Mama anamtetea mke wangu pamoja na kunisaliti

msalala kwetu

Member
Jan 29, 2016
71
63
Wakuu habari zenu,

Mwaka 2012 nilienda kozi nje ya nchi kwa miezi 3 hapa hapa Africa, nyuma niliacha mke na watoto wawili walio primary school,
nikiwa kozi rafiki yangu akawa anakwenda kulala kwangu mara kwa mara especially weekends, akawa analala chumbani kwangu, haijajulikana hadi leo walianza lini uhusiano huo, alikua akienda kwangu kwa gia ya kuwaona wanaendeleaje.

Niliporudi, nikakuta wife kamtimua kazi house girl wetu bila maelezo ya kueleweka, nikapuuzia, baadae rafiki kipenzi wa wife wa tangu shule na ambae wanasali jumuia moja maana amepanga mitaa yetu, akaniambia kwa urefu uhusiano wa wife na mshikaji wangu, ila kwa sharti la kutomtaja whatsoever the case.

Baadae nikaona niende kumtafuta yule housegurl aliefukuzwa kazi na wife nikampata, aka confirm habari zile na kunieleza kwa kirefu na ndio kisa cha yy kufukuzwa kazi pale kwangu baada ya kumuhoji kuwa " kwanini unamfanyia shemeji matendo haya.

Baada ya kujiridhisha nikamuita wife mbele ya wazazi wake na kueleza kila kitu akabaki kimya akilia, nikamkabidhisha kwa wazee wake hapo hapo, akiwa kwao aliendelea kunibembeleza na kuniomba msamaha kwa kutuma watu mbali mbali wenye heshima, sikurudi nyuma, akasafiri kijijini kwetu kuwaona wazazi wangu na kuwaangukia, alikaa huko mwezi mzima.

Baadae wakaja wote na wazazi wangu hadi kwangu, wakasema pamoja na yote yaliyotokea niishi nae hivyo ametubu, sio ombi ni amri ndio maana wamemleta wao, moyoni nikasema najua cha kufanya, nilishindwa kuwaelewa, wanamtetea mtu ambae ameniumiza despite kuwa nilimuachia kadi ya benki awe anachukua mshahara wangu kuendesha familia, mimi kule kozi nikawa naishi kwa chakula cha kulipiwa na posho kidogo tu.

Wazazi walipoondoka tu, nikaanza kumfanyia visa na matendo mabaya ili aondoke, nikatafuta msichana wangu nikawa najiachia nae pale mtaani bila woga, nakunywa nae bar za mtaani, nikaanza kuja nae home nalala nae chumba kingine, akawa anatufanyia fujo lakini namdhibiti kiume hadi tunajifungia chumbani, nilikua nafanya haya yote ili wife aondoke lakini wapi, yupo tu, anawapigia simu wazazi kushitaki wakinipigia nawaambia huyu ni mke wenu mimi nilimtimua nyinyi mkamleta tena, ni mke wenu.

Tumeishi kwa hali hii tangu 2012 hadi sasa, yule msichana wangu akachoka hizi vurugu akaamua kuniacha, sasa nina mwingine, sina uhakika kama yupo mwanamke huko nje angeweza kuvumilia matendo niliyomtendea huyu wife, lengo ni aondoke lakini hataki kuondoka hata baada ya kumu offer kugawana mali, watoto wameathirika sana na hizi vurugu huwa nikiwapeleka kwa dada yangu wanakataa kurudi

Lakini yote haya aliyasababisha yeye kwa tamaa, nilishamueleza tangu siku ya ndoa kanisani kuwa nitakusamehe yote lakini uzinzi huwa sisamehi, sijamgusa tangu 2012.

Wadau naombeni ushauri nimtoe vipi huyu mwanamke?
Au mnadhani ipo siku naweza kusahau usaliti wake na kumpenda?

Na kama ni kumuacha ndani tutaishi hivi hadi lini?

