Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,011
- 144,371
Mama Shelukindo, awali ya yote nakupongeza sana kwa mchango wako wa jana bungeni kuhusu bajeti.Umeonyesha ukomavu wa hali ya juu kisiasa kwa kutambua mchango wa upinzani ktk maendeleo ya taifa lolote tofauti na wale wanaojiita wachumi wa daraja la kwanza lakini kisiasa,kimaadili,na hata kiungozi wametuthibitishia ni bure kabisa au tuseme ni zero.Wamesoma lakini hawajaelimika!
Katika jambo moja uliloligusia ktk kuchangia bajeti jana, ni juu ya uamuzi ambao kwa kweli, una harufu ya ubinafsi na jambo hilo si lingine bali ni kuhusu uuzaji wa nyumba za serikali.Mimi binafsi nilisikitishwa na kuumizwa sana na huu uamuzi.Nachokushauri mama yangu ni kuwa hebu peleka hoja binafsi juu ya swala hili ili ikiwezekana nyumba hizi zirudishwe.Wabunge mkiamua jambo hili linawezekana kabisa.
Nakumbuka mh.Christopher Ole Sendeka aliwahi kuahidi pale bungeni kuleta hoja binafsi juu ya swala hili lakini nashangaa mpaka leo yuko kimya.Sasa sijiu alitoa kauli ile kisiasa tu kutupiga changa la macho au bado ana nia ya kufanya hivyo mimi sijiu.
Mama Shelukindo, maadamu umeligusia swala hili, ni vizuri ulifanyie kazi kwa uzito unaostahili na utakumbukwa siku zote za maisha yako kama ulivyofanya juu ya bwana Jairo.Najua hata huko bungeni wako wengi waliofaidika na uamuzi huu ila wewe timiza wajibu wako tu.
Mwisho nasema mungu akupe nguvu na ujasiri na sisi wazalendo tuko nyuma yako ktk maombi.
Katika jambo moja uliloligusia ktk kuchangia bajeti jana, ni juu ya uamuzi ambao kwa kweli, una harufu ya ubinafsi na jambo hilo si lingine bali ni kuhusu uuzaji wa nyumba za serikali.Mimi binafsi nilisikitishwa na kuumizwa sana na huu uamuzi.Nachokushauri mama yangu ni kuwa hebu peleka hoja binafsi juu ya swala hili ili ikiwezekana nyumba hizi zirudishwe.Wabunge mkiamua jambo hili linawezekana kabisa.
Nakumbuka mh.Christopher Ole Sendeka aliwahi kuahidi pale bungeni kuleta hoja binafsi juu ya swala hili lakini nashangaa mpaka leo yuko kimya.Sasa sijiu alitoa kauli ile kisiasa tu kutupiga changa la macho au bado ana nia ya kufanya hivyo mimi sijiu.
Mama Shelukindo, maadamu umeligusia swala hili, ni vizuri ulifanyie kazi kwa uzito unaostahili na utakumbukwa siku zote za maisha yako kama ulivyofanya juu ya bwana Jairo.Najua hata huko bungeni wako wengi waliofaidika na uamuzi huu ila wewe timiza wajibu wako tu.
Mwisho nasema mungu akupe nguvu na ujasiri na sisi wazalendo tuko nyuma yako ktk maombi.