Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,347
- 6,471
Kutoa maagizo kwa mkuu wa mkoa wa Mara, Mafuru, awaambie wana usalama wampeleke yule mjane ikulu ndogo ili amweleze shida zake ni sahihi kweli? Kwa nini asitoe maagizo kwa mwenyekiti wa UWT? Hivi nae akiwa peke yake anafikia Ikulu ndogo?
"Rushwa ilipingwa na nchi yetu zama za TANU hata vyama vya upinzani havikuwepo, ambapo katika ahadi za wana TANU zilisema kuwa rushwa ni adui wa haki sitatoa wala kupokea rushwa sasa kama kwa wapinzani kama hawana sera wanyamaze kuliko kusema kitu wasichokijua" alisema Mama Salma (Mtanzania, 15/09/2010, uk. 3).
Moja, huyu mama hajui historia ya nchi yetu, kwani wakati wa miaka ya mwanzo baada ya uhuru kulikuwa na vyama vya upinzani. Pili, vita vya rushwa si vya maneno ni vya vitendo; je, Andy Chenge na Idrissa kuhusu rushwa ya rada CCM na chombo chake TAKUKURU wamewafanya nini mpaka sasa? Tatu, hivi Dr. Slaa na Prof. Lipumba hawaijui hii nchi kama anavyoijua huyu mama? Nne, naomba huyu mama alete data zenye inference kutoa ushahidi dhidi ya vita ya rushwa na ushindi wa serikali kwenye vita hivyo. tano, atuambie kwa nini ripoti ya Warioba sehemu ya pili imefichwa kabisa na serikali? Sita, hivi kati ya mumewe na Dr. Slaa nani ameiga kutumia helikopta kwenye kampeni? Saba, hivi WAMA ni sister organisation ya UWT?
"Rushwa ilipingwa na nchi yetu zama za TANU hata vyama vya upinzani havikuwepo, ambapo katika ahadi za wana TANU zilisema kuwa rushwa ni adui wa haki sitatoa wala kupokea rushwa sasa kama kwa wapinzani kama hawana sera wanyamaze kuliko kusema kitu wasichokijua" alisema Mama Salma (Mtanzania, 15/09/2010, uk. 3).
Moja, huyu mama hajui historia ya nchi yetu, kwani wakati wa miaka ya mwanzo baada ya uhuru kulikuwa na vyama vya upinzani. Pili, vita vya rushwa si vya maneno ni vya vitendo; je, Andy Chenge na Idrissa kuhusu rushwa ya rada CCM na chombo chake TAKUKURU wamewafanya nini mpaka sasa? Tatu, hivi Dr. Slaa na Prof. Lipumba hawaijui hii nchi kama anavyoijua huyu mama? Nne, naomba huyu mama alete data zenye inference kutoa ushahidi dhidi ya vita ya rushwa na ushindi wa serikali kwenye vita hivyo. tano, atuambie kwa nini ripoti ya Warioba sehemu ya pili imefichwa kabisa na serikali? Sita, hivi kati ya mumewe na Dr. Slaa nani ameiga kutumia helikopta kwenye kampeni? Saba, hivi WAMA ni sister organisation ya UWT?