BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Mama Maria: Kuilipa Dowans tatizo kubwa
* Ataka CCM, wanachama watafakari kabla ya kulipa
Na Daud Magesa, Butiama
Majira
MJANE wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere ameibuka na kusema kulipa mabilioni ya fedha kwa kampuni ya
Dowans ni sawa na kuwaingiza wananchi kwenye matatizo makubwa.
Mama Nyerere amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wanachama wake wakae watafakari kwanza kabla ya kulipa fedha hizo, zinazokadiriwa kufikia sh. bilioni 94, kwa kuwa suala hilo litafanya CCM ama isiaminike, au wananchi waichukie.
Aliitaka serikali kuwawajibisha wote wanaohusika na Dowans ili kurejesha maadili ya uongozi kama ilivyokuwa wakati wa mwalimu, badala ya kukurupuka kulipa sh. bilioni 94 bila kuangalia athari watakazopata wananchi.
Mama Maria Nyerere alitoa kauli hiyo nyumbani kwake Mwitongo, Butiama, juzi, wakati akizungumza na Kamanda wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa wa Mbeya, Bw. Mwakajumilo Isaac ambaye pia ni Mhasibu Mwandamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Tawi la Mbeya, waliomtembelea baada ya kuanguka hivi karibuni na kuumia wakati akielekea kanisani.
Alisema kwamba jahazi hili (Tanzania) linaelekea kuzama kutokana na vurugu na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, na hivyo kuwataka Watanzania watambue kuwa, 'sote tutaangamia kutokana na athari za machafuko hayo'.
Alisema kuwa baadhi ya viongozi na Watanzania wamepoteza maadili na hivyo kutoa kauli zinazoweza kuiingiza nchi kwenye machafuko kwa maslahi ysao binafsi, na kwa manufaa yao kisiasa.
Baadhi ya kauli hizo, alisema ni zinazohusiana na mifarakano ya kidini, na nyingine kuhusu na suala la dowans , ambayo alikuwa anaifuatulia kwenye televisheni.
Kuhusu mabadiliko ya katiba, Mama Nyerere alisema amekuwa akifuatilia mijadala mbalimbali kwenye runinga na kuona ulivyopamba moto, na hata kijijini kwake, Mwitongo, nako mjadala unaendelea.
Alisema kwamba Watanzania waendelee kuwa watulivu na mijadala hiyo iendeshwe kwa kushirikisha wadau na viongozi kutoka makundi yote kwa haki na usawa, huku wakizingatia umoja, amani na utulivu wa taifa ili kuenzi mazuri yaliyoachwa na waasisi wa taifa hili kwa manufaa ya wote.
Mjane huyo wa Baba wa Taifa alieleza kuwa viongozi mbalimbali, wananchi na wadau wote wawe watulivu huku wakiliombea taifa wakati mchakato wa katiba mpya ukisubiriwa
kuanza.
Akigeukia sera ya Kilimo Kwanza, aliwaeleza makada hao wa UV-CCM kwamba watu hawapendi tena kilimo, hasa vijana wenye nguvu ,wamekuwa wakikimbilia mijini kufanya biashara na kusababisha maeneo mengi ya vijijini kukabiliwa na tishio la njaa huku mabepari nao wakipigania kuondoa historia nzuri ya taifa.
Vijana wangu, hakuna mtu ambaye angependa kuwa maskini, lakini pia huwezi kuwa tajiri kwa njia za mkato, hasa kwa hawa watumishi wa umma, jambo kubwa ni viongozi kuzingatia na kufuata maadili kama ilivyokuwa kwenye uongozi wa serikali ya awamu ya kwanza ya hayati Mwl Julius Nyerere kwa kuthubutu kuwaondoa wasiofaa na kuwataja hadharani, alisema na kuongeza:
Serikali inapaswa iwaondoe wanaoiharibia, hata kama wanafahamiana. Pia ikihakikisha kauli za watu na wanasiasa zisizofaa kwa Watanzania, zenye lengo la kuhatarisha amani hazipewi nafasi na hatua kali zichukuliwe kwa wale wanaotoa kauli za uchochezi ili kuliangamiza jahazi la taifa letu lenye historia ya pekee na mfano kwa mataifa mengine.
Alitoa wito kwa viongozi wa serikali kuhakikisha misingi yote ya taifa iliyoasisiwa na viongozi waliotanguliwa wanaendelea kuilinda wakiweka mazingira mazuri kwa kuboresha huduma mbalimbali za kijamii hususani vijijini ambako utoaji wa huduma hauridhishi na hauna tija.
Alisema uduni wa huduma hizo husababisha jamii kulalamikika kutokana na wananchi wengi wa kipato cha chini kukosa huduma za afya, maji, elimu, barabara, bei nzuri ya mazao na upatikanaji rahisi wa nishati ya umeme.
Aliwaasa Watanzania kuacha kukubali kutumiwa na watu ambao malengo yao ni kujinufaisha kisiasa na kupata umaarufu ,huku wakiliacha taifa likiangamia kutokana na kutaka kuwagawa kwa kuzungumzia ukabila, udini na rangi vitu ambavyo wakati nchi ikipata uhuru Mwl. Nyerere na waasisi wengine walivipinga kwa nguvu zote, na hadi leo tu wamoja.
* Ataka CCM, wanachama watafakari kabla ya kulipa
Na Daud Magesa, Butiama
Majira
MJANE wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere ameibuka na kusema kulipa mabilioni ya fedha kwa kampuni ya
Dowans ni sawa na kuwaingiza wananchi kwenye matatizo makubwa.
Mama Nyerere amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wanachama wake wakae watafakari kwanza kabla ya kulipa fedha hizo, zinazokadiriwa kufikia sh. bilioni 94, kwa kuwa suala hilo litafanya CCM ama isiaminike, au wananchi waichukie.
Aliitaka serikali kuwawajibisha wote wanaohusika na Dowans ili kurejesha maadili ya uongozi kama ilivyokuwa wakati wa mwalimu, badala ya kukurupuka kulipa sh. bilioni 94 bila kuangalia athari watakazopata wananchi.
Mama Maria Nyerere alitoa kauli hiyo nyumbani kwake Mwitongo, Butiama, juzi, wakati akizungumza na Kamanda wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa wa Mbeya, Bw. Mwakajumilo Isaac ambaye pia ni Mhasibu Mwandamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Tawi la Mbeya, waliomtembelea baada ya kuanguka hivi karibuni na kuumia wakati akielekea kanisani.
Alisema kwamba jahazi hili (Tanzania) linaelekea kuzama kutokana na vurugu na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, na hivyo kuwataka Watanzania watambue kuwa, 'sote tutaangamia kutokana na athari za machafuko hayo'.
Alisema kuwa baadhi ya viongozi na Watanzania wamepoteza maadili na hivyo kutoa kauli zinazoweza kuiingiza nchi kwenye machafuko kwa maslahi ysao binafsi, na kwa manufaa yao kisiasa.
Baadhi ya kauli hizo, alisema ni zinazohusiana na mifarakano ya kidini, na nyingine kuhusu na suala la dowans , ambayo alikuwa anaifuatulia kwenye televisheni.
Kuhusu mabadiliko ya katiba, Mama Nyerere alisema amekuwa akifuatilia mijadala mbalimbali kwenye runinga na kuona ulivyopamba moto, na hata kijijini kwake, Mwitongo, nako mjadala unaendelea.
Alisema kwamba Watanzania waendelee kuwa watulivu na mijadala hiyo iendeshwe kwa kushirikisha wadau na viongozi kutoka makundi yote kwa haki na usawa, huku wakizingatia umoja, amani na utulivu wa taifa ili kuenzi mazuri yaliyoachwa na waasisi wa taifa hili kwa manufaa ya wote.
Mjane huyo wa Baba wa Taifa alieleza kuwa viongozi mbalimbali, wananchi na wadau wote wawe watulivu huku wakiliombea taifa wakati mchakato wa katiba mpya ukisubiriwa
kuanza.
Akigeukia sera ya Kilimo Kwanza, aliwaeleza makada hao wa UV-CCM kwamba watu hawapendi tena kilimo, hasa vijana wenye nguvu ,wamekuwa wakikimbilia mijini kufanya biashara na kusababisha maeneo mengi ya vijijini kukabiliwa na tishio la njaa huku mabepari nao wakipigania kuondoa historia nzuri ya taifa.
Vijana wangu, hakuna mtu ambaye angependa kuwa maskini, lakini pia huwezi kuwa tajiri kwa njia za mkato, hasa kwa hawa watumishi wa umma, jambo kubwa ni viongozi kuzingatia na kufuata maadili kama ilivyokuwa kwenye uongozi wa serikali ya awamu ya kwanza ya hayati Mwl Julius Nyerere kwa kuthubutu kuwaondoa wasiofaa na kuwataja hadharani, alisema na kuongeza:
Serikali inapaswa iwaondoe wanaoiharibia, hata kama wanafahamiana. Pia ikihakikisha kauli za watu na wanasiasa zisizofaa kwa Watanzania, zenye lengo la kuhatarisha amani hazipewi nafasi na hatua kali zichukuliwe kwa wale wanaotoa kauli za uchochezi ili kuliangamiza jahazi la taifa letu lenye historia ya pekee na mfano kwa mataifa mengine.
Alitoa wito kwa viongozi wa serikali kuhakikisha misingi yote ya taifa iliyoasisiwa na viongozi waliotanguliwa wanaendelea kuilinda wakiweka mazingira mazuri kwa kuboresha huduma mbalimbali za kijamii hususani vijijini ambako utoaji wa huduma hauridhishi na hauna tija.
Alisema uduni wa huduma hizo husababisha jamii kulalamikika kutokana na wananchi wengi wa kipato cha chini kukosa huduma za afya, maji, elimu, barabara, bei nzuri ya mazao na upatikanaji rahisi wa nishati ya umeme.
Aliwaasa Watanzania kuacha kukubali kutumiwa na watu ambao malengo yao ni kujinufaisha kisiasa na kupata umaarufu ,huku wakiliacha taifa likiangamia kutokana na kutaka kuwagawa kwa kuzungumzia ukabila, udini na rangi vitu ambavyo wakati nchi ikipata uhuru Mwl. Nyerere na waasisi wengine walivipinga kwa nguvu zote, na hadi leo tu wamoja.