Babu Lao
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 2,043
- 179
Mtoto Juma ambaye alikuwa akijieleza huku akilia, alisema, "pamoja na kujitetea kwa muda mrefu lakini mama hakunielewa hata kidogo na kuendelea kuning'ang'aniza kwamba mimi ndiye mwizi niliyemuibia fedha zake," alisema na kuongeza:
"Aliniingiza ndani na kisha kunifunga mikono yote miwili pamoja na miguu kwa mpira wa kufungia mizigo kwenye baiskeli na kuanza kunipiga" .
Alidai baada ya kipigo hicho, mama yake hakumfungulia mpira aliokuwa amemfunga miguuni na mikononi hali iliyomlazimu kulala sakafuni kwa siku tatu kabla ya kufunguliwa na kukutwa mikono imevimba.
Kwa mujibu wa mtoto huyo, mama yake alipokuta mikono imevimba alichemsha maji ya moto na kumkanda na alipoona uvimbe haupungui, aliamua kuchukua barafu na kumuwekea kwenye mikono.
Inaelezwa kwamba jana asubuhi ndipo mtoto huyo alifunguliwa na baada ya kutoka nje, alikimbilia barabarani alipokutana na wasamaria wakampeleka kwa Mwenyekiti wa Kitongoji, Sosthenes Mahushi.
Angalizo: Je huyu ni mama mzazi kweli wa mtoto au alimuiba akiwa mdogo?????
"Aliniingiza ndani na kisha kunifunga mikono yote miwili pamoja na miguu kwa mpira wa kufungia mizigo kwenye baiskeli na kuanza kunipiga" .
Alidai baada ya kipigo hicho, mama yake hakumfungulia mpira aliokuwa amemfunga miguuni na mikononi hali iliyomlazimu kulala sakafuni kwa siku tatu kabla ya kufunguliwa na kukutwa mikono imevimba.
Kwa mujibu wa mtoto huyo, mama yake alipokuta mikono imevimba alichemsha maji ya moto na kumkanda na alipoona uvimbe haupungui, aliamua kuchukua barafu na kumuwekea kwenye mikono.
Inaelezwa kwamba jana asubuhi ndipo mtoto huyo alifunguliwa na baada ya kutoka nje, alikimbilia barabarani alipokutana na wasamaria wakampeleka kwa Mwenyekiti wa Kitongoji, Sosthenes Mahushi.
Angalizo: Je huyu ni mama mzazi kweli wa mtoto au alimuiba akiwa mdogo?????