Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Taasisi ya kuzuia rushwa malawi ACB imekamata mali za aliekuwa RAIS WA MALAWI BAKILI MULUZI....kama dhamana katika kesi ya rushwa inayomkabili....hatua hiyo imechukuliwa wakati bado inaendelea na uchunguzi katika kesi hiyo ambayo muluzi anadaiwa kujiingizia zaidi ya doller million 11...,taasisi hiyo imesema wamkamata magari 44 kati ya 149 anayomiliki muluzi...na jumba alimokuwa anaishi lenye thamani ya mamilion ya fedha katika mji wa blantyre...vingine vilivyokamata ni jumba lake la biashara la KEZA OFFICE PARK...ambalo lilizinduliwa kwa mbwembwe za ajabu na aliekuwa rais wa tanzania FISADI BENJAMINI WILLIAM MKAPA..
na pia imesema imekamata account zake zote...afisa huyo amesema uchunguzi bado unaendelea kujiridhisha ili kuendelea kukamata mali zaidi...
Kwa taarifa hii Je kuna umuhimu wa kuwa na PCCB TANZANIA???
na pia imesema imekamata account zake zote...afisa huyo amesema uchunguzi bado unaendelea kujiridhisha ili kuendelea kukamata mali zaidi...
Kwa taarifa hii Je kuna umuhimu wa kuwa na PCCB TANZANIA???