Enny
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 962
- 130
Kuna rafiki yangu kaja jana kunilalamika kuhusu mama yake mdogo kuwa ana roho mbaya sana hataki watoto wa dada yake wapate bali watoto wake tu. Jamaa kaniambia alikuwa anafanya kazi kongo kwenye kampuni moja ya madini kama expat sasa waliingiliwa na majambazi mara mbili kwa kipindi cha interval ya miezi mitatu. Sasa jamaa akaamua kutafuta kazi tz na akapata, hivyo akaamua kuacha kule na kurudi tz. Basi aliporudi akafunga safari kwenda mkoani alipo mama mdogo wake kuwasalimia, na katika story za maisha akawasimulia jinsi walivyopona kuumizwa na majambazi, alipewa pole sana kwa yaliyowakuta huko. Lakini baada mwaka mmoja akaja kusikia kuwa mama yake mdogo huyo anatangaza kuwa huyo jamaa alipanga na majambazi waje waibe pale kazini kwao na wakagawana hela ndio maana amefanya mambo mengi ya maendeleo. Wakati jamaa alikuwa analipwa vizuri kule kwa kipindi cha miaka miwili yote aliyokaa huko ameweza kufanya mambo mengi nyumbani. Sasa alitaka ampigie simu huyo mama ili kumtukana. Mimi nikamshauri asifanye hivyo aachane nae. Akaniambia mara nyingi amekuwa akiongea negative kuhusu yeye na wadogo zake. Je ni ushauri gani una mfaa huyu rafiki yangu maana naona amechukia sana.