Malipo ya king'amuzi cha Dstv yanatisha

Kwanza unatakiwa ujue sio wote wanaolipia kwa dola, pili kwa wanaoangalia majumbani au wanaoonyesha bila kiingilio wanalipa 120,000/: na wanaotoza kiingilio wanalipia 180,000 kwa mwezi. Kama unataka risiti njoo nikuonyeshe.
Wote tunalipa kwa dola. Unapofika pale unaambiwa rate ya dola kwa siku hiyo ndio unatoa hayo madafu yako. Kwa nini serikali yetu imeshindwa kuwadhibiti hawa jamaa? Mbona kwenye mitandao ya simu imeweza? Mbaya zaidi ni kuwa hata usipofungua king'amuzi siku hiyo pesa bado inatafunwa tu. Anguko la shilingi yetu linachangiwa na mambo kama haya pia.
 
Star Times wao wanacheka tu, hamna lolote la maana Tv ya Taifa inashindwa kuonesha hata AFCON hii ni aibu sana. Dawa yao hawa DSTV ni kuwachakachua tu.
 
Star Times wao wanacheka tu, hamna lolote la maana Tv ya Taifa inashindwa kuonesha hata AFCON hii ni aibu sana. Dawa yao hawa DSTV ni kuwachakachua tu.

Tv ya Taifa ni ipi? Au unamaanisha ile ya Chama Tawala?
 
Gharama yake ni kubwa sana. Nimetazama film,ngapi,sijui,5.10,15,halafu wamekata connection. Na fedha hizo,si bora ninunue pirated dvd's mtaani?
 
Inategemea na sura yako......ukija kibosibosi bei inapanda.......lakini ni kama Tshs 100,000 hivi....ni PM nikupatie mmoja ila usije kumkamata tu.....manake watu wengine wanoko kwelikweli
Duh, hiyo bei ni ya kweli kaka??
Mi nilipigwa 400 but ilijumuisha na dish 2, decorder, waya, ufundi, faida nk
 
bora wamekuja Zuku TV inaweza ikaleta mabadiliko.

DSTV wanajiamini hakuna zaidi yao ndio sababu wanaamua kuweka kiwango cha malipo wanachotaka wao, dawa yao ni kuwachakachua tu, unalipa ela kidogo unajilipua mwaka mzima, shida hakuna.
 
UHURU WA KUPATA HABARI NI HAKI YA KIKATIBA, SIYO ANASA!!
Tunaelekea kwenye enzi za digitalia (ving'amuzi) enzi za analogia zimekwisha.
TCRA JITOKEZENI HADHARANI mtueleze mmejiandaje, mnatusaidiaje kutekeleza haki yetu ya uhuru wa
habari???? Tutanunua ving'amuzi vingapi ili kuona local channels??? Ni lini bei ya malipo ya ving'amuzi itashuka???
 
Dstv siku hizi kila kukicha wanapandisha gharama ya malipo ya king'amuzi chao, je kampuni hii imeshakuwa ya kifisadi? Kwa sasa malipo yamefikia shilingi 180,000/: kwa mwezi, huu c unyonyaji! Hawaoni kwamba tunawafanyia Kazi wao, ama kweli kaburu ni kaburu hata ukimpaka rangi habadiliki. Wadau nauliza hakuna mamlaka inayoweza kuzibiti unyonyaji huu?. Nawasilisha.

Ni kweli mkuu gharama zao ziko juu sana. Naungana na mmoja wa wachangiaji ya kwamba kwakua hawana mshindani, automatically they have control over the price. Nimekua mteja wao kwa miezi mingi, nakubali bila ubishi matangazo yao yana ubora, lakini it is very expensive. Ngoja tuwe na subra nadhani muda si mrefu huu ukiritimba utafikia ukingoni.
 
Inategemea na sura yako......ukija kibosibosi bei inapanda.......lakini ni kama Tshs 100,000 hivi....ni PM nikupatie mmoja ila usije kumkamata tu.....manake watu wengine wanoko kwelikweli

Hallow na mimi nahitaji huyo kishoka ni activate sijalipia muda mrefu walau ni fsidi AFCON maana timu yangu UK performance mbnofumbofu!
 
mm kuna mmoja alinimbia laki 4, loooh kumbe alitaka kunipiga duuu, naomba contact za wa kwako basi
 
Starehe gharama mkuu! Kama huna Pesa bora ukomae na channel za kwenye Antenna.
 
bora wamekuja Zuku TV inaweza ikaleta mabadiliko.

DSTV wanajiamini hakuna zaidi yao ndio sababu wanaamua kuweka kiwango cha malipo wanachotaka wao, dawa yao ni kuwachakachua tu, unalipa ela kidogo unajilipua mwaka mzima, shida hakuna.

tatizo zuku tv package zao hazijashiba kama hawa dstv maana dstv wako sawa na sky ya uk na ndio shareholders wao kwa kuhusu vitu vyao ingawa viko juu kazi kwelikweli kuwakimbia mkuu...
 
Dstv siku hizi kila kukicha wanapandisha gharama ya malipo ya king'amuzi chao, je kampuni hii imeshakuwa ya kifisadi? Kwa sasa malipo yamefikia shilingi 180,000/: kwa mwezi, huu c unyonyaji! Hawaoni kwamba tunawafanyia Kazi wao, ama kweli kaburu ni kaburu hata ukimpaka rangi habadiliki. Wadau nauliza hakuna mamlaka inayoweza kuzibiti unyonyaji huu?. Nawasilisha.

Yaah ni kweli kabisa hizi gharama ni za juu sana. labda tuwacheki hawa jamaa wapya wa ZUKU watakuja ni jipya gani labda kuwasheki hata kidogo hawa jamaa washtuke.
 
Dstv siku hizi kila kukicha wanapandisha gharama ya malipo ya king'amuzi chao, je kampuni hii imeshakuwa ya kifisadi? Kwa sasa malipo yamefikia shilingi 180,000/: kwa mwezi, huu c unyonyaji! Hawaoni kwamba tunawafanyia Kazi wao, ama kweli kaburu ni kaburu hata ukimpaka rangi habadiliki. Wadau nauliza hakuna mamlaka inayoweza kuzibiti unyonyaji huu?. Nawasilisha.

Kwani wamekulazimisha uwe mteja wao?
 
Acha Uzushi wewe Leo nimelipia Premium 125,000?= Acha kupotosha watu!
 
Back
Top Bottom