Meya Kimbisa na Sofia Simba sasa wameamua kuokoka na wanasali kanisa la Mama Rwakatare, hivi hii ni serious issue au kuna issue nyuma ya pazia?
Jicho leo hii limeshuhudia Mh Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Utawala Bora Mh Sophia Simba katika ibada ya maombezi pale Mikocheni B Ass of God kwa Mch Rwakatare,
Mh Simba alipata maombi ya nguvu toka kwa waumini wote yakiongozwa na Mch Dk Rwakatare na mara baada ya kuombewa alijumjuika na wakristo ama walokole katika ibada ya kusifu na kuabudu ambapo alikuwa akifuatisha vyema nyimbo zote pamoja na kunesanesa ama kucheza kama wafanyavyo waumuni wengine wa makanisa haya ya pentekoste.
Hapana shaka hii haitakuwa mwisho kwa Mh Simba kuudhuria ibada mahali pale kwani ameoneshwa kukunwa sana na maombezi yale, ingawa sina hakika kama atakubali kumpokea Bwana na kuwa Mwokozi wa maisha yake.
Ubarikiwe sana Mh Simba.
Unajua, Ndugu yangu, RMashauri Huyu mama Rwakatare na Sophia Simba wanawaangusha sana wanawake Tanzania na dunia nzima. Si Rwakatare wala Sophia Simba anaweza kujigamba kuwa ni mfano bora wa mwanamke wa Afrika. Tunahitaji sura nyingine kabisa za wanawake ambazo ndizo zitakuwa mfano wa bara letu, ambalo wanawake bado wako nyuma.
Rwakatare na Sophia Simba wanaitumia nafasi hiyo vibaya sana, wakielewa wazi kuwa kuna pengo kubwa hasa katika nyanja hizo, Dini na Siasa.
Tukirudi kwa Rwakatare, huyu si mtumishi wa Yesu wala Mungu, kwa hili ninahakika kabisa. Huyu mama anatafuta pesa, na amezipata kwa kutumia jina la Yesu. Na amini usiamini, lakini wateja wake anaowaota usiku ni hawa wenye pesa kama Sophia Simba na si wale wenzangu walala hoi wanaokwenda kwake bila pesa. Hao huwatumia kujaza kanisa na kujitangaza tu. Sikiliza maneno yake yalivyojaa vishawishi vya kiuchumi.
Sophia Simba ni Msema ovyo, aliyebahatika kupata vyeo zaidi ya uwezo wake kwa kubahatisha kutumia ukichaa wake kugusa hisia za watu waliochoshwa na mafisadi wanaume. Swali linalotawala hapa ni MARA NGAPI ATAWEZA KUBAHATISHA KUCHAGUA NAMBA 6 KATIKA NDOO ILIYOJA VIKARATASI VYENYE NAMBA 35 MILIONI.
Jibu la swali hilo ni ngumu, na wengi wanadhani ni MLEMBE au Rwakatare. Well, time will tell!
Malila, as quoted above, issue ya Mama Sofia haikuwa ngeni, lakini jana nilimwona hata Kimbisa kanisani akitoa ushuhuda. Sina tatizo na kuwa muumini wa kanisa hilo na wengine wengi (wanasiasa) niliowaona ambao walikuwa wakitoa shuhuda zao na kupewa fursa za kunena mbele za madhabahu, wasiwasi wangu ni kama wamedhamiria kweli toka kwenye mioyo yao, kama ni kutoka moyoni basi watenda vema, kama wanacheza deal wajue wanacheza mchezo wa hatari ambao kinyume chake wanaweza kukabiliana na balaa kubwa hapo mbeleni na sishauri wala sitamani kuona wengine wakifanya usanii kupitia njia ya imani/dini.Tupe chanzo cha habari yako hii?
Meya Kimbisa.....eamua kuokoka na wanasali kanisa la Mama Rwakatare, hivi hii ni serious issue au kuna issue nyuma ya pazia?
Malila, as quoted above, issue ya Mama Sofia haikuwa ngeni, lakini jana nilimwona hata Kimbisa kanisani akitoa ushuhuda. Sina tatizo na kuwa muumini wa kanisa hilo na wengine wengi (wanasiasa) niliowaona ambao walikuwa wakitoa shuhuda zao na kupewa fursa za kunena mbele za madhabahu, wasiwasi wangu ni kama wamedhamiria kweli toka kwenye mioyo yao, kama ni kutoka moyoni basi watenda vema, kama wanacheza deal wajue wanacheza mchezo wa hatari ambao kinyume chake wanaweza kukabiliana na balaa kubwa hapo mbeleni na sishauri wala sitamani kuona wengine wakifanya usanii kupitia njia ya imani/dini.
Mkuu Ibra, kama nimekosea basi samahani mkuu wangu. Naomba kama topic inakugusa kwa namna moja ama nyingine au imekukera wafahamishe mods wafute kabisa. Nimeianzisha kwa wema kabisa mkuu wangu
Hivi mnamkumbuka yule kijana aliyekamatwa na kichwa cha mtu pale Muhimbili?hivi unawajua vizuri wanasiasa wewe? makamba hujawahi kumuona makanisani?
kwa taarifa yako, inawezekana hakuna aliyeokoka hapo, hata rwakatare mwenyewe. we subiri tu utaona
Wanasiasa ni viumbe wa ajabu sana, wanaweza kufanya vituko ilimradi vinawapatia kura!! Juzi juzi nimensikia Lyatonga Mrema akiwa anahojiwa pale TBC wakiwa na Lipumba ananukuu aya za Q'oran tukufu kwa kiarabu; Lipumba alishindwa kujizuia ikabidi acheke !!
Thi is the extent politicians can go in search of votes.