Nna jirani yangu mwenye mtoto wa mwaka mmoja. Ye na mume wake wote wameajiriwa kwahiyo huwa wanamuacha mtoto na dada wa kazi.
Kitu cha kwanza kunotice ni kwamba siku mmoja wao akiwepo nyumbani mtoto halii lii sana.Mpaka kuna wakati hua nadhani labda wametoka kwa ukimya kumbe wapo. Ila wakiwa hawapo mtoto analia kila saa, na dada wa kazi full kumfokea na kumtisha kumpiga(pengine hua anafanya kweli).
Sasa juzi ndio alinichosha kabisa. Nilimkuta kakaa barazani alafu kamlaza yule mtoto juu ya miguu yake, kichwa kimegusa sakafu alafu anamnywesha uji. Uji mwingi unaishia chini na puani, mtoto analia, dada ni kelele tu "ntakupiga!!!"kwa wingi na kulalama kuhusu uji unaomwagika.
Sikusema neno ila leo nimefikiria weee nikaona kuwa mimi nisingependa mtoto wangu awe analishwa kwa style hiyo au kupigwa hata kufinywa na mtu yeyote yule katika umri huo. Sasa najiuliza kama nimweleze jirani namna mwanawe anavyokuwa treated akiwa hayupo au la. Kama jibu ni ndio, nianzeje????
Maoni tafadhali.
Kitu cha kwanza kunotice ni kwamba siku mmoja wao akiwepo nyumbani mtoto halii lii sana.Mpaka kuna wakati hua nadhani labda wametoka kwa ukimya kumbe wapo. Ila wakiwa hawapo mtoto analia kila saa, na dada wa kazi full kumfokea na kumtisha kumpiga(pengine hua anafanya kweli).
Sasa juzi ndio alinichosha kabisa. Nilimkuta kakaa barazani alafu kamlaza yule mtoto juu ya miguu yake, kichwa kimegusa sakafu alafu anamnywesha uji. Uji mwingi unaishia chini na puani, mtoto analia, dada ni kelele tu "ntakupiga!!!"kwa wingi na kulalama kuhusu uji unaomwagika.
Sikusema neno ila leo nimefikiria weee nikaona kuwa mimi nisingependa mtoto wangu awe analishwa kwa style hiyo au kupigwa hata kufinywa na mtu yeyote yule katika umri huo. Sasa najiuliza kama nimweleze jirani namna mwanawe anavyokuwa treated akiwa hayupo au la. Kama jibu ni ndio, nianzeje????
Maoni tafadhali.