Kuhusu watoto mnaonaje niwaache uko uko kwa dada yangu walelewe huko wasomee huko huko? Maana tangu likizo ya December wamekatalia huko hivyo school bus huwa linawafuata huko badala ya kwangu.

Nitaheshimu mawazo yenu as my last resort.
 
dawa nyepesi sana ondoka wewe kaanze maisha kwingine mbona simple like that mkuu..... weka miakakati namana ya kullipia watoto ada na matunzo yote.. acheni ubinafsi vikojoleo vyenu vinawaumiza watoto embu wapeni watoto relief hata kidogo jamani.. baba analala na mwanamke mwingine mama analala na wanaume mwingine kweli? mnafundisha nini hawa malaika? embu we mwanume kuwa mwanaume ondoka hapo kama ni swala la hati ya nyumba transfer kwenye majina ya watoto that all .... usiwaze kwamaba unampa faida mama waza kuwa watoto wako wanahitaji malezi mema .. kama ni wasi wasi wa mkeo kuja kutiwa ndani kwako kashatiwa hata kwabla ujamwacha.......

kuwaacha watoto kwa dada yako eti kisa nyie mnashindana kugongana kwenye nyumba yeni ni upuuzi tena upuuzi mkubwa
 
utaishi nae kwenye shida na raha.
Na anapoanguka mwenzako mshike mkono umwinue.
Tafakari kwa kina dunia ya leo magonjwa mengi yamejaa kemkem, kubadilisha wanawake sio kutatua tatizo hapo, unajimaliza wewe mwenyewe mkuu.
Maadamu amekuomba msamaha kaeni chini myazungumze mmalize tofauti zenu na mjenge familia yenu pia.
 
Wakuu habari zenu

Mwaka 2012 nilienda kozi nje ya nchi kwa miezi 3 hapa hapa Africa, nyuma niliacha mke na watoto wawili walio primary school
Nikiwa kozi rafiki yangu akawa anakwenda kulala kwangu mara kwa mara especially weekends, akawa analala chumbani kwangu, haijajulikana hadi leo walianza lini uhusiano huo, alikua akienda kwangu kwa gia ya kuwaona wanaendeleaje

Niliporudi, nikakuta wife kamtimua kazi house girl wetu bila maelezo ya kueleweka, nikapuuzia, baadae rafiki kipenzi wa wife wa tangu shule na ambae wanasali jumuia moja maana amepanga mitaa yetu, akaniambia kwa urefu uhusiano wa wife na mshikaji wangu, ila kwa sharti la kutomtaja whatsoever the case, baadae nikaona niende kumtafuta yule hg aliefukuzwa kazi na wife nikampata, aka confirm habari zile na kunieleza kwa kirefu na ndio kisa cha yy kufukuzwa kazi pale kwangu baada ya kumuhoji kuwa "" kwa nn unamfanyia shemeji matendo haya

Baada ya kujiridhisha nikamuita wife mbele ya wazazi wake na kueleza kila kitu akabaki kimya akilia, nikamkabidhisha kwa wazee wake hapo hapo, akiwa kwao aliendelea kunibembeleza na kuniomba msamaha kwa kutuma watu mbali mbali wenye heshima, sikurudi nyuma, akasafiri kijijini kwetu kuwaona wazazi wangu na kuwaangukia, alikaa huko mwezi mzima

Baadae wakaja wote na wazazi wangu hadi kwangu, wakasema pamoja na yote yaliyotokea niishi nae hivyo ametubu, sio ombi ni amri ndio maana wamemleta wao, moyoni nikasema najua cha kufanya, nilishindwa kuwaelewa, wanamtetea mtu ambae ameniumiza despite kuwa nilimuachia kadi ya benki awe anachukua mshahara wangu kuendesha familia, mm kule kozi nikawa naishi kwa chakula cha kulipiwa na posho kidogo tu

