Malecela avunja ukimya!

Invisible,

..tunaomba AUDIO CLIP tuweze kumsikiliza Mzee Cygwiyemwisi John Malecela.

..baada ya kumsikiliza ndipo tutaweza kutoa michango yenye tija.
 
Kuna taarifa kwamba wakati wowote ndani ya siku mbili hizi Mzee John Malecela anatarajiwa kutoa tamko zito ambalo linaweza kutikisa nchi na Chama cha Mapinduzi (CCM). Lakini pia tamko lake linaweza kuweka mambo sawa na kutoa mwelekeo.

Tunafuatilia.

hanishangazi kwa nini Humwita TINGA TINGA
 
Malecela alifanya kosa fulani baada ya mchakato wa 2005; alikuwa too royal kwa CCM. Mzee wa watu alifanyiwa mizengwe ya ajabu na CCM wakati ule huku akiwa ndiye mtu pekee aliyekuwa kaijenga CCM ile kwa mikono yake kuliko mtu mwingine yeyote aliyetaka kiti cha urais wakati ule. Jampo alilotakiwa kufanya wakati huo ni kuacha partisanship na kuchukua statesmanship roles zaidi. Leo hii angekuwa anaogopwa na hata akina JK.

CCM walifanya kosa kubwa sana kumwachia Malecela asiendelee kuwa Makamu mwenyekiti wa CCM.

Msekwa naona anayumba kweli kweli. Wewe angalia CCM hii, juu JK, kushoto Msekwa na kulia Makamba. Hakuna mtu hapo, bora wamrudishe tingatinga aanze kuswaga takataka zozote.
 
Jamani kila mtu fisadi nani msafi sasa.

Ametumia vizuri haki yake ya kikatiba ya uhuru wa kutoa maoni.

What is the problem?
 
Wanajamii I don't see anything hapa unless kama kuna habari zaidi.Aliyoyasema ni sawa na kasoma gazeti hakuna la kusisimua.I think mke wake yuko juu kisiasa ni vyema akaplay a background politics because of his age.Today people wanna see change ni vyema mzee wetu akarecruit someone and again his days in politics is over.

SAHIBA.
 
CCM walifanya kosa kubwa sana kumwachia Malecela asiendelee kuwa Makamu mwenyekiti wa CCM.

Msekwa naona anayumba kweli kweli. Wewe angalia CCM hii, juu JK, kushoto Msekwa na kulia Makamba. Hakuna mtu hapo, bora wamrudishe tingatinga aanze kuswaga takataka zozote.

Usisahau kuwa wakati wa Mkapa ndio alikuwa makamu mwenyekiti na EPA ilifanyika akiwa ni makomo. Hivyo ambacho angekifanya kama angekiwa makamo mpaka sasa ni kuhakikisha hizo taarifa za ufisadi wa EPA wananchi hawazipati. Huko ndio kuswaga mnakokutaka?
 
Uhuru wa maoni ni ibara namba ngapi vile?

Ibara ya 18 & 19; na Ibara ya 20 ni uhuru wa kushirikiana na wengine (right of association)!!! na sheria zinazohusiana ni

Uhuru wa Maoni Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 na Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1992 Na.4 ib…


Nawasilisha!!!

Haki ya Uhuru wa Mawazo


18
.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru

kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta,


kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo

chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu
matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu
kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.









19



.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani

na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu


kubadilisha dini au imani yake.

(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya
Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza
dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na
shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya
shughuli za mamlaka ya nchi.
(3) Kila palipotajwa neno "dini" katika ibara hii ifahamike
kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na
maneno mengineyo yanayofanana au kuambatana na neno hilo
nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo.


 
Malecela ni yule aliyewahi kubadili jina na kuitwa jumanne akapewa magari zaidi ya 64 kwa ajili ya kampeni na waarabu. nakumbuka nyerere alimwambia John ukisha kuwa raisi utalipajie hiyo mali. Mwalimu akamwambia Ali akimpitisha Jumanne atampigia mrema debe.
CCM ni dampo kweli hata aongee nani dampo limeoza linatoa funza hakuna wa kumsikiliza.Hana jipya ana hasira ya kunyimwa ulaji yeye na kilango.

There is an inherent connotation that when you say "atampigia Mrema debe" unaongelea urais.

Nyerere hakuwahi kusema on record kwamba atampigia Mrema debe urais, alichosema ni kwamba alimshauri Mrema agombee ubunge na aache kugombea urais, na yeye Nyerere yuko tayari kumpigia Mrema kampeni ya ubunge, which to me was like saying Mrema's leadership calibre to Nyerere was not presidential, but parliamentalian.

Ningefurahi kuelimishwa juu ya Nyerere alisema lini na kwenye chombo gani kwamba akipitishwa Malecela yeye Nyerere atampigia Mrema kampeni ya urais.
 
Mtanzania, Malecela ni Mgogo. Ili uweze kuishi Dodoma, inabidi uwe Mvumilivu sana. Wagoggo AKA AGWE, wana kauvimilivu sana. Wao huwa hawana maneno maneno kama sisi/nyinyi. Hata wakoloni hapo walipita tu bila kupata matatizo yoyote. Ukichunguza sana unakubali kuwa Wagogo ni Wazaramo walioenda Dodoma kuchukua Mbuzi wa Arobaini........ mengine yatakuja endelea.

... huenda ni kweli Chief Mangungo alikuwa ni mgogo eeh, shanga tu ambazo hata hakujua ni za kazi gani zilitosha kuuza nchi yake na watu wake!!
 
This country has gone to the DOGS believe me my Dear Wadanganyika

Join Date: Wed Feb 2009
Posts: 1
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif

Credits: 279

Hii haijakaa vizuri!!! Karibu basi kwenye jamvi ingawa hujapiga hodi! Du! hizi sio mila zetu au uongo waTanzania?
 
Mzee Malecela kama kawaida yake atakuwa katikati kujaribu kuweka mambo sawa.

Huyu mzee pamoja na kufanyiwa fouls zote na CCM lakini hakupiga kelele za kuonewa.

Anajijua si safi ndiyo maana pamoja na rafu alizochezewa ameamua kukaa kimya maana akitoa kauli ya kuwagusa wana mtandao basi wanaweza kummaliza kabisa.
 
Mbona heading imebadilika kutoka tetesi kuwa Breaking News lakini mpaka sasa sijaona jipya?? Au ndiyo kusema tumeingizwa mjini???
 
Which reminds me, aliwahi kuwajibu watu waliokuwa wanalalamikIa usafiri wa kwenda Kigoma miaka ya 80 alipokuwa waziri wa mawasiliano kwamba "THEY CAN GO TO HELL", na sisi tumjibu hivyohivyo ?

hapana.
tukitaka kushinda vita dhidi ya ufisad ni lazima tuwashirikishe hata waliokuwa wanakosea zamani. na hima hima tuwahimize wakemee ufisad

hiyo ni muhimu moja kwa sababu karibu wengi (kama sio wote) waliokuwa viongoz wana matatizo ya hapa na pale. ndio waliotufikisha hapa. lakin tusipoungana nao leo kupambana na ufisadi wa sasa tukataka kupigana peke yetu hatutoshinda

bado wakiongea sauti zao nzito kuliko wengi wetu humu. bado wanaushawishi mkubwa kwa wananchi na viongoz waliopo madarakan

watusaidie kupigana leo. wala tusiwadhihaki. lakin tunajua walikosea jana
 
KLHN Wire

Mbunge wa Mtera Mhe. John S. C Malecela amevunja ukimya wake wa muda mrefu na kuzungumza na waandishi leo hii kuhusu masuala mbalimbali yakitaifa hususan hali ya kisiasa ndani ya chama hicho, bungeni na katika hadhara ya Watanzania. Mzee Malecela ambaye amewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM (Bara) amefanya hivyo leo nyumbani kwake na kufanya kile ambacho watu wengi walikuwa wanajiuliza msimamo wa mzee huyo katika hali ya mgongano wa kisiasa unaoendelea ndani ya CCM. Akizungumza mbele ya vyombo vichache vya habari ambavyo alivikubalia kuwepo, Mzee Malecela alijadili kwa kirefu kuhusu malumbano yanayoendelea nchini hususan kati ya wana CCM. Akionekana kuzungumzia mgongano kati ya kambi ya Mwakyembe na ile ya Rostam katika sakata la Richmond/Dowans na mjadala wa mgongano wa maslahi mzee Malecela alisema kuwa malumbano hayo ni ya kipuuzi, hayana wala ufanisi kwa taifa.

Alielezea kushangazwa kwake na malumbano hayo kati ya wana CCM kwani wanavyovyombo vya kutosha kabisa kuzungumzia tofauti zao au hoja zao kuliko wanavyofanya sasa kupitia magazetini. Alitaja baadhi ya vyombo ambavyo anaamini vingeweza kutumika kuwa ni pamoja na vikao vya chama, Bunge, na taratibu za serikali.

Mzee Malecela amesema ameamua kuzungumza kama Mjumbe wa Kudumu wa Kamati Kuu ya CCM na miongoni mwa wazee wa CCM ambao wanasauti katika chama hicho. Amesema kuwa endapo malumbano hayo yataendelea basi ataenda hatua mbele zaidi ya kuzungumza kwenye vikao vya chama akitahadharisha kuwa CCM haitosita kumtimua mtu yeyote ambaye chama kinaona haendani nacho. Alitoa mifano ya huko nyuma jinsi CCM ilivyoshughulikia uasi ndani ya CCM ambapo baadhi ya viongozi wake (wabunge) walichukuliwa hatua.

Akikumbushia maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuwa "upinzani madhubuti utatoka CCM" mzee Malecela aliwahakikishia wananchi kuwa bado CCM kina muda mrefu wa kutawala na hakuna mtu au kikundi ambacho kinaweza kutoka na kusababisha chama hicho kumeguka.

Japo alijaribu kukwepa kuzungumzia suala la kashfa ya Richmond/Dowans moja kwa moja au kumtaja mtu yeyote kwa jina Mzee Malecela alisema kuwa kuendelea kuzungumzia suala la Dowans wakati serikali, tanesco na wizara wameshatoa msimamo wao ni sawa na "kuuchapa viboko mzoga wa mbwa". Alisema kuwa kama kuna mtu yeyote mwenye jambo ambalo anataka lizungumzwe basi lizunguzwe kwenye Bunge au vikao vya chama.

Yeye naye kama alivyofanya Dr. Mwakyembe karibu wiki moja iliyopita alivilaumu baadhi ya vyombo vya habari kuwa vinatumiwa na baadhi ya watu kwa maslahi yao na ameoneshwa kukerwa na ubora wa vyombo vya habari. Alionesha kutokufurahishwa na utitiri wa vyombo vya habari ambavyo vinatumia pia nafasi yao katika jamii kurushiana matusi hata yale "ya nguoni". Alisema haitoshi tu kuwa na wingi wa vyombo vya habari bali ni lazima viwe na maadili na vinavyofanya kazi kwa kanuni zinazoeleweka. Alitoa wito kwa Wizara ya Habari kuingilia kati hali hii iliyojitokeza ambayo kwa kiasi kikubwa alionesha wazi kukerwa nayo.

Alipoulizwa kuhusu mipango yake ya kisiasa ya baadaye na hasa kama ataingia tena katika kinyang'anyiro cha kugombea Urais Mzee Malecela alisema kuwa imekuwa ni utamaduni ndani ya CCM kwa Rais aliyeko madarakani kuachwa kukamilisha vipindi viwili vinavyoruhusiwa kikatiba na hivyo mpango huo kwake kwa mwakani haupo.

Hata hivyo ameonesha nia ya kuendelea kiti chake cha Jimbo la Mtera.
 
KLHN Wire



Alipoulizwa kuhusu mipango yake ya kisiasa ya baadaye na hasa kama ataingia tena katika kinyang'anyiro cha kugombea Urais Mzee Malecela alisema kuwa imekuwa ni utamaduni ndani ya CCM kwa Rais aliyeko madarakani kuachwa kukamilisha vipindi viwili vinavyoruhusiwa kikatiba na hivyo mpango huo kwake kwa mwakani haupo. Hata hivyo alionesha kuwa ana mpango wa kuendelea kulitetea jimbo lake la Mtera ambalo ameliongoza kwa karibu miaka 40 sasa.

Naanza kukubaliana na waliosema hana jipya. Utaratibu my a.. Siasa za kiafrika taabu kwelikweli yaani hata kama mtu kaharibu basi kwa sababu tu sisiemu wamemweka utaratibu wa kijinga, kishenzi, kipumbavu,kiuendawazimu, kizandiki na anything you can name basi tukubali tu
I miss Nyani Ngabu but I'll quote him "MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO"
 
The folly of this laughably obsolette and monopolistic obfuscating Ottoman-like ombudsmanship is in the non-realization of the time we live in.

Can they really say this after Mkapa's call for "Uwazi na Ukweli"?
 
Hivi kweli kuna mwanachama yeyote wa JF aliyetegemea jipya kutoka kwa huyo mzee John Samwel Malecela (ex- Waziri, balozi na Waziri Mkuu). Kweli watanzania tuna safari ndefu - kama fisi tutabaki kumfuata binadamu huku mate yakitudondoka tukiusubiri mkono udondoke. Naona wengi hawaijui CCM - ina wenyewe !!
 
Huyu Mzee hana jipya, naona amejaribu kusimama kwenye fence aone upepo unelekea wapi lakini wengine tunaona zama zake zimeshapita!
 
Back
Top Bottom