Mama, "Kwani si tunaalika watu kuhalalisha hilo hilo (tendo la Ndowa)"

Kiranga nimekuelewa,kuhusu neno "kuoa" au "kuolewa" wewe unalitafsiri vipi?Kuhusu mwanamke kutokuacha nafikiri hiyo inatokana na imani fulani,sidhani kama tunaweza lizungumzia hapa.Hayo maneno ya kiswahili bado sijaona ubaya wake,tatizo tunayachukulia kutokana na dhana ya mwanamke kutokutoa talaka ambayo kama nilivyosema ni dhana ya imani fulani tena moja tu.Kwenye mfumo dume hapo napo kuna mkanganyiko.Mwanaume na mambo ya kiume.Mwanamke na mambo ya kike.Tukubali kuwa mwanamke anapoambiwa "acha kufanya mambo ya kiume" ni sifa?Sidhani,pia mwanaume anapoambiwa acha mambo ya kike,sio aibu.Unapoyataja mambo ya kikekike wewe ndie unaamua yawe tusi,kashfa au vinginevyo.Tafsiri iliyoko kichwani mwako.Lakini pia huu mfumo unaoitwa dume una mambo mengi lakini mengi zaidi yapo vichwani mwetu zaidi,sio halisi!
 
Kamchumbia wa nini? Mie nilidhani uchumba maanake yake, maandalizi ya kuja kukuoa,au?

Unaendeleza mfumodume.

Mie nakuuliza kwa nini unafikiri huyu dada, mwanamke, anataka kuolewa.

Wewe unaniuliza mwanamme kamchumbia kwa nini? Unampa prominence mwanamme, mtu ambaye hata sijamuulizia hapa. Mwanamke anaweza kuwa katika mahusiano na mwanamke, akitaka kumuoa huyo mwanamke, na mwanamke asiwe na haja ya kuolewa.

Zaidi ya hapo, neno "mchumba" hutumika loosely katika kiswahili kwa kumaanisha "boyfriend/girlfriend" na pia "fiancee" kwa sababu hatuna utamaduni wa boyfriend/girlfriend, ni mgeni. Sina hakika katika hii thread neno hili limetumika kama boyfriend au fiancee.

Kwa nini unamleta mwanamme katika swali lililomlenga mwanamke?
 
Imenibidi nisome upya thread,nadhani neno ndoa lina maana tofauti vichwani mwetu.Mfano baba anaamini ndoa ni mpaka waende kwenye nyumba ya ibada au mkuu wa wilaya au kwa kiongozi wa mila na hii ndo tafsiri ya wengi!
 
Imenibidi nisome upya thread,nadhani neno ndoa lina maana tofauti vichwani mwetu.Mfano baba anaamini ndoa ni mpaka waende kwenye nyumba ya ibada au mkuu wa wilaya au kwa kiongozi wa mila na hii ndo tafsiri ya wengi!

Wakati kiserikali kuna kitu kinaitwa "common law marriage" nayo ni ndoa tosha inayotambulika kisheria.
 
Wakati kiserikali kuna kitu kinaitwa "common law marriage" nayo ni ndoa tosha inayotambulika kisheria.

Mkanganyiko mkubwa!Hivi dhana ya ndoa ilianza lini na wapi?Siamini kama dini ndo chanzo!
 
Kiranga nimekuelewa,kuhusu neno "kuoa" au "kuolewa" wewe unalitafsiri vipi?Kuhusu mwanamke kutokuacha nafikiri hiyo inatokana na imani fulani,sidhani kama tunaweza lizungumzia hapa.Hayo maneno ya kiswahili bado sijaona ubaya wake,tatizo tunayachukulia kutokana na dhana ya mwanamke kutokutoa talaka ambayo kama nilivyosema ni dhana ya imani fulani tena moja tu.Kwenye mfumo dume hapo napo kuna mkanganyiko.Mwanaume na mambo ya kiume.Mwanamke na mambo ya kike.Tukubali kuwa mwanamke anapoambiwa "acha kufanya mambo ya kiume" ni sifa?Sidhani,pia mwanaume anapoambiwa acha mambo ya kike,sio aibu.Unapoyataja mambo ya kikekike wewe ndie unaamua yawe tusi,kashfa au vinginevyo.Tafsiri iliyoko kichwani mwako.Lakini pia huu mfumo unaoitwa dume una mambo mengi lakini mengi zaidi yapo vichwani mwetu zaidi,sio halisi!

habari nzima ya "kuoa" na "kuolewa" ni medieval, smacks of slavery, ownership and territory marking as if we are still hunter gatherers.

