Mama kwa Mtoto wa Kiume

Haya mambo yapo sana hasa kwa mama na mtoto wa kiume .Kwenye familia yetu yametokea mimi nina kaka watatu;mama yangu anampenda na kumjali sana huyo wa katikati,hakuna baya analolifanya.Wale wakaka wengine wamelalamika sana huo upendeleo alionao mama kwa mwenzao.Hilo la kufuliwa nalo lipo lakini si zile nguo za ndani.Mfano kwa sasa kijana ana miaka 29 na ameajiriwa lakini ikifika tarehe 20 huwa ana tabia ya kulia ukata wa pesa kiasi kwamba mama huangaika mpaka amtumie fedha Tumeshakaa chini na kumtaadharisha madhara ya kumdekeza kupita maelezo. mama hataki huyu kijana akue na aweze kujitegea.Kwanza kwa sasa yeye anapaswa kutumiwa fedha.
 
Huko kudekeza kumezidi toto kubwa hivyo analidekeza kihivyo khaaa! kwa kifupi mimi sipendi kumdekeza mtoto wa kiume anaweza kuja pata shida sana inapotokea mama anafariki ghafla.Mtoto wa kiume lazima upitie ugumu fulani sio kila kitu cha ubwete tu
 
Hellow Dena! Umeshafika mlangoni kwako? Fungua tu uingie ukapumzike. Natamani niamini hakuna kibaya kinachoendelea ila huyo mtoto akioa mama yake atakufa haraka!
 
Watu kama nyie ndo mnajiita masister duu mtoto wako akijinyea huwezi msafisha mpaka afanye house girl kwani kuna tatizo gani hapo? Wacha mama ampende mwanae hata akifua kufuli ya mwanae hakuna ubaya si wkt alivyo kuwa mtoto alikuwa anafanya hivyo kwa nn sasa asifanye? Vp na matusi nayo wanafanyana?


Dogo dogo unaanzaga vizuri lakini ukifika mwisho kama apo kwenye red noma!
 
Habari Zenu wote haijalishi ni shikamooo, hujambo, mambo vipi, mzima wewe, nk salamu ni salamu nawasalimu kwa heshima kubwa niliyofundishwa na Wazazi wangu(nieleweke siwasifii wazazi wangu)

Naishi nyumba ya kupanga huku nilipo (Afrika) mwenye nyumba ni Land Lady (Mama Mwenye nyumba), Land Lord (spelling sijui kama ziko sawa maana mie kidhungu noti reachable) alifariki muda kidogo hata mimi sikuwepo wala sikudhani kama nitakuja kuishi nchi hii.

Nieleweke sisemi kwa ubaya hapa kwa hili ila kuna kitu kimeniishangaza sana huyu mama yuko karibu sana na kijana wake wa tatu kuzaliwa mpaka watoto wengine wanaona vibaya kabisa mf. rent na bill zote kama umeme, maji, simu, takataka, ulinzi nk anachukua yeye (kijana), matengenezo ya nyumba yeye na mengine mengi anafanya bila kuwashirikisha ndugu zake, mind you anashirikiana na mama yake tena kwa karibu sana.

My pointi is: Kilichonifanya nilete thread hii hapa ni kuwa nimetoka kazini leo jioni narudi home nakuta Mama anafua nguo za kijana aka mtoto wake wa kiume(yule the best of the best) more than 23 yrs mpaka soksi, ch*** nimestuka nusu nizimie kha iweje??? Usiniulize kwanini kwasababu sitajibu


Sitaki mambo ya umbea lakini nimeshangaa nakujiuliza bila kupata majibu na sikutaka kumuuliza mtu wa karibu ili kutaka kujua mambo ya ndani kwao, naona kama hayanihusu vileeee.

Ila nauliza wanajamii hii ni haki kweli maza anakufulia nguo, soksi mpaka nanihinooooo kweli au kuna kitu kinaendelea hapo zaidiii..................... (I stand to be corrected)

Mie ni mpangaji lakini sijapenda hii tabia.

Usiku mwema woteee nawapenda.......................
We umeisi nini DA mana sisi tunaweza judge kutokana na thread tukawa tunatoa maamuz pumba.
 
mi bado naendelea kuamini kuwa LABDA NI UPENDO TU WA KAWAIDA BAINA YA MAMA NA MWANA WAKE.
 
Huko kudekeza kumezidi toto kubwa hivyo analidekeza kihivyo khaaa! kwa kifupi mimi sipendi kumdekeza mtoto wa kiume anaweza kuja pata shida sana inapotokea mama anafariki ghafla.Mtoto wa kiume lazima upitie ugumu fulani sio kila kitu cha ubwete tu

Fafanua hapo kwenye red shida gani ?.
 
habari zenu wote haijalishi ni shikamooo, hujambo, mambo vipi, mzima wewe, nk salamu ni salamu nawasalimu kwa heshima kubwa niliyofundishwa na wazazi wangu(nieleweke siwasifii wazazi wangu)

naishi nyumba ya kupanga huku nilipo (afrika) mwenye nyumba ni land lady (mama mwenye nyumba), land lord (spelling sijui kama ziko sawa maana mie kidhungu noti reachable) alifariki muda kidogo hata mimi sikuwepo wala sikudhani kama nitakuja kuishi nchi hii.

Nieleweke sisemi kwa ubaya hapa kwa hili ila kuna kitu kimeniishangaza sana huyu mama yuko karibu sana na kijana wake wa tatu kuzaliwa mpaka watoto wengine wanaona vibaya kabisa mf. Rent na bill zote kama umeme, maji, simu, takataka, ulinzi nk anachukua yeye (kijana), matengenezo ya nyumba yeye na mengine mengi anafanya bila kuwashirikisha ndugu zake, mind you anashirikiana na mama yake tena kwa karibu sana.

My pointi is: Kilichonifanya nilete thread hii hapa ni kuwa nimetoka kazini leo jioni narudi home nakuta mama anafua nguo za kijana aka mtoto wake wa kiume(yule the best of the best) more than 23 yrs mpaka soksi, ch*** nimestuka nusu nizimie kha iweje??? Usiniulize kwanini kwasababu sitajibu


sitaki mambo ya umbea lakini nimeshangaa nakujiuliza bila kupata majibu na sikutaka kumuuliza mtu wa karibu ili kutaka kujua mambo ya ndani kwao, naona kama hayanihusu vileeee.

Ila nauliza wanajamii hii ni haki kweli maza anakufulia nguo, soksi mpaka nanihinooooo kweli au kuna kitu kinaendelea hapo zaidiii..................... (i stand to be corrected)

mie ni mpangaji lakini sijapenda hii tabia.

Usiku mwema woteee nawapenda.......................
mtoto kwa mama........................?????????:
 
Fafanua hapo kwenye red shida gani ?.

Amezoea kufanyiwa kila kitu kwahiyo mama akifariki atapata shida ya kuanza kufanya mambo yake mwenyewe au kutafuta atakaechukua nafasi ya mama!!Kwani hujasoma thread yote?
 
mmh!!! watu kwa kuelewa ndivyo sivyo .... eti afafanue maana ya kupata shida mamake akifariki!!!!.................
 
Ngongo naamini ulielewa tofauti kabisa .........na hiyo shida aliyoisema Lizzy.
 
Kwa ulimwengu ulivyoharibika (bora kusema tulivyouharibu) lolote linawezekana, ingawa mimi hilo la kubanjuana siliweki akilini sana. Ni kweli mapenzi ya mama kwa mtoto wa kiume yanapovuka mipaka watu wanaweza kuwa na wasiwasi, hasa katika jamii zetu za Kiafrika, ambapo falsafa ya malezi ni "kama hukutwanga huli na ukibalehe tu unapewa panga ujenge kibanda chako pembeni". Haya mambo ya kufuliana mpaka chupi na umri wa miaka 40 bado unaishi na wazazi wako yako sana uzunguni na kwenye miji kwa baadhi ya familia.

Lakini kama ilivyosemwa, "mtoto kwa mama hakui" kwa hiyo hakuna zaidi ya kumdekeza tu. Ubaya ni kama alivyosema Lizy, mtoto wa kiume kudekezwa kiasi hicho ni hatari kwa mtoto. Mtoto wa malezi ya aina hii hata akioa huwa hatafuti mke bali mama.
 
hayaaaaaaaaa babuu!!!

Hujambo mpenzi?

Naomba unisaidie kumuuliza Dena, alijuaje hizo ch.upi zinazofuliwa ni za mtoto wa huyo mama?.......... Alishawahi kumwona amezivaa? Wapi? Saa ngapi? Ilikuwaje?

Narudi kitandani kulala.
 
Hujambo mpenzi?

Naomba unisaidie kumuuliza Dena, alijuaje hizo ch.upi zinazofuliwa ni za mtoto wa huyo mama?.......... Alishawahi kumwona amezivaa? Wapi? Saa ngapi? Ilikuwaje?

Narudi kitandani kulala.

Mhhh...babu kwa maswali??!!!!

mzima lakini wewe?
 
Back
Top Bottom