Ngaliba Dume
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,710
- 3,669
Jimbo la Ismani ni moja kati ya majimbo maskini Tanzania na mkoa wa Iringa.Ni jimbo linalongoza kwa njaa,ukosefu wa Elimu,maji na huduma ya Afya. Kwa mda mrefu vijana na wazee wamehtaji mabadiliko lakin hawakupata wa kumdhamini,alikuwepo Dr.Kapwani kwa tiketi ya Chadema,lakini alikuwa mwepesi kwa kuhongwa na hatimaye kutorudisha fomu adi siku ya mwisho(Mungu ampe uzima mana amepooza) Tumefarijika na ujasiri wa Chiku Abwawa,tumeona harakati zako,na usisite kutembelea Jimbo la Isman walau upate shida na matatizo yetu uyapeleke Bungeni.Mbunge wetu hatuwakilishi,hatujawah muona na wala hajawah kutetea maslah yetu kwa kisingzio kuwa n waziri wa Serikali. Vijiji vyetu havina maji,hatuna huduma ya afya ya uhakika.Maji tunapata toka mto Ruaha,makorongoni msimu wa mvua na bwawa la Mtera ambayo si salama kabisa kwa afya zetu. Vituo vya afya n kwa msaada wa kanisa,vijana hawana uwezeshaji na hatuna wa kutusemea Dunia ikajua dhima na shida zetu.Karibu mama Chiku Abwao,katka wewe tumeona matumaini. LUKUVI VANGIMEMBE WILLIAM ametukimbia,hayupo tena nasi.