Mwanamke kutokuacha inatokana na imani fulani damn right, imani hiyo ni mfumodume, kwamba mwanamke anaachwa tu, hawezi kuacha kwa sababu anaolewa tu, hawezi kuoa. Ndiyo maana nikatoa mfano wa kiswahili, mwanamke hawezi kuoa, anaolewa tu. Hujaona ubaya wa lugha kutowapa usawa katika ndoa mwanamke na mwanamme, then mfumodume umeshameza thought process yako.

Hakuna mambo yasiyo na msingi wa kibaiolojia yaliyo ya kiume au ya kike.

Mwanamke anapoambiwa "acha kufanya mambo ya kiume" unakusudia mambo gani? Maana usitake kuniuliza swali lisilo specicif na linaloweza kubeba tani za vijimambo tofauti kiasi cha kunifunga kukubali nisichokijuua. be specific, nipe mfano, mambo gani ya kiume? Mie nishatoa mfano specific hapo juu. Ex-Speaker Msekwa aliposema "acheni wivu wa kike" hakuwatendea haki wanawake, aliongea kimfumodume kwa kutumia imani ya kwamba tabia ya wivu ni domain ya wanawake, wakati tunajua otherwise.

Issue si kwamba "mwanamme anapoambiwa aache kufanya mambo ya kike" ni aibu au si aibu, issue ni, mambo gani unaona ni ya kike? Mwanamme anayeomba msaada wa hisabati anafanya mambo ya kike kwa sababu wanawake ndio hawajui hisabati? Mwanamme mwenye wivu anafanya mambo ya kike kwa sababu wivu ni jambo la kike? Mwanamme anayependa kupika anafanya mambo ya kike kwa sababu kupika ni jambo la kike? Mwanamme anayependa kucheza na watoto anafanya mambo ya kike kwa sababu kucheza na watoto ni jambo la kike?

Mie sijayataja mambo ya kike, nimekutolea mfano wa Msekwa aliyesema "acheni wivu wa kike" akimaanisha kwamba wivu ni tabia ya kike na wananume wenzie waliomkashifu hawatakiwi kuwa na wivu.

Kuhusu mfumodume kuwa na mambo mengi vichwani mwetu, lakini yasiwe halisi, umeshindwa kujenga hoja kwa mifano, umetoa a blanket statement tu. Jaribu kunithibitishia kwa mifano kwa nini unaamini hivyo.

Mie nimekuonyesha jinsi gani mfumodume ulivyo katikati ya jamii yetu. upo katika taasisi inayoheshimika sana katika jamii. Ndoa.mpaka l;ugha ya ndoa ina mfumodume.Lugha ina tabia ya kuonyesha jinsi jamii nzima inavyofikiri.

Ukiona lugha inafanya mwanamke kuwa passive katika ndoa, na mwanamme kuwa active, ujue mfumodume upo katika ndoa. Mwanamke anatakiwa kusema hewala bwana hata akizabwa kibao.

Tutaweza kuwalaumu dada zetu wasipotaka kuolewa?
 
