Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Jirani zangu wawili ambao ni vijana kiumri wana watoto wachanga/wadogo. Wa kwanza aliwahi kuzalishwa na mtoto alipoanza kutembea akampost mkoa kwa babu zake. Yeye anakula raha tu kwa ninavyomwona. Ndio kwanza anasoma ile stail ya 2 in 1 ya sec. Wa pili ni binti yuko chuo kikuu. Ana bwanaake wanaishi wote. Nae anasoma ila sijui wapi. Hawa mtoto wao alipofikisha miezi 3 walimpost kwa bibi hapahapa dar kwa kisingizio cha shule. Malezi ya hawa watoto yanakuwaje? Swali langu ni kuwa kuna ulazima wa kukimbilia kuzaa wakati mambo mengine yamekubana? Tulijadili hili