Alfu Lela Ulela
JF-Expert Member
- Oct 29, 2010
- 1,255
- 77
Rais wa Chuo Kikuu cha St.Augustine Mwanza Bw.Malisa Godlisten EJ, amechaguliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa shirikisho la vyuo vikuu vinavyomilikiwana baraza kuu la maaskofu Tanzania (TEC), na vilivyo chini ya Chuo Kikuu cha St.Augustine yaani SU-SAUT.
Malisa ambaye anafahamika kwa harakati zake za kupigania maslahi ya wanyonge na kukosoa udhaifu wa serikali alipata kura 16 dhidi ya kura 4 alizopata Bw.Donath Salla aliyekuwa mpinzani wake.
Uchaguzi huo ulifanyika juzi katika chuo kikuu kishiriki cha Elimu Mwenge kilichopo Moshi, wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SU-SAUT (Annual General Meeting). Jumla ya vyuo tisa vilishiriki katika mkutano huo, isipokuwa Chuo Kikuu kishiriki cha Jordan Morogoro,na Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Bugando ambavyo vilikosa uwakilishi.
Malisa ambaye alishinda urais wa SAUT kwa kishindo licha ya hujuma nyingi zilizofanywa dhidi yake, alikuwa Katibu Mwenezi wa Chadema (CHASO-SAUT) chuoni hapo, kabla ya kugombea Urais. Pia amewahi kuwa mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA wilaya ya Moshi Mjini.
Pamoja na kuwa kiongozi Malisa amekuwa mwanaharakati wa muda mrefu, ambapo makala zake nyingi zimekuwa zikiibua gumzo miongoni mwa jamii. Mwaka 2009 akiwa kidato cha sita alivamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa kichwani kwa panga, ikiwa ni siku chache tu baada ya makala yake kuchapwa gazeti la MwanaHalisi yenye kichwa MTOTO WA MKULIMA AMEANZA KUPOTEZA IMANI
Viongozi wengine waliochaguliwa katika mkutano huo ni Malima Silas (Mwenyekiti), Joseph Rufili (Makamu Mwenyekiti), Donath Salla (Naibu Katibu Mkuu) na Ephraim Kababaa (Mweka Hazina).
Malisa ambaye anafahamika kwa harakati zake za kupigania maslahi ya wanyonge na kukosoa udhaifu wa serikali alipata kura 16 dhidi ya kura 4 alizopata Bw.Donath Salla aliyekuwa mpinzani wake.
Uchaguzi huo ulifanyika juzi katika chuo kikuu kishiriki cha Elimu Mwenge kilichopo Moshi, wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SU-SAUT (Annual General Meeting). Jumla ya vyuo tisa vilishiriki katika mkutano huo, isipokuwa Chuo Kikuu kishiriki cha Jordan Morogoro,na Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Bugando ambavyo vilikosa uwakilishi.
Malisa ambaye alishinda urais wa SAUT kwa kishindo licha ya hujuma nyingi zilizofanywa dhidi yake, alikuwa Katibu Mwenezi wa Chadema (CHASO-SAUT) chuoni hapo, kabla ya kugombea Urais. Pia amewahi kuwa mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA wilaya ya Moshi Mjini.
Pamoja na kuwa kiongozi Malisa amekuwa mwanaharakati wa muda mrefu, ambapo makala zake nyingi zimekuwa zikiibua gumzo miongoni mwa jamii. Mwaka 2009 akiwa kidato cha sita alivamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa kichwani kwa panga, ikiwa ni siku chache tu baada ya makala yake kuchapwa gazeti la MwanaHalisi yenye kichwa MTOTO WA MKULIMA AMEANZA KUPOTEZA IMANI
Viongozi wengine waliochaguliwa katika mkutano huo ni Malima Silas (Mwenyekiti), Joseph Rufili (Makamu Mwenyekiti), Donath Salla (Naibu Katibu Mkuu) na Ephraim Kababaa (Mweka Hazina).