Wazazi walipoondoka tu, nikaanza kumfanyia visa na matendo mabaya ili aondoke, nikatafuta msichana wangu nikawa najiachia nae pale mtaani bila woga, nakunywa nae bar za mtaani, nikaanza kuja nae home nalala nae chumba kingine, akawa anatufanyia fujo lakini namdhibiti kiume hadi tunajifungia chumbani, nilikua nafanya haya yote ili wife aondoke lakini wapi, yupo tu, anawapigia simu wazazi kushitaki wakinipigia nawaambia huyu ni mke wenu mm nilimtimua nyinyi mkamleta tena, ni mke wenu

Tumeishi kwa hali hii tangu 2012 hadi sasa, yule msichana wangu akachoka hizi vurugu akaamua kuniacha, sasa nina mwingine, sina uhakika kama yupo mwanamke huko nje angeweza kuvumilia matendo niliyomtendea huyu wife, lengo ni aondoke lakini hataki kuondoka hata baada ya kumu offer kugawana mali, watoto wameathirika sana na hizi vurugu huwa nikiwapeleka kwa dada yangu wanakataa kurudi

Lakini yote haya aliyasababisha yy kwa tamaa, nilishamueleza tangu siku ya ndoa kanisani kuwa nitakusamehe yote lakini uzinzi huwa sisamehi, sijamgusa tangu 2012,

Wadau naombeni ushauri nimtoe vipi huyu mwanamke?
Au mnadhani ipo siku naweza kusahau usaliti wake na kumpenda?

Na kama ni kumuacha ndani tutaishi hivi hadi lini?

Kuhusu watoto mnaonaje niwaache uko uko kwa dada yangu walelewe huko wasomee huko huko? Maana tangu likizo ya December wamekatalia huko hivyo school bus huwa linawafuata huko badala ya kwangu

Nitaheshimu mawazo yenu as my last resort
fanya haya:
1.peleka watoto boarding school. hakikisha kila visiting day unakwenda kuwaona. jiandikishe shuleni kuwa wewe ndio ccontact person in case of anything kuhusu watoto japokuwa usimnyime nafasi ya mama kwenda kuwaona watoto shuleni
2.hama hapo nyumbani. tafta chumba/nyumba na ishi huko. nyumba hiyo acha huyo mama aishi na watoto wako. usimtimue.
3.watoto wakiwa likizo waache wakae kwa mama yao
4.tunza familia muda wote watoto wanapokuwa likizo.likizo ikiisha na watoto kurudi shule, huyo mama usimpe matunzo yoyote kwa sababu hastahiki kwa muda huo,unless watoto wamerudi kwa dharura nyumbani kama ugonjwa nk.
5.watoto wakiwa likizo , hakikisha una spend muda mwingi nao na toka nao out mara kwa mara kwa michezo, kutembelea ndugu nk. show them love , kumbuka mama ndie atakuwa anakaa nao nyumbani likizo hivyo kuwa nao muda mwingi, usipoonesha love mama ni rahisi kuwaspoil watoto na wakakichukia.

mwisho: ugomvi wenu na visirani vyenu visiwahusishe watoto, they are very innocent , mbele yao mnatakiwa mbehave in a very mature way.
 
Hukupaswa kulipiza baya kwa baya kwakua hiyo imeathiri hadi watoto amabao hawana hatia, cha msingi hapo ni kumsamehe ukimwekea kinyongo ni sawa na kunywa sumu ambayo itakua inakua polepole pia uwe na huruma na watoto usidhani wanajisikia vizuri kukaa kwa shangazi ni kwa vile tu hawana mbadala. Hata wewe unastahili lawama kwakua unamletea mwanamke mwingine tena mbele yake na unafanya naye huo upuuzi wenu, si bora hata yeye alifanya hivyo wakati haupo? Usijione kua wewe ni mtakatifu sana kwa hayo unayofanyia mwenzio, ebu huyo anaishi vizuri na familia yake wewe haueleweki. Hata ukioa mwanamke mwingine haitakua suluhisho. Take care mwana wane.
 
msalala kwetu, Pole sana, Lakini wewe ni katilii khaswa.... Una moyo wa chuma/jiwe !! Mwenzio alifanya maovu kwa siri .. Nawe ulifanya dhahiri mbele ya macho yake kwa miaka kadhaa (kuzini na ke z nyumani kwenu) !!