Kiranga, Ex spika aliposema "acha wivu wa kike" alimaanisha kuna wivu wa kike na wivu wa kiume,hakuwa na maana wivu ni jambo la kike.But sisemi alikuwa sahihi kusema hivyo ila nimerekebisha kauli yako kuhusu ex spika.Niliposema mfumo dume una mambo mengi yaliyo vichwani mwetu ninamaana kuwa kwanza dhana yenyewe haijaanzia kwetu,imeletwa,lakini haina maana ni mbaya kwa msingi huo.Cha msingi inazungumzia mambo ya msingi ama la.Mambo yaliyo vichwani ni kama tafsiri ya kuoa na kuolewa,hiyo tafsiri ya kumilikiwa imetokana na tafsiri ya kidini ambayo haiko sahihi.Naamini kuoa sio mbaya ubaya ni tafsiri tuliyowekewa vichwani.Mfano nikikuambia hakuna sehem za siri kwenye mwili wako unaweza ukanishangaa.Ni kawaida si umeambiwa zipo?Lakini hii haina maana dhana ya mfumo dume haina maana.Kuna mambo kama mwanamke kutokua kiongozi ni mambo ya ukweli ya kimfumo dume.Ila sijasikia hawa wanaodai haki za wanawake wakipinga viti maalum kwaajili ya wanawake pamoja na kupewa max za chini kwenye ufaulu.Mwanamke apewe viti maalum bungeni kwa sababu gani?Huku ni kumwaminisha kuwa yeye ni dhaifu.Unampa upendeleo wa ufaulu kwa nini?Hii sio HAKI!
 
Una introduce kitu kigeni kabisa ambacho mie sijakiongelea halafu unakiunganisha tu kama vile nimesema kwamba wanawake wanapenda kuchupachupa.

Mie sijasema kwamba wanawake wanapenda kuchupachupa, nimesema mfumodume unasifia wanaume kuchupachupa (urijali, kiwembe etc) lakini hapo hapo unadharau umalaya huo huo kwa mwanamke (mama huruma, jamvi la wageni etc)

Mtu akiisema hii double standard ya mfumodume hamaanishi kwamba wanawake wanao"chupachupa" wanapenda kufanya hivyo.

Hii kilatini inaitwa "Non sequitur", it does not follow, umeunganisha vitu viwili ambavyo havina uhusiano, out of nowhere.

Kuna kitu formal kinachoitwa mfumo dume? Nafikiri umeitwa hivyo kwa kuwa wanaume wanajipendelea. Swala langu lipo palepale jee huko kuitwa malaya kunaitwa na wanaume tu au hata wanawake wenyewe wasiopenda hali hiyo? Jee ulishawahi kuwasikia wanawake wakilalamika wenzao wakiitwa hivyo kwa tabia yao? Huwezi kubebesha uzuri katika jambo baya na hivyo jambo baya litabaki kuwa jambo baya kwa jamii. Umalaya ni umalaya awe mwanamme au mwanamke as far as jamii inavyoona.
 
ukisema "stable relations out of marriage lazima itakuwa na flaws chungu mzima, tayari umeshaji contradict.

Halafu "stable marriage nje ya ndowa" ni kitu gani?

Bottom line, kuna mapenzi yanayostawi nje na ndani ya ndoa, ndoa si kitu kibaya wala kizuri. Kama unaweza kustawisha mapenzi bila ndoa, ndoa si lazima.

Kuna watu wamekaa bila ndoa miaka kibao, wameishi vizuri tu. Kwa pressure wakaamua kuoana, baada ya kuoana wamedumu miaka miwili tu.Talaka.

ndoa ni kama kukaa ndani ya nyumba mliyofungiwa. Hamuwezi kutoka mpaka mvunje milango (talaka) jambo ambalo litaleta kelele na bughudha (aibu kwa jamii, bado tuna stigmatize talaka). Kwa hiyo hata hao wanaodumu katika ndoa hatujui kama wanadumu kwa mapenzi ya kweli au kwa sababu wanakwepa aibu tu ya kuachana.

Watu wanaoamua kukaa wenyewe kwa kuelewana bila ndoa wanaweza kusema wanapendana kikweli bila kushurutishwa na ndoa. Ni kama watu walioamua kukaa pamoja ndani ya nyumba huku milango ikiwa wazi. kila mmoja ana uwezo wa kuondoka bila kuvunja mlango, lakini haamui kufanya hivyo kwa sababu anapenda kuwa pamoja na mwenzake.

Naona hujauliza hizo flaws ni zipi au tayari umeshazijuwa na hivyo unajaribu kuzikimbia? Tusiwe wakubwa wa nadharia kusahau real applications. Hebu niambie hao watu waliostaarabika wote duniani wanafikia wapi mwisho wa relations zao, si celebrities, si royals , si viongozi ambao walio huru kuwa na uhusiano huo unaoueleza wewe.
 
Mi nadhani,kwa mtazamo wangu,hatujui ndoa ni nini,tafsiri mbovu za kidini ndo zinaleta shida hapa.Kukifuata kitu kimkumbo ni tatizo kubwa.Niliwahi kuanzisha mada siku moja hapa nikitaka kila mmoja aeleze ndoa ni nini,majibu yaliyotoka yanachekesha.Watu wanafungwa na dhana zaidi kuliko kitu halisi.Umapokuwa kwenye mahusiano nje ya ndoa mnaishi muda mrefu kwa sababu mnajiongoza wenyewe,kwenye ndoa tatizo mnataka muongozwe na dhana zaidi ya nyie wenyewe.Ndo maana mtu anakua mwaminifu nje ya ndoa,akiingia kwenye ndoa mambo yanabadilika![/QUOTE
Inawezekana kila mtu anataka namna yake ya ndowa lakini kwa ukweli hakuna asiejuwa maana ya ndowa. Ndowa uskitaka utaihusanisha na dini na isipotaka basi dini haihusiki. Kwa ufupi ni kuwa ndowa ni mfumo wa uhusiano unaokubalika na jamii. Sasa tafuta njia utakayoifanya isikubaliwe na jamii iwe ndowa.
Fikira kuwa ndowa ni kitu mteremko ni fikira potofu kwani hata huo uhusiano utakaofanya nje ya ndowa utakuwa na misukosuko yake na laiti kama hauuwezi kuwa na misukosuko kuna kitu gani cha zaidi iwapo mtafunga ndowa kitakacholetw tatizo?
 
Kiranga, Ex spika aliposema "acha wivu wa kike" alimaanisha kuna wivu wa kike na wivu wa kiume,hakuwa na maana wivu ni jambo la kike.But sisemi alikuwa sahihi kusema hivyo ila nimerekebisha kauli yako kuhusu ex spika.Niliposema mfumo dume una mambo mengi yaliyo vichwani mwetu ninamaana kuwa kwanza dhana yenyewe haijaanzia kwetu,imeletwa,lakini haina maana ni mbaya kwa msingi huo.Cha msingi inazungumzia mambo ya msingi ama la.Mambo yaliyo vichwani ni kama tafsiri ya kuoa na kuolewa,hiyo tafsiri ya kumilikiwa imetokana na tafsiri ya kidini ambayo haiko sahihi.Naamini kuoa sio mbaya ubaya ni tafsiri tuliyowekewa vichwani.Mfano nikikuambia hakuna sehem za siri kwenye mwili wako unaweza ukanishangaa.Ni kawaida si umeambiwa zipo?Lakini hii haina maana dhana ya mfumo dume haina maana.Kuna mambo kama mwanamke kutokua kiongozi ni mambo ya ukweli ya kimfumo dume.Ila sijasikia hawa wanaodai haki za wanawake wakipinga viti maalum kwaajili ya wanawake pamoja na kupewa max za chini kwenye ufaulu.Mwanamke apewe viti maalum bungeni kwa sababu gani?Huku ni kumwaminisha kuwa yeye ni dhaifu.Unampa upendeleo wa ufaulu kwa nini?Hii sio HAKI!

Wivu wa kike ukoje na wakiume ukoje?

mfumodume una mambo mengi yaliyo vichwani mwetu? Kipi ambacho hakipo vichwani mwetu?

Unaposema dhana yenyewe haijaanzia kwetu, halafu unajirudi hapohapo kusema haina maana ni mbaya, maana yako nini kusema haijaanzia kwetu kama si kuonyesha kwamba haitufai kwa sababu si yetu ni ya wakoloni wazungu wenye conspiracies zote against muafrika?

Una hakika tafsiri ya kuoa na kuolewa kwenye utamaduni wetu imetokana na dini? Dini gani hasa?

Viti maalum mie navipinga vyote, regardless, au kama anavyosema Masha, irregardless.
 
Ungetaka kuishi kama jamii static usingekuwa kwenye internet sasa hivi wewe, kwani jamii yetu ndiyo iliyovumbua umeme, computer na internet?

Swala si jambo limeanzia wapi, swala ni je, linafaa au halifai?

Hizi habari za kutukuza sana a failing othodoxy zinatufaa au hazitufai?

Utakuta mtu kwao masikini hajiwezi hali wala mali, na yeye anachangisha masikini wenzake kibaooo wenye majukumu kemkem, bora hata kama angekuwa anawachangisha kujenga nyumba tungejua anafanya la maana.

Kumbe muharusi mkuuubwa.

Halafu baada ya harusi wanaingia kwenye chumba cha kupanga, hata zawadi walizonunuliwa hawana pa kuziweka.

Baada ya miaka miwili talaka.

Hivyo hiyo akili?

Kati ya huyo na anayefuatisha mapenzi ya kweli yasiyo na kelele za miharusi wala ndoa za kuapishana nani afadhali?

Kiranga kumbe tatizo ni michango ya Harusi? Jee iwapo hakuna michango jee hakuna tatizo?
Hebu kwa muwazi ,nini tatizo lako ndowa au mambo yanayofanywa kabla ya ndowa?
Tumekuwa tkihangaishana bure kumbe hukufahamu maudhui yangu! Labda niweke wazi zaidi.
Kwanini katika mara nyingi wazee wanawake wanawasaidia watoto wao na uhusiano wa nje ya ndowa? Na kwanini sisi wanaume huwa tunapinga mabinti wetu kuwa na uhusiano wa nje ya ndowa wakati tunajigharimukatika ndowa za wenetu ili uhusiano uwe ndani ya ndowa?
 
Naona hujauliza hizo flaws ni zipi au tayari umeshazijuwa na hivyo unajaribu kuzikimbia? Tusiwe wakubwa wa nadharia kusahau real applications. Hebu niambie hao watu waliostaarabika wote duniani wanafikia wapi mwisho wa relations zao, si celebrities, si royals , si viongozi ambao walio huru kuwa na uhusiano huo unaoueleza wewe.

Wewe unayetaka ku prove kwamba kuna flaws ndiye unatakiwa kuniambia mie flaws ni zipi, usisubiri nizi extract kama dentist anayetaka ku extract a molar.

Wakubwa wa nadharia ni wale wanaofikiri kwamba dunia hii haibadiliki, mwanamke anaolewa, mwanamme anaoa, mtoto wa kike anatakiwa kutaka kuolewa siku zote, na hawezi kukataa kuolewa hata kama jamii yake inamshurutisha kuolewa kwa mfumodume.

Wanaokata nadharia ni wale wanaosema dunia inabadilika, dhana ya kwamba mwanamke anaolewa na mwanamme anaoa inaweza kuwa challenged, mtoto wa kike anaweza kuchumbiwa akaona kuolewa gozigozi akataka kusoma, hususan kwa sababu ndoa zenyewe zimekuwa predicated katika mfumo dume unaomtaka yeye "aolewe" na mwanamme "amuoe".

Nani kasema kuna watu waliostaarabika duniani? Dhana nzima ya "kustaarabika" ni ya kumdharau muafrika kwa sababu mzizi wa neno "kustaarabika" ni "arabika" na "arab". Kwamba huwezi kuwa enlinghtened mpaka ugeze waarabu. Mi natafuta vingine, si kustaarabika, kwani kwangu mimi kustaarabika ni utumwa wa kumfuata muarabu.

Naenda kwa etymology, inayoangalia mizizi ya fikra katika mizizi ya maneno ya lugha.

Zaidi ya hapo, siamini kwamba kuna watu walio "enlightened" zaidi ya wengine kama nisivyoamini kwamba kuna zaidi kati ya mwanamke na mwanamme. Kuna wanawake wengine wako zaidi ya wanawake na wanaume wengi, kuna wanaume wengine wako zaidi ya wanawake na wanaume, lakini kama kuna tofauti kati ya wanawake na wanaume it is purely social, nothing inherent.

Kama vile kuna wazungu wengine walio zaidi ya waafrika, na kuna waafrika wengine walio zaidi ya wazungu, social, nothing inherent or biological.

Kwa msingi huu notion nzima ya "waliostaarabika" inakuwa suspect kama sio a relic of the past.

Kuna concepts zilizo enlightened, nyingine hazipo hivyo. Zaidi ya hapo, open season.
 
Unaiaminisha jamii nzima.

Take ndoa for example. Ndoa ni kitu so central katika jamii kiasi cha kwamba ninavyokuja hapa kui-deconstruct watu wengine wanapata pause. Wanasema Astaghafirullah huyu Kiranga.

Lakini ukiangalia ninayoyasema yana ukweli. Ndoa ni stage ambayo katika utamaduni wetu wote tunategemewa kupita, ukishafikisha thirties tu watu wanaanza kukuzonga, harusi lini, wifi yetu yuko wapi, tunataka mjukuu etc.

Lakini ndoa yenyewe kiswahili mwanamme anaoa, mwanamke anaolewa.Na kiswahili hata kama mwanamke kachoka anataka kujitoa, hawezi kum divorce mume, inabidi amuombe mume amdivorce yeye mke.

Huo ndio mfumodume, umekaa katikati ya jamii yetu hata tunaposema "anaoa" na "anaolewa" hatujui kwamba ni mfumodume.

kwa hiyo, unamwaminisha nani? Jamii nzima. Unaiaminisha jamii kwamba mwanamme ni bora katika nini? Practiocally mambo yote ukiondoa mambo ya kike kama urembo, kuzaa, kulea watoto, kupika, umbea na mengine "ya kike kike" kama hayo.

Waliostaarabika wanafanya nini?
 
Kwani nani anamsifia mwanaume kwa umalaya?

SIO SIFA KABISA KAMA SIFA BALI MWANAUME AKIWA MALAYA JAMII HAIONI KAMA TATIZO SANA LAKINI MWANAMKE ANAPOKUWA NA MULTIPLE PARTNER KILA MTU ANAMSHANGAA INCLUDING WANAWAKE WENZAKE WAKATI KWA MWANAUME WATAONGEA NA KUACHA LIPITE (NADHANI Kiranga NDO ALIMAANISHA
 
not to derail the original topic.

My sense is, huyu mama kauliza swali lililo so central katika kupata a paradigm shift katika jamii yetu.

Kwa nini tunakuwa so obsessed over sexual chastity kabla ya ceremony ya harusi/ndoa halafu tukishaihalalisha kwa misherehe inakuwa si big deal?

Watu wazima wawili wakipendana kwa kweli, what's the big deal about misherehe na other farcical extravagances?

Hakuwa na maana hiyo, maana yake ni kuwa unamkataza binti asifanye uzinzi ( nakumbuka ulitumia conception hiyo post yako ya mwanzo) wakati ukialika watu unajuwa kuwa atakwenda kufanya tendo la ndowa?( pengine kwa mtazamo wako wa kimapinduzi tofauti ya majina kwa kitendo kimoja haina maana)
 
Kiranga,kuna wakati unakua mgumu kuelewa na kueleweka.Mtafute ex spika umuulize wivu wa kike na wa kiume ni upi kwa sababu wewe ndo ulimnukuu at the first place,mimi nilikusaidia kuelewa kuwa hakusema wivu ni u-kike bali alisema wivu wa kike.Kuna tofauti kaji ya unaposema wivu ni tabia ya kike na unaposema acha wivu wa kike.Niliposema mfumo dume una mambo yaliyo vichwani nilimaanisha hayapo kwenye hali halisi,pia niliposema dhana mfumo ya dume sio mbaya yote nilimaanisha ina mazuri na ina nadharia zisizokuwepo kwenye uhalisia.Suala la viti maalum sikukulaumu wewe unless uwe mwanaharakati wa haki za wanawake!
 
Kiranga nimekuelewa,kuhusu neno "kuoa" au "kuolewa" wewe unalitafsiri vipi?Kuhusu mwanamke kutokuacha nafikiri hiyo inatokana na imani fulani,sidhani kama tunaweza lizungumzia hapa.Hayo maneno ya kiswahili bado sijaona ubaya wake,tatizo tunayachukulia kutokana na dhana ya mwanamke kutokutoa talaka ambayo kama nilivyosema ni dhana ya imani fulani tena moja tu.Kwenye mfumo dume hapo napo kuna mkanganyiko.Mwanaume na mambo ya kiume.Mwanamke na mambo ya kike.Tukubali kuwa mwanamke anapoambiwa "acha kufanya mambo ya kiume" ni sifa?Sidhani,pia mwanaume anapoambiwa acha mambo ya kike,sio aibu.Unapoyataja mambo ya kikekike wewe ndie unaamua yawe tusi,kashfa au vinginevyo.Tafsiri iliyoko kichwani mwako.Lakini pia huu mfumo unaoitwa dume una mambo mengi lakini mengi zaidi yapo vichwani mwetu zaidi,sio halisi!

Eiyer, tuna mifumo mitatu ya ndowa katika jamii yetu nayo ni dini, mila na Serikali na nafikiri hakuna mfumo wowote unaomzuiya mwanamke kudai talaka. Usimfate Kiranga ambaye anatumia uhaba wa maneno ya Kiswahili kusema kuwa mwanamke hawezi kudai talaka. Kwani hao waliostaarabika hawana sheria na mpangilio wa mwanamke kudai talaka?
Hebu niambie katika mifumo mitatu hii upi haumruhusu mwanamke kudai talaka au kwa vile tunasema mwanamke ameachika,iwapo talaka kadai yeye au kapewa yeye?
 
Unaendeleza mfumodume.

Mie nakuuliza kwa nini unafikiri huyu dada, mwanamke, anataka kuolewa.

Wewe unaniuliza mwanamme kamchumbia kwa nini? Unampa prominence mwanamme, mtu ambaye hata sijamuulizia hapa. Mwanamke anaweza kuwa katika mahusiano na mwanamke, akitaka kumuoa huyo mwanamke, na mwanamke asiwe na haja ya kuolewa.

Zaidi ya hapo, neno "mchumba" hutumika loosely katika kiswahili kwa kumaanisha "boyfriend/girlfriend" na pia "fiancee" kwa sababu hatuna utamaduni wa boyfriend/girlfriend, ni mgeni. Sina hakika katika hii thread neno hili limetumika kama boyfriend au fiancee.

Kwa nini unamleta mwanamme katika swali lililomlenga mwanamke?

Kwa vile wahusika wapo wawili mmoja hana budi kwenda kumchumbia mwengine na bado nasema hata hao waliowastaarabu huomba ridhaa ya wazee wa mwanamke kabla ya ndowa, sisemi uzinifu au kwenda serikalini. Huyo msichana angekuwa huru kukataa ili kuepuka mfumo dume.
 
Kiranga kumbe tatizo ni michango ya Harusi? Jee iwapo hakuna michango jee hakuna tatizo?
Hebu kwa muwazi ,nini tatizo lako ndowa au mambo yanayofanywa kabla ya ndowa?
Tumekuwa tkihangaishana bure kumbe hukufahamu maudhui yangu! Labda niweke wazi zaidi.
Kwanini katika mara nyingi wazee wanawake wanawasaidia watoto wao na uhusiano wa nje ya ndowa? Na kwanini sisi wanaume huwa tunapinga mabinti wetu kuwa na uhusiano wa nje ya ndowa wakati tunajigharimukatika ndowa za wenetu ili uhusiano uwe ndani ya ndowa?

Nimeongelea mengi sana tu, mpaka swala zima la "kuacha milango wazi" na mapenzi ya kweli.

Kama michango ya harusi mbona wengine tunachanga kila siku bila bajeti lakini kuoa hatutaki?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom