Ninavyoelewa mimi, Mama Kikwete hawezi kutumia hiyo ndege bila ruhusa ya JK. Gharama za first lady ziko chini ya mfuko wa ikulu, ambao mdhibiti wake ni JK.

Kuna maana kubwa sana kuwa kiongozi wa kuchaguliwa. Maana yake ni kwamba unawajibika moja kwa moja kwa wananchi na kulinda maslahi yao.

Mara nyingi nimeona watu wakiwahifadhi mawaziri na kutaka watendaji wa chini yao mf.,makatibu wakuu wawajibike badala yao. Ubadhirifu umefanywa na ofisi ya Raisi na anayepaswa kubeba lawama ni Raisi.

Mwisho, nilipinga vikali ziara hiyo kwamba maudhui yake yanaathari kubwa kwa maendeleo ya mtoto wa kike. Kwa ujumla kilichoendelea pale ni mila potofu.

Wako wale walionipinga na kudai ngoma zile ni moja ya jadi zetu hapa tanzania na tunapaswa kuzitukuza. Ukichunguza Tanzania maeneo yanayoendekeza sana unyago na watoto wa kike kuchezwa ngoma yamebobea katika utoro watoto wa kike shuleni.

Raisi Mkapa aliumbuka alipopewa takwimu za watoto walioachishwa masomo na kufungishwa ndoa Mtwara ambao ni mkoa kinara wa ngoma za unyango.
 
Mzee Es,
Naona kama umemtaja Bi Asha... tufafanunulie mkuu, manake sisi wengine tulishapitwa na hilo.
 
Mafuchila,

Umekuwa mgeni mnooooooo, karibu. Bi Asha ni mke mdogo. Si unakumbuka hata AHM alivyopata urais aliongeza mke?

FD
 
Wandugu
Mwaka jana kama sikosei mkewe GB alikuwa Tanzania .Je alikuja na Airpforce? Hivi ni kweli kwamba mke wa Rais hawezi kupata ndege za kawaida hata kwenye business aka save pesa kidogo za walala hoi ? Hii ndege imenunuliwa na wote JK na Mkapa maana wote walikuwa ni serikali moja na sioni ubaya hata tukisema ndege kanunuliwa yeye JK .Safari 2 ni nyingi kwa mke wa Rais kupelekwa na kufuatwa .Wangapia wana sida huku Tanzania wanakosa hata udhamini wa serikali kisa haina pesa ?
Juzi Chuo Kikuu wamerushwa na FFU wakidai pesa na wana njaa Salma yeye na dege la gharama angani bado nidhani ni kawaida kisa First woman ?

Jamani, sioni kwa nini mke wa rais kupanda ndege ya rais iwe ni issue. Kama ndege hiyo ni kwa ajili ya kumpa rais convenience basi inafaa tuelewe tu kuwa convenience ya mke ni convenience ya mume isipokuwa kwa mtu asiyejali maisha ya utulivu na familia yake. Nakubali nchi inamatatizo lakini tukianza kuhusisha kila matumizi ya kiongozi na mamia ya matatizo ambayo yanaweza kutatuliwa kwa vyanzo vingine vya mapato itakuwa si haki na ni kurudisha nyuma maendeleo.
 
first lady inaweza kuitwa kuwa ni just a term lakini term hii ina kazi fulani.

kabla sijaanza na kusema kuhusu first lady, wizara ya mambo ya nje imepitisha mwaka jana kuwa wake/waume wa wanadiplomasia wa tanzania walioko nje ya nchi walipwe robo ya mishahara ya waume/wake zao kwa sababu na wao wakiwa kwenye posts za spouse zao, hulitangaza taifa kwa shughuli mbali mbali. (hii tayari nchi nyengine za ulaya na za africa inatekelezwa, tanzania wamepitisha ila mishahara haijatolewa bado)

ikiwa hawa spouses wa wanadiplomasia wanalipwa mishahara, sioni sababu ya kuwa first lady asilipwe fungu lake, kwa sababu na yeye anafanya kazi kubwa ya kulitangaza taifa.

kwenda swaziland kama first lady na kusema ni safari binafsi, kwa maoni yangu ni kumuonea....japokuwa tunachoweza kusema ni kuwa labda haikuwa na haja ya kwenda safari hiyo, au angeenda ila kwa ndege ya kawaida ingekuwa bora kwa taifa.

first lady wetu anaweza kuwa mfujaji wa pesa za jamii, lakini kwa hili hajafanya safari binafsi.
 
Huyu mama ni mswahili sana anapenda makuu, sikuwahi kuona mke wa rais yeyeote aliyetangulia akisidukizwa na msafara mrefu wa mapikipiki na magari chungu mzima, anaongeza kera ya msongamano wa magari dar kwani hatulii ndani, mala ngomani, bagamoyo nk.
 
Mama anakwenda kufungua mechi kwa kupiga penalt, nini tatizo jamani? Alipanda kandege kuona kana taste gani?

Muacheni mama wa Kwanza ale dunia. Jamani hizo habari za Bi Asha ni kweli?
 
atulie ndani kwani yeye mwali? halafu akitulia si utasema festi lady gani anakaa tu kama gogo na kuishia kunenepa, kweli kwa mwanadamu hakuna jema heri kumfadhili mbuzi!
 
Mama anakwenda kufungua mechi kwa kupiga penalt, nini tatizo jamani? Alipanda kandege kuona kana taste gani?

Muacheni mama wa Kwanza ale dunia. Jamani hizo habari za Bi Asha ni kweli?

hata kama habari za asha ni kweli, anayetakiwa kuumia ni salma mwenyewe, kama salma karidhika wengine pilipili iko shamba twawashwa je ikiingia ndani ya nyumba
 
............first lady wetu kero barabarani...anafuja pesa hilo ndio tatizo kubwa...msafara wake una piki piki moja ,pasat moja,landcruizer kama nne yake na za usalama..THATS TOO MUCH!!!..KWA NCHI MASIKINI HII...wake wote wa marais waliotangulia walikuwa wakitembelea gari moja tu mercedes au landcruizer....na wala hakuna kusimamisha magari..ikiwa wanaenda kwenye shughuli za kijamii zilizo rasmi..basi walipewa piki piki moja tu la kuwaongoza ili wawahi....

...siku hizi inaboa sana mnaweza kukaa kwenye foleni nusu saa ...mnasubiri labda ni rais au kiongozi stahili anapita....lakini mara unaona huyoo salma anapita kwa mikogo...hii hufanya watu walio kwenye foleni wanaaza kufyonya na kutukana....kupotezewa muda na mtu ambaye kikatiba si kiongozi ....hicho tu ndicho kinawaudhi watu hawakupata kukiona nyuma!!......kuhusu kufuja pesa kwenye ziara ..hilo..lingine...naamini ingebidi awe anaongozana na mume wake na kufanya shughuli zake sambamba na ziara za mumewe kama ilivyo kwa first ladies wengine ,....hii huokoa gharama na kumpa muda wa kumtunza mumewe ambalo hilo ndilo jukumu la kwanza la first lady kwa TAIFA
 
first lady alipokwenda swatziland aliongozwa na pride ya kike ya kutaka kujifagharisha mbele za wanwake wenziwe atakaowaona huko, kuwa yeye pia yumo katika watu wakubwa.
salma kikwete, tunaomba safari za kupanda ndege ya rais peke yako iwe hiyo tu, safari ya kwenda kutizama mila za swatziland kwa gharama tele kwa taifa ziwe mwisho.
wewe kama mke wa kwanza ndio unatakiwa kuongoza kutuonyesha utunzaji wa fedha za nchi, na sio vyenginevyo.
 
Unajua nivizuri watu kulalamika but at the same time hii ndege sio ya Rais ni ya Serikali... Mke wa Rais anakila haki yakuitumia as long as it is within reason .. Kama anaenda kwenye shuhuli Swaziland akiwa kama First Lady then anaruhusiwa but kama anaenda as Salma Kikwete shopping USA hatakiwi kutitumia.... Hii trip ya Swaziland sio tatizo. It is within her mandate maana yeye ni First Lady msitake awe exactly kama sisi...
 
Hii habari ni ya mwaka jana???au hata huko Nzega kaenda na hiyo eropleni ya Rais?
 
Kwa kweli msafara wa huyo mama unakera.Hivi ni lazma asindikizwe hivyo??Mbona wengine hawakufanya hivyo.Anaogopa nini mpaka asindikizwe kiasi hicho????????????
 
Hii ni kulazimisha scandal, hakuna tatizo lolote kwa first lady kusafiri kwa hiyo ndege kwa sababu hata asingeenda na hiyo ndege bado gharama za ndege ya kukodisha zingekuwa kubwa pia.

Hii ni kumuweka Mama Kikwete chini ya microscope kwa standard za kimarekani.Hatuna dege kubwa kama airforce one, sisi tuna kadege kadogo ambacho gharama yake haitofautiani sana na za kukodisha.

Halafu ikumbukwe kuwa nduge hii tumeshainunua hivyo kama mna advocate isitumiwe then ni bora muanze kushauri iuzwe!
 
changeni lakini habari hii ni ya mwaka 2006. hebu angalieni hiyo thread ilianzishwa lini ili muwe upto date
 
Gharama ya ndege ikiwa angani ni DOLA $6,000, au SHILLINGI MILLIONI SITA kwa saa, kama nilivyoambiwa na wataalamu wanaohusika nayo,

Watawala wa Tanzania kwa matanuzi tu na mashauzi yanayoumiza uchumi wa ndo wenyewe

Ni halali kwa mke wa Rais kutumia ndege ya Rais, katibu mkuu wa chama tawala kujicheki afya India baada ya muda mrefu bila kucheki, n.k.

Lakini kuna wanawake wengi Tanzania wanafia njiani wakienda kujifungua, na kuna hospitali nyingi za wilaya hazina XRAY...

Halafu hata hapa JF bado watu wanawatetea kuwa ni halali..ina maana wao maisha ni peponi ndani ya nchi ambapo wananchi hawali hata mlo 1? Ndo hizi hizi kauli za kupumbavu za Basil Mramba kuwa hata watanzania tukila manyasi ndege itanunuliwa? Unapanda ndege ya Rais kwenda ulaya huku ukiwa Matonya wa kuombeleza msaada wa miundombinu na fedha za bajeti??
UPUUZI ULIOJE?
 
Hata kapuya alishaenda na dege la jeshi unyanyembe katika ziara binafsi akiwa waziri wa ulinzi..
NInachotaka watawala waone, kwanini wao waishi peponi ilhali siye tunasota..
Na wanaishi peponi kwa kodi zetu hizi hizi! Nachukia sana hii tabia!
 
Back
Top Bottom