Ushauri ntakaokuppa ni huu:- TUBU na ufute Msongo unaokutafuna kichwani kwako "START A NEW PAGE" !!
naye mke aTUBU na mupalilie upya shamba la mapenzi na muitunze familia yenu kwa Upendo !1 (usisahu una watoto the need you both) !!
Huko Msalala si geita huko au.......??
 
fanya haya:
1.peleka watoto boarding school. hakikisha kila visiting day unakwenda kuwaona. jiandikishe shuleni kuwa wewe ndio ccontact person in case of anything kuhusu watoto japokuwa usimnyime nafasi ya mama kwenda kuwaona watoto shuleni
2.hama hapo nyumbani. tafta chumba/nyumba na ishi huko. nyumba hiyo acha huyo mama aishi na watoto wako. usimtimue.
3.watoto wakiwa likizo waache wakae kwa mama yao
4.tunza familia muda wote watoto wanapokuwa likizo.likizo ikiisha na watoto kurudi shule, huyo mama usimpe matunzo yoyote kwa sababu hastahiki kwa muda huo,unless watoto wamerudi kwa dharura nyumbani kama ugonjwa nk.
5.watoto wakiwa likizo , hakikisha una spend muda mwingi nao na toka nao out mara kwa mara kwa michezo, kutembelea ndugu nk. show them love , kumbuka mama ndie atakuwa anakaa nao nyumbani likizo hivyo kuwa nao muda mwingi, usipoonesha love mama ni rahisi kuwaspoil watoto na wakakichukia.

mwisho: ugomvi wenu na visirani vyenu visiwahusishe watoto, they are very innocent , mbele yao mnatakiwa mbehave in a very mature way.
Your Great Thinker.Respect
 
Msamehe, ona unavyohangaika mwisho utapata maradhi utakufa umwachie kila kitu.
Chukulia tu kiume, jikaze msamehe rudini chumbani ya huko mkapime ili uendelee na maisha.

Hakika hakuna mtu wa kuvumilia harufu ya mav.i ya mtu mwingine, hakuna mwanamke wa kuweza kumlea mtoto wa mwanamke mwingine.

Utaishia kufa mwanangu msamehe yaishe. Wapo wanaume wenzio wanaoumizwa zaidi yako lakini kwa ajili ya watoto wanavumilia tu. Jikaze mtoto wa kiume, yamalize.
 
Wakuu habari zenu


Baada ya kujiridhisha nikamuita wife mbele ya wazazi wake na kueleza kila kitu akabaki kimya akilia, nikamkabidhisha kwa wazee wake hapo hapo, akiwa kwao aliendelea kunibembeleza na kuniomba msamaha kwa kutuma watu mbali mbali wenye heshima, sikurudi nyuma, akasafiri kijijini kwetu kuwaona wazazi wangu na kuwaangukia, alikaa huko mwezi mzima


Kumbe wewe mtu wa Mkoa na siyo born town ndiyo maana huyo demu amekuzingua ameshakuona wewe mlugaluga, madem wa town tunawezana nayo sisi wa town!
 
Mkuu hiyo ID yako inanikumbushaga mbali sana, it was 2011 nilipata breakdown ya siku 4 hapo Msalala kwenu.. Nimekumbuka mbali sana, enzi hizo nilikua nasafiri sana hasa kwa gari.. Natembea mpaka 1200km per day tena mwenyewe tu.
 
Mmn,Hii kuacha wife nyumbani imewatokea puani wengi na kuna wengi wanajulikana wapo mjini hapa,Bw unasoma nje huku nyuma jamaa anakuwa kama ameoa yeye.Mkeo anafirigiswa siku ukija njia unaukuta imekuwa kubwa ajabu ...!
 

Similar Discussions

9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom