Mbunge wa CCM
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 475
- 22
katika mchango wangu leo kwenye thread moja nilitoa kisa hiki cha kweli kama mfano wa kile nilichochangia. kutokana na utata wake nimeona niweke hapa kama thread inayojitegemea ili great thinkers wa JF wapate fursa ya kuijadili kwa kina kwani inatugusa sote na hususani ndoa zetu tunazozienzi daima.
kisa chenyewe ni hiki:
kuna jamaa yangu mmoja mkewe alikuwa jeuri sana hadi akampiga talaka. kwa sababu ya mtoto, jama hakumwondoa nyumbani mara moja bali alimtegea aondoke mwenyewe kwa hiyari yake na wakati wote alimpa mtaumizi kamili bila kukosa. haukupita muda yule bwana alimhurumia kwa kumwona hana raha, akamhakikishia kuwa kama hataondoka kwa hiyari yake, kamwe yeye hatamfukuzza na kumtaka aondoe mawazo, waheshimiane na kulea mtoto wao mpendwa. mama akaanza kupata amani moyoni, mume akajiona hana tena uhalali na wife kwani alishamkana. akapata nyumba ndogo, na wife akabaki kulea mtoto tu. yalipomshinda wife aliomba na anaendelea kuomba kila anapotaka na sasa ni mwaka wa pili na majuzi wamebarikiwa mtoto mwingine! wanmpenda na kumlea kwa furaha.
wasipokuambia habari yao, kamwe huwezi kujua kuwa wana talaka mikononi mwaao.
kuna wengine alifikiri ni hadithi na wengine wakasema inafafanana na filamu moja ya kihindi, lakini ni kisa cha kweli na mimi niliyekileta si tu nilichangia na kushiriki kwa hali na mali katika harusi yao bali pia nimekuwa mshauri wao mkubwa katika maisha yao ya ndoa ndio maana ni mmoja wa watu wachache sana wanojua habari hii hapa duniani.
kweli ndoa zina mambo. leteni maoni yenu tuwasaidie wenzetu na tujimulike nasi wenyewe tuko salama kiasi gani.
Mungu zibarki ndoa zetu.
kisa chenyewe ni hiki:
kuna jamaa yangu mmoja mkewe alikuwa jeuri sana hadi akampiga talaka. kwa sababu ya mtoto, jama hakumwondoa nyumbani mara moja bali alimtegea aondoke mwenyewe kwa hiyari yake na wakati wote alimpa mtaumizi kamili bila kukosa. haukupita muda yule bwana alimhurumia kwa kumwona hana raha, akamhakikishia kuwa kama hataondoka kwa hiyari yake, kamwe yeye hatamfukuzza na kumtaka aondoe mawazo, waheshimiane na kulea mtoto wao mpendwa. mama akaanza kupata amani moyoni, mume akajiona hana tena uhalali na wife kwani alishamkana. akapata nyumba ndogo, na wife akabaki kulea mtoto tu. yalipomshinda wife aliomba na anaendelea kuomba kila anapotaka na sasa ni mwaka wa pili na majuzi wamebarikiwa mtoto mwingine! wanmpenda na kumlea kwa furaha.
wasipokuambia habari yao, kamwe huwezi kujua kuwa wana talaka mikononi mwaao.
kuna wengine alifikiri ni hadithi na wengine wakasema inafafanana na filamu moja ya kihindi, lakini ni kisa cha kweli na mimi niliyekileta si tu nilichangia na kushiriki kwa hali na mali katika harusi yao bali pia nimekuwa mshauri wao mkubwa katika maisha yao ya ndoa ndio maana ni mmoja wa watu wachache sana wanojua habari hii hapa duniani.
kweli ndoa zina mambo. leteni maoni yenu tuwasaidie wenzetu na tujimulike nasi wenyewe tuko salama kiasi gani.
Mungu zibarki ndoa